Zaburi
Muziki wa Daudi.
143 Ee Yehova, isikie sala yangu;+
Sikiliza sihi yangu ya kuomba msaada.
Nijibu katika uaminifu wako na katika uadilifu wako.
2 Usinihukumu mimi mtumishi wako,
Kwa maana hakuna yeyote aliye hai anayeweza kuwa mwadilifu mbele zako.+
3 Kwa maana adui ananifuatia;
Ameuponda uhai wangu ardhini.
Amenifanya nikae gizani kama wale waliokufa zamani za kale.
5 Ninazikumbuka siku za kale;
Ninatafakari utendaji wako wote;+
Ninatafakari* kwa bidii kazi ya mikono yako.
6 Ninakunyooshea mikono yangu;
Mimi ni kama nchi iliyokauka yenye kiu kwa ajili yako.+ (Sela)
8 Acha nisikie upendo wako mshikamanifu asubuhi,
Kwa maana ninakutumaini wewe.
9 Niokoe kutoka kwa maadui wangu, Ee Yehova.
Ninatafuta ulinzi wako.+
10 Nifundishe kufanya mapenzi yako,+
Kwa maana wewe ni Mungu wangu.
Roho yako ni nzuri;
Na iniongoze kwenye nchi tambarare.*
11 Ee Yehova, nihifadhi hai kwa ajili ya jina lako.
Katika uadilifu wako, niokoe kutoka katika taabu.+