Zaburi
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
109 Ee Mungu ninayekusifu,+ usinyamaze.
2 Kwa maana waovu na wadanganyifu hufumbua vinywa vyao dhidi yangu.
Wanaongea kunihusu kwa ndimi za uwongo;+
3 Wananizingira kwa maneno ya chuki,
Na kunishambulia bila sababu.+
4 Wananipinga licha ya kwamba ninawapenda;+
Lakini ninaendelea kusali.
6 Mweke mtu mwovu amhukumu;
Mpinzani* na asimame mkono wake wa kulia.
9 Watoto wake* na wawe mayatima,
Na mke wake awe mjane.
10 Watoto wake* na watangetange wakiombaomba,
Wakitafuta chakula katika nyumba zao zilizoharibiwa.
11 Anayemdai na achukue kwa nguvu* vitu vyote alivyo navyo,
Wageni na wapore mali zake.
12 Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea kwa fadhili,*
Na asiwepo mtu yeyote wa kuwahurumia watoto wake mayatima.
14 Kosa la mababu zake na likumbukwe na Yehova,+
Na dhambi ya mama yake isifutwe.
15 Yehova na akumbuke daima waliyotenda;
Na afutilie mbali kumbukumbu lao kutoka duniani.+
16 Kwa maana hakukumbuka kutenda kwa fadhili,*+
Bali aliendelea kumfuatia mtu aliyekandamizwa,+ maskini, na aliyevunjika moyo
Ili amuue.+
17 Alipenda kulaani, kwa hiyo laana hiyo ikampata;
Hakupenda kubariki, kwa hiyo hakupata baraka yoyote.
18 Alivishwa laana kama vazi lake.
Nazo zikamwagwa mwilini mwake kama maji,
Mifupani mwake kama mafuta.
19 Laana zake na ziwe kama vazi analojifunika+
Na kama mshipi anaovaa daima.
20 Hayo ndiyo malipo yanayotoka kwa Yehova ya mtu anayenipinga+
Na ya wale wanaosema mambo maovu dhidi yangu.
21 Lakini wewe, Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu,
Tenda kwa niaba yangu kwa ajili ya jina lako.+
Niokoe, kwa sababu upendo wako mshikamanifu ni mwema.+
23 Ninapitilia mbali kama kivuli kinachofifia;
Nimekung’utwa kama nzige.
24 Magoti yangu yanalegea kwa sababu ya kufunga;
Mwili wangu umekonda, unazidi kupungua.*
25 Nimekuwa kitu cha kudhihakiwa nao.+
Wanaponiona, wanatikisa vichwa vyao.+
26 Nisaidie, Ee Yehova Mungu wangu;
Niokoe kwa upendo wako mshikamanifu.
27 Na wajue kwamba mkono wako ndio uliotenda hili;
Kwamba wewe, Ee Yehova, umetenda hili.
28 Waache watangaze laana, lakini wewe toa baraka.
Na waaibishwe wanapoinuka dhidi yangu,
Lakini acha mtumishi wako ashangilie.
30 Kinywa changu kitamsifu Yehova kwa bidii;
Nitamsifu yeye mbele ya watu wengi.+
31 Kwa maana atasimama mkono wa kulia wa maskini
Ili amwokoe kutoka kwa wale wanaomhukumu.