Zaburi
Wimbo. Muziki wa Daudi.
108 Moyo wangu uko imara, Ee Mungu.
Nitaimba na kupiga muziki kwa nafsi yangu yote.*+
2 Amka, Ee kinanda; nawe pia, Ee kinubi.+
Nitayaamsha mapambazuko.
3 Nitakusifu miongoni mwa mataifa, Ee Yehova,
Nami nitakuimbia sifa* miongoni mwa mataifa.
4 Kwa maana upendo wako mshikamanifu ni mkubwa, uko juu kama mbingu,+
Na uaminifu wako, unafika mpaka angani.
5 Ukwezwe juu ya mbingu, Ee Mungu;
Utukufu wako na uwe juu ya dunia yote.+
6 Ili wapendwa wako waokolewe,
Tuokoe kwa mkono wako wa kuume na unijibu.+
7 Mungu ameongea katika utakatifu wake:*
8 Gileadi+ ni yangu, na Manase ni yangu,
Na Efraimu ni kofia ya kukinga* kichwa changu;+
Yuda ni fimbo yangu ya kiongozi.+
9 Moabu ni beseni langu la kuogea.+
Nitatupa kiatu changu juu ya Edomu.+
Nitapaza sauti kwa ushindi juu ya Ufilisti.”+
10 Ni nani atakayenipeleka kwenye lile jiji lenye ngome?
Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?+
11 Je, si wewe, Ee Mungu, ambaye umetukataa,
Mungu wetu, ambaye haendi tena na majeshi yetu?+