Zaburi
149 Msifuni Yah!*
2 Watu wa Israeli na washangilie kwa sababu ya Muumba wao Mkuu;+
Wana wa Sayuni na washangilie kwa sababu ya Mfalme wao.
4 Kwa maana Yehova anawafurahia watu wake.+
Anawapamba wapole kwa wokovu.+
5 Washikamanifu na washangilie kwa utukufu;
Na wapaze sauti kwa shangwe vitandani mwao.+
6 Nyimbo zinazomsifu Mungu na ziwe kooni mwao,
Na upanga wenye makali pande mbili uwe mkononi mwao,
7 Ili kuyalipiza kisasi mataifa
Na kuyaadhibu mataifa,
8 Ili kuwafunga wafalme wao kwa pingu
Na viongozi wao kwa pingu za chuma,
9 Ili kutekeleza hukumu iliyoandikwa kuwahusu.+
Heshima hii ni ya washikamanifu wake wote.
Msifuni Yah!*