Methali
22 Ni afadhali kuchagua jina jema* kuliko mali nyingi;+
Kuheshimiwa* ni bora kuliko fedha na dhahabu.
2 Matajiri na maskini wanafanana katika jambo hili:*
Yehova aliwaumba wote.+
3 Mtu mwerevu huona hatari na kujificha,
Lakini wajinga husonga mbele na kupata madhara.*
4 Unyenyekevu na kumwogopa Yehova huleta
Utajiri na utukufu na uzima.+
5 Miiba na mitego iko kwenye njia ya mtu aliyepotoka,
7 Tajiri humtawala maskini,
Na mkopaji ni mtumwa wa mkopeshaji.+
11 Mtu anayependa moyo safi na ambaye husema maneno yenye fadhili
Atakuwa rafiki ya mfalme.+
12 Macho ya Yehova huulinda ujuzi,
Lakini Yeye huyapindua maneno ya wenye hila.+
13 Mvivu anasema: “Kuna simba nje!
Nitauawa katikati ya uwanja wa jiji!”+
14 Kinywa cha wanawake waliopotoka* ni shimo refu.+
Anayeshutumiwa na Yehova ataanguka ndani yake.
16 Anayempunja maskini ili aongeze mali yake+
Na yule anayewapa zawadi matajiri
Mwishowe watakuwa maskini.
17 Tega sikio lako usikie maneno ya wenye hekima,+
Ili uufanye moyo wako uzingatie ujuzi wangu,+
18 Kwa maana inapendeza kuyahifadhi ndani yako kabisa,+
Ili yote yawe midomoni mwako daima.+
19 Ili umtegemee Yehova,
Ninakupa ujuzi leo.
20 Je, tayari sijakuandikia,
Na kukupa mashauri na ujuzi,
21 Ili nikufundishe maneno ya kweli yanayotegemeka,
Uweze kumpelekea habari sahihi yule aliyekutuma?
22 Usimwibie mtu maskini kwa kuwa ni maskini,+
Wala usimkandamize mtu wa hali ya chini katika lango la jiji,+
23 Kwa maana Yehova mwenyewe atawatetea+
Naye atawaangamiza wanaowapunja.
24 Usiwe na urafiki na mtu mwenye hasira kali
Wala kushirikiana na mtu anayekasirika upesi,
25 Ili usijifunze kamwe njia zake
Na kujitia mtegoni.+
26 Usiwe miongoni mwa wale wanaopeana mikono wanapotoa dhamana,
Wanaoweka dhamana kwa ajili ya mikopo.+
27 Ikiwa huna kitu cha kulipa,
Kitanda chako kitavutwa na kuchukuliwa ukiwa umekilalia!
28 Usiisogeze alama ya kale ya mpaka
Iliyowekwa na mababu zako.+
29 Je, umemwona mtu aliye stadi katika kazi yake?
Atasimama mbele ya wafalme;+
Hatasimama mbele ya watu wa kawaida.