Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 40
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Zaburi—Yaliyomo

      • Kumshukuru Mungu asiyeweza kulinganishwa na yeyote

        • Kazi za Mungu ni nyingi sana zisiweze kusimuliwa (5)

        • Dhabihu si jambo kuu kwa Mungu (6)

        • “Ninafurahia kufanya mapenzi yako” (8)

Zaburi 40:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Nilimngojea Yehova kwa subira.”

  • *

    Au “akainama chini ili kunisikiliza, akasikia.”

Marejeo

  • +Zb 34:15

Zaburi 40:3

Marejeo

  • +Zb 33:3; 98:1

Zaburi 40:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “waongo.”

Zaburi 40:5

Marejeo

  • +Ufu 15:3
  • +Kut 15:11
  • +Zb 139:17, 18

Zaburi 40:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Hukupendezwa na.”

Marejeo

  • +1Sa 15:22; Zb 51:16, 17; Ho. 6:6
  • +Isa 50:5
  • +Ebr 10:5-9

Zaburi 40:7

Marejeo

  • +Lu 24:44

Zaburi 40:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ninatamani.”

Marejeo

  • +Yoh 4:34
  • +Zb 37:31; Ro 7:22

Zaburi 40:9

Marejeo

  • +Zb 22:22
  • +Ebr 13:15

Zaburi 40:10

Marejeo

  • +Ebr 2:12

Zaburi 40:11

Marejeo

  • +Zb 61:6, 7

Zaburi 40:12

Marejeo

  • +Zb 71:20
  • +Zb 38:4

Zaburi 40:13

Marejeo

  • +Zb 25:17
  • +Zb 38:22; 70:1-5

Zaburi 40:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wanaoitafuta nafsi yangu.”

Zaburi 40:16

Marejeo

  • +Kum 4:29
  • +Zb 13:5
  • +Zb 35:27

Zaburi 40:17

Marejeo

  • +Zb 54:4; Isa 50:7; Ebr 13:6
  • +Zb 143:7

Jumla

Zab. 40:1Zb 34:15
Zab. 40:3Zb 33:3; 98:1
Zab. 40:5Ufu 15:3
Zab. 40:5Kut 15:11
Zab. 40:5Zb 139:17, 18
Zab. 40:61Sa 15:22; Zb 51:16, 17; Ho. 6:6
Zab. 40:6Isa 50:5
Zab. 40:6Ebr 10:5-9
Zab. 40:7Lu 24:44
Zab. 40:8Yoh 4:34
Zab. 40:8Zb 37:31; Ro 7:22
Zab. 40:9Zb 22:22
Zab. 40:9Ebr 13:15
Zab. 40:10Ebr 2:12
Zab. 40:11Zb 61:6, 7
Zab. 40:12Zb 71:20
Zab. 40:12Zb 38:4
Zab. 40:13Zb 25:17
Zab. 40:13Zb 38:22; 70:1-5
Zab. 40:16Kum 4:29
Zab. 40:16Zb 13:5
Zab. 40:16Zb 35:27
Zab. 40:17Zb 54:4; Isa 50:7; Ebr 13:6
Zab. 40:17Zb 143:7
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Zaburi 40:1-17

Zaburi

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.

40 Nilimtumaini Yehova kwa bidii,*

Naye akanitegea sikio lake na kusikia* kilio changu cha kuomba msaada.+

 2 Akanipandisha kutoka katika shimo linalonguruma,

Kutoka katika matope yenye utelezi.

Akaiweka miguu yangu juu ya jabali;

Akanifanya nisimame mahali palipo imara.

 3 Kisha akaweka wimbo mpya kinywani mwangu,+

Asifiwe Mungu wetu.

Wengi watatazama kwa hofu

Na kumtumaini Yehova.

 4 Mwenye furaha ni mtu anayemtumaini Yehova

Na ambaye hawatumaini wakaidi au watu wadanganyifu.*

 5 Jinsi ulivyotenda mambo mengi sana,

Ee Yehova Mungu wangu,

Kazi zako zinazostaajabisha na mawazo yako kutuelekea.+

Hakuna yeyote anayeweza kulinganishwa nawe;+

Ikiwa ningejaribu kusimulia na kuongea kuzihusu,

Zingekuwa nyingi sana kwangu kusimulia!+

 6 Hukutamani* dhabihu na toleo,+

Lakini ulifungua masikio yangu ili yasikie.+

Hukuomba dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za dhambi.+

 7 Kisha nikasema: “Tazama, nimekuja.

Katika kitabu cha kukunjwa imeandikwa kunihusu.+

 8 Ee Mungu wangu, ninafurahia* kufanya mapenzi yako,+

Na sheria yako imo ndani yangu kabisa.+

 9 Ninatangaza habari njema ya uadilifu katika kutaniko kubwa.+

Tazama! Siizuii midomo yangu,+

Ee Yehova, kama unavyojua vema.

10 Siufuniki uadilifu wako moyoni mwangu.

Ninatangaza uaminifu wako na wokovu wako.

Siufichi upendo wako mshikamanifu na ukweli wako katika kutaniko kubwa.”+

11 Ee Yehova, usininyime rehema yako.

Upendo wako mshikamanifu na ukweli wako na unilinde daima.+

12 Misiba inayonizunguka ni mingi sana haihesabiki.+

Makosa yangu mengi yananilemea hivi kwamba siwezi kuona njia yangu;+

Ni mengi sana kuliko nywele za kichwa changu,

Nami nimevunjika moyo.

13 Tafadhali, Ee Yehova, uwe tayari kuniokoa.+

Ee Yehova, njoo haraka unisaidie.+

14 Wote wanaotaka kuniua*

Na waaibishwe na kufedheheshwa.

Wale wanaofurahia msiba wangu

Na wakimbie kwa aibu.

15 Wale wanaoniambia: “Aha! Aha!”

Na washtuke kwa sababu ya aibu yao.

16 Lakini acha wale wanaokutafuta+

Wafurahi na kushangilia kwa sababu yako.+

Wale wanaopenda matendo yako ya wokovu na waseme daima:

“Yehova na atukuzwe.”+

17 Lakini sina uwezo, nami ni maskini;

Yehova na anitunze.

Wewe ni msaidizi wangu na mwokozi wangu;+

Mungu wangu, usikawie.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki