Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 6
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Isaya—Yaliyomo

      • Maono ya Yehova katika hekalu lake (1-4)

        • “Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu ni Yehova” (3)

      • Midomo ya Isaya yasafishwa (5-7)

      • Isaya atumwa (8-10)

        • “Mimi hapa! Nitume mimi!” (8)

      • “Ni mpaka lini, Ee Yehova?” (11-13)

Isaya 6:1

Marejeo

  • +2Nya 26:23
  • +1Fa 22:19; Da 7:9

Isaya 6:3

Marejeo

  • +Kut 15:11; Ufu 4:8

Isaya 6:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “sauti ya yule aliyekuwa akiita.”

Marejeo

  • +Ufu 15:8

Isaya 6:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “nimenyamazishwa.”

Marejeo

  • +Isa 29:13

Isaya 6:6

Marejeo

  • +Eze 10:2
  • +Ufu 8:5

Isaya 6:8

Marejeo

  • +Mwa 1:26; Yoh 1:1, 2; 12:41
  • +Zb 110:3; Mt 4:19, 20

Isaya 6:9

Marejeo

  • +Yer 5:21; Mt 13:14, 15; Lu 8:9, 10; Mdo 28:25-27

Isaya 6:10

Marejeo

  • +Eze 3:7
  • +Yer 6:10; Yoh 3:20

Isaya 6:11

Marejeo

  • +2Nya 36:20, 21; Isa 3:26; 24:1

Isaya 6:12

Marejeo

  • +2Fa 25:11

Isaya 6:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “uzao mtakatifu utakuwa.”

Jumla

Isa. 6:12Nya 26:23
Isa. 6:11Fa 22:19; Da 7:9
Isa. 6:3Kut 15:11; Ufu 4:8
Isa. 6:4Ufu 15:8
Isa. 6:5Isa 29:13
Isa. 6:6Eze 10:2
Isa. 6:6Ufu 8:5
Isa. 6:8Mwa 1:26; Yoh 1:1, 2; 12:41
Isa. 6:8Zb 110:3; Mt 4:19, 20
Isa. 6:9Yer 5:21; Mt 13:14, 15; Lu 8:9, 10; Mdo 28:25-27
Isa. 6:10Eze 3:7
Isa. 6:10Yer 6:10; Yoh 3:20
Isa. 6:112Nya 36:20, 21; Isa 3:26; 24:1
Isa. 6:122Fa 25:11
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Isaya 6:1-13

Isaya

6 Katika mwaka ambao Mfalme Uzia alikufa,+ nilimwona Yehova akiwa ameketi kwenye kiti cha ufalme kilicho juu na kilichoinuliwa,+ na pindo za kanzu yake zilijaa hekaluni. 2 Maserafi walikuwa wamesimama juu yake; kila mmoja wao alikuwa na mabawa sita. Kila mmoja aliufunika uso wake kwa mabawa mawili na alifunika miguu yake kwa mawili, na kila mmoja wao aliruka huku na huku kwa mawili.

 3 Na kila mmoja alimwambia mwenzake:

“Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu ni Yehova wa majeshi.+

Dunia yote imejaa utukufu wake.”

4 Na viegemeo vya milango vikatetemeka kwa sababu ya ile sauti kubwa,* na nyumba ikajaa moshi.+

 5 Kisha nikasema: “Ole wangu!

Kwa maana ni kama nimekufa,*

Kwa maana mimi ni mtu asiye na midomo safi,

Nami ninaishi kati ya watu wasio na midomo safi;+

Kwa maana macho yangu yamemwona Mfalme, Yehova wa majeshi mwenyewe!”

6 Ndipo mmoja wa maserafi akaruka kunijia, na mkononi mwake alikuwa na kaa linalowaka+ alilokuwa amechukua kwa koleo kutoka kwenye madhabahu.+ 7 Akakigusa kinywa changu na kusema:

“Tazama! Hili limeigusa midomo yako.

Hatia yako imeondolewa,

Na dhambi yako imefunikwa.”

8 Kisha nikasikia sauti ya Yehova ikiuliza: “Nimtume nani, na ni nani atakayeenda kwa ajili yetu?”+ Nami nikasema: “Mimi hapa! Nitume mimi!”+

 9 Ndipo akasema, “Nenda, uwaambie hivi watu hawa:

‘Mtasikia tena na tena,

Lakini hamtaelewa;

Mtaona tena na tena,

Lakini hamtapata ujuzi wowote.’+

10 Ufanye moyo wa watu hawa uwe mgumu,+

Yafanye masikio yao yawe mazito,+

Na uyafunge kabisa macho yao,

Ili wasione kwa macho yao

Na wasisikie kwa masikio yao,

Ili moyo wao usielewe

Nao wasigeuke na kuponywa.”

11 Ndipo nikauliza: “Ni mpaka lini, Ee Yehova?” Kisha akasema:

“Mpaka majiji yabomoke yawe magofu bila mkaaji

Na nyumba zisiwe na watu

Na nchi iharibiwe na kubaki ukiwa;+

12 Mpaka Yehova awaondoe watu na kuwapeleka mbali+

Na hali ya ukiwa ya nchi ienee sana.

13 “Lakini bado kutakuwa na sehemu ya kumi ndani yake, nayo itateketezwa tena, kama mti mkubwa na kama mwaloni, ambayo inapokatwa huacha kisiki; mbegu takatifu itakuwa* kisiki chake.”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki