Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 35
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Mwanzo—Yaliyomo

      • Yakobo aondoa miungu ya kigeni (1-4)

      • Yakobo arudi Betheli (5-15)

      • Benjamini azaliwa; Raheli afa (16-20)

      • Wana 12 wa Israeli (21-26)

      • Kifo cha Isaka (27-29)

Mwanzo 35:1

Marejeo

  • +Mwa 28:19; 31:13
  • +Mwa 27:42-44

Mwanzo 35:2

Marejeo

  • +Mwa 31:19; Kum 5:7; Yos 23:7; 1Ko 10:14

Mwanzo 35:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “katika njia niliyotembea.”

Marejeo

  • +Mwa 28:13, 15; 31:42

Mwanzo 35:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “akavificha.”

Mwanzo 35:6

Marejeo

  • +Mwa 28:19

Mwanzo 35:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Maana yake “Mungu wa Betheli.”

Marejeo

  • +Mwa 28:20-22

Mwanzo 35:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Maana yake “Mwaloni wa Kilio.”

Marejeo

  • +Mwa 24:59

Mwanzo 35:10

Marejeo

  • +Mwa 25:26; 27:36
  • +Mwa 32:28

Mwanzo 35:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “watatoka katika kiuno chako.”

Marejeo

  • +Mwa 17:1; Kut 6:3; Ufu 15:3
  • +Mwa 48:3, 4
  • +Mwa 17:5, 6; Yoh 12:13

Mwanzo 35:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mbegu yako.”

Marejeo

  • +Mwa 15:18; Kum 34:4

Mwanzo 35:14

Marejeo

  • +Mwa 28:18

Mwanzo 35:15

Marejeo

  • +Mwa 28:19

Mwanzo 35:17

Marejeo

  • +Mwa 30:22-24

Mwanzo 35:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Maana yake “Mwana wa Maombolezo Yangu.”

  • *

    Maana yake “Mwana wa Mkono wa Kulia.”

Marejeo

  • +Mwa 46:21; 49:27; Kum 33:12

Mwanzo 35:19

Marejeo

  • +Mwa 48:7; Mik 5:2; Mt 2:6

Mwanzo 35:22

Marejeo

  • +Mwa 49:3, 4; 1Nya 5:1

Mwanzo 35:23

Marejeo

  • +Mwa 49:3

Mwanzo 35:27

Marejeo

  • +Mwa 31:17, 18
  • +Mwa 15:13; Ebr 11:9

Mwanzo 35:28

Marejeo

  • +Mwa 25:20, 26

Mwanzo 35:29

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Akakusanywa kwa watu wake.” Huu ni msemo wa kishairi unaorejelea kifo.

  • *

    Tnn., “akiwa amezeeka na akiwa amejaa siku.”

Marejeo

  • +Mwa 49:30, 31

Jumla

Mwa. 35:1Mwa 28:19; 31:13
Mwa. 35:1Mwa 27:42-44
Mwa. 35:2Mwa 31:19; Kum 5:7; Yos 23:7; 1Ko 10:14
Mwa. 35:3Mwa 28:13, 15; 31:42
Mwa. 35:6Mwa 28:19
Mwa. 35:7Mwa 28:20-22
Mwa. 35:8Mwa 24:59
Mwa. 35:10Mwa 25:26; 27:36
Mwa. 35:10Mwa 32:28
Mwa. 35:11Mwa 17:1; Kut 6:3; Ufu 15:3
Mwa. 35:11Mwa 48:3, 4
Mwa. 35:11Mwa 17:5, 6; Yoh 12:13
Mwa. 35:12Mwa 15:18; Kum 34:4
Mwa. 35:14Mwa 28:18
Mwa. 35:15Mwa 28:19
Mwa. 35:17Mwa 30:22-24
Mwa. 35:18Mwa 46:21; 49:27; Kum 33:12
Mwa. 35:19Mwa 48:7; Mik 5:2; Mt 2:6
Mwa. 35:22Mwa 49:3, 4; 1Nya 5:1
Mwa. 35:23Mwa 49:3
Mwa. 35:27Mwa 31:17, 18
Mwa. 35:27Mwa 15:13; Ebr 11:9
Mwa. 35:28Mwa 25:20, 26
Mwa. 35:29Mwa 49:30, 31
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Mwanzo 35:1-29

Mwanzo

35 Baada ya hayo Mungu akamwambia Yakobo: “Ondoka, nenda Betheli+ ukaishi huko, na unijengee madhabahu mimi Mungu wa kweli, niliyekutokea ulipokuwa ukimkimbia ndugu yako Esau.”+

2 Basi Yakobo akawaambia watu wa nyumba yake na wote waliokuwa pamoja naye: “Ondoeni kabisa miungu ya kigeni iliyo kati yenu,+ na mjisafishe wenyewe na kubadili mavazi yenu, 3 na acheni tuondoke twende Betheli. Huko nitamjengea madhabahu Mungu wa kweli, aliyenijibu katika siku yangu ya taabu na ambaye amekuwa pamoja nami kila mahali nilipoenda.”*+ 4 Basi wakampa Yakobo miungu yote ya kigeni waliyokuwa nayo na vipuli walivyovaa masikioni, kisha Yakobo akavifukia* chini ya mti mkubwa uliokuwa karibu na Shekemu.

5 Walipokuwa wakisafiri, hofu ya Mungu iliyakumba majiji yaliyowazunguka, kwa hiyo wakaaji wake hawakuwafuatia wana wa Yakobo. 6 Hatimaye Yakobo akafika Luzi,+ yaani, Betheli, katika nchi ya Kanaani, pamoja na watu wote waliokuwa naye. 7 Akajenga madhabahu huko na kupaita mahali hapo El-betheli,* kwa sababu Mungu wa kweli alikuwa amemtokea mahali hapo alipomkimbia ndugu yake.+ 8 Baadaye Debora,+ mlezi wa Rebeka, akafa na kuzikwa chini ya mwaloni karibu na Betheli. Basi akauita mwaloni huo Alon-bakuthi.*

9 Mungu akamtokea Yakobo tena alipokuwa akitoka Padan-aramu, akambariki. 10 Mungu akamwambia: “Jina lako ni Yakobo.+ Hutaitwa tena Yakobo, jina lako litakuwa Israeli.” Naye akaanza kumwita Israeli.+ 11 Mungu akaendelea kumwambia: “Mimi ni Mungu Mweza-Yote.+ Zaa uwe na watoto wengi. Mataifa na kusanyiko la mataifa litatoka kwako,+ na wafalme watatoka kwako.*+ 12 Na nchi niliyompa Abrahamu na Isaka, nitakupa wewe na uzao wako* baada yako.”+ 13 Kisha Mungu akapanda na kumwacha mahali alipoongea naye.

14 Basi Yakobo akasimamisha nguzo mahali hapo alipoongea naye, nguzo ya mawe, naye akamimina toleo la kinywaji juu yake na pia akamimina mafuta juu yake.+ 15 Na Yakobo akaendelea kupaita mahali hapo ambapo Mungu alikuwa ameongea naye, Betheli.+

16 Kisha wakaondoka Betheli. Na walipokuwa umbali fulani kabla ya kufika Efrathi, Raheli akaanza kuzaa, na uchungu wa kuzaa ulikuwa mkali sana. 17 Lakini alipokuwa aking’ang’ana kuzaa, mkunga akamwambia: “Usiogope, kwa maana utamzaa mwana huyu pia.”+ 18 Uhai wake ulipokuwa ukitoka (kwa kuwa alikuwa akifa), akamwita mwana huyo Ben-oni,* lakini baba yake akamwita Benjamini.*+ 19 Kwa hiyo Raheli akafa na kuzikwa njiani kuelekea Efrathi, yaani, Bethlehemu.+ 20 Yakobo akasimamisha nguzo juu ya kaburi lake; hiyo ndiyo nguzo ya kaburi la Raheli mpaka leo hii.

21 Kisha Israeli akaendelea na safari na kupiga hema lake umbali fulani mbele ya mnara wa Ederi. 22 Siku moja, Israeli alipokuwa akiishi katika nchi hiyo, Rubeni alienda na kulala na Bilha suria wa baba yake, naye Israeli akasikia habari hizo.+

Basi Yakobo alikuwa na wana 12. 23 Wana wa Lea walikuwa Rubeni,+ mzaliwa wa kwanza wa Yakobo, kisha Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, na Zabuloni. 24 Wana wa Raheli walikuwa Yosefu na Benjamini. 25 Na wana wa Bilha kijakazi wa Raheli walikuwa Dani na Naftali. 26 Na wana wa Zilpa kijakazi wa Lea walikuwa Gadi na Asheri. Hao ndio wana wa Yakobo waliozaliwa Padan-aramu.

27 Hatimaye Yakobo akafika mahali ambapo Isaka baba yake alikuwa kule Mamre,+ Kiriath-arba, yaani, Hebroni, ambako Abrahamu na pia Isaka waliishi wakiwa wageni.+ 28 Isaka aliishi miaka 180.+ 29 Kisha Isaka akakata pumzi na kufa, akazikwa pamoja na watu wake,* baada ya kuishi maisha marefu na yenye kuridhisha;* na Esau na Yakobo wanawe wakamzika.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki