Methali
26 Kama theluji wakati wa kiangazi na mvua wakati wa mavuno,
Ndivyo heshima isivyomfaa mpumbavu.+
2 Kama ndege alivyo na sababu ya kukimbia na mbayuwayu kuruka,
Ndivyo laana isivyokuja bila sababu nzuri.*
4 Usimjibu mpumbavu kulingana na ujinga wake,
Ili usiwe kama yeye.*
5 Mjibu mpumbavu kulingana na ujinga wake,
Ili asifikiri kwamba ana hekima.+
6 Kama mtu anayeilemaza miguu yake na kujidhuru mwenyewe*
Ndivyo alivyo mtu anayemkabidhi mambo mpumbavu.
8 Kama jiwe linavyofungwa kwenye kombeo,
Ndivyo ilivyo kumpa utukufu mtu mpumbavu.+
9 Kama mmea wa miiba mkononi mwa mlevi,
Ndivyo ilivyo methali kinywani mwa watu wapumbavu.
10 Kama mpiga mishale anayemjeruhi yeyote yule,*
Ndivyo alivyo mtu anayemwajiri mpumbavu au wapita njia.
11 Kama mbwa anayerudia matapishi yake,
Ndivyo mpumbavu anavyorudia ujinga wake.+
12 Je, umemwona mtu anayefikiri ana hekima?+
Kuna tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwa mtu huyo.
13 Mvivu anasema: “Kuna mwanasimba barabarani,
Kuna simba katika uwanja wa jiji!”+
15 Mvivu huutumbukiza* mkono wake katika bakuli la karamu,
Lakini amechoka sana kuurudisha kinywani mwake.+
16 Mvivu hufikiri kwamba ana hekima zaidi
Kuliko watu saba wanaojibu kwa busara.
17 Kama mtu anayemkamata mbwa masikio
Ndivyo alivyo mpita njia anayekasirishwa na* ugomvi usiomhusu.+
18 Kama mwenda wazimu anayetupa vishale vinavyowaka moto, mishale, na kifo*
19 Ndivyo alivyo mtu anayemhadaa jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”+
20 Pasipo na kuni moto huzimika,
Na pasipo na mchongezi, ugomvi hukoma.+
21 Kama makaa yanavyoongezwa kwenye makaa yanayozimika na kuni zinavyoongezwa motoni,
Ndivyo mtu mgomvi anavyochochea ugomvi.+
23 Kama fedha inayopakwa juu ya chombo cha udongo
Ndivyo yalivyo maneno ya upendo yanayotoka katika* moyo mwovu.+
24 Anayewachukia wengine huficha chuki hiyo kwa midomo yake,
Lakini ndani amesitiri udanganyifu.
25 Ingawa anaongea kwa fadhili, usimwamini,
Kwa maana kuna mambo saba yanayochukiza moyoni mwake.*
26 Ingawa chuki yake imefichwa kwa udanganyifu,
Uovu wake utafunuliwa kutanikoni.
27 Anayechimba shimo ataanguka ndani yake,
Na yeyote anayebingirisha jiwe—litamrudia.+
28 Ulimi unaosema uwongo huwachukia watu uliowaponda,
Na kinywa kinachosifusifu huleta uharibifu.+