Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Luka 18
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Luka—Yaliyomo

      • Mfano wa mjane aliyeendelea kuomba (1-8)

      • Farisayo na mkusanya kodi (9-14)

      • Yesu na watoto (15-17)

      • Mtawala tajiri auliza swali (18-30)

      • Kifo cha Yesu chatabiriwa tena (31-34)

      • Kipofu aliyekuwa akiombaomba aponywa (35-43)

Luka 18:1

Marejeo

  • +Ro 12:12; Efe 6:18; Flp 4:6; Kol 4:2; 1Th 5:17

Luka 18:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kunishambulia mpaka animalize.”

Marejeo

  • +Lu 11:7, 8

Luka 18:7

Marejeo

  • +Ufu 6:9, 10
  • +2Pe 3:9

Luka 18:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “imani kama hii.” Tnn., “ile imani.”

Luka 18:12

Marejeo

  • +Mt 23:23

Luka 18:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nionyeshe rehema.”

Marejeo

  • +Zb 51:1-3

Luka 18:14

Marejeo

  • +Isa 66:2; Mt 21:28-31
  • +Isa 2:11; Mt 23:12; Yak 4:6; 1Pe 5:5

Luka 18:15

Marejeo

  • +Mt 19:13-15; Mk 10:13-16

Luka 18:16

Marejeo

  • +1Pe 2:2

Luka 18:17

Marejeo

  • +Mt 18:3; Mk 10:15

Luka 18:18

Marejeo

  • +Mt 19:16-22; Mk 10:17-22; Lu 10:25-28

Luka 18:19

Marejeo

  • +Mt 19:17; Mk 10:18

Luka 18:20

Marejeo

  • +Kut 20:14; Kum 5:18
  • +Kut 20:13; Kum 5:17
  • +Kut 20:15; Kum 5:19
  • +Kut 20:16; Kum 5:20
  • +Kut 20:12; Kum 5:16; Ro 13:9; Efe 6:2

Luka 18:22

Marejeo

  • +Mt 6:20; 19:21; Mk 10:21; Lu 12:33; 1Ti 6:18, 19

Luka 18:23

Marejeo

  • +Mt 19:22; Mk 10:22

Luka 18:24

Marejeo

  • +Met 11:28; Mt 19:23; Mk 10:23, 24; 1Ti 6:9

Luka 18:25

Marejeo

  • +Mt 19:24; Mk 10:25

Luka 18:26

Marejeo

  • +Mt 19:25

Luka 18:27

Marejeo

  • +Mt 19:26; Mk 10:27

Luka 18:28

Marejeo

  • +Mt 19:27

Luka 18:29

Marejeo

  • +Mt 19:28, 29; Mk 10:29, 30

Luka 18:30

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Ufu 2:10

Luka 18:31

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “yatakamilika.”

Marejeo

  • +Mt 16:21; 20:17-19; Mk 10:32-34

Luka 18:32

Marejeo

  • +Mt 27:2; Mdo 3:13
  • +Zb 22:7
  • +Isa 50:6

Luka 18:33

Marejeo

  • +Isa 53:5, 7
  • +Mk 10:33, 34; Lu 9:22

Luka 18:35

Marejeo

  • +Mt 20:29-34; Mk 10:46-52

Luka 18:38

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nionyeshe rehema!”

Luka 18:39

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nionyeshe rehema!”

Luka 18:42

Marejeo

  • +Lu 7:50; 17:19

Luka 18:43

Marejeo

  • +Mt 20:34
  • +Lu 5:26

Jumla

Luka 18:1Ro 12:12; Efe 6:18; Flp 4:6; Kol 4:2; 1Th 5:17
Luka 18:5Lu 11:7, 8
Luka 18:7Ufu 6:9, 10
Luka 18:72Pe 3:9
Luka 18:12Mt 23:23
Luka 18:13Zb 51:1-3
Luka 18:14Isa 66:2; Mt 21:28-31
Luka 18:14Isa 2:11; Mt 23:12; Yak 4:6; 1Pe 5:5
Luka 18:15Mt 19:13-15; Mk 10:13-16
Luka 18:161Pe 2:2
Luka 18:17Mt 18:3; Mk 10:15
Luka 18:18Mt 19:16-22; Mk 10:17-22; Lu 10:25-28
Luka 18:19Mt 19:17; Mk 10:18
Luka 18:20Kut 20:14; Kum 5:18
Luka 18:20Kut 20:13; Kum 5:17
Luka 18:20Kut 20:15; Kum 5:19
Luka 18:20Kut 20:16; Kum 5:20
Luka 18:20Kut 20:12; Kum 5:16; Ro 13:9; Efe 6:2
Luka 18:22Mt 6:20; 19:21; Mk 10:21; Lu 12:33; 1Ti 6:18, 19
Luka 18:23Mt 19:22; Mk 10:22
Luka 18:24Met 11:28; Mt 19:23; Mk 10:23, 24; 1Ti 6:9
Luka 18:25Mt 19:24; Mk 10:25
Luka 18:26Mt 19:25
Luka 18:27Mt 19:26; Mk 10:27
Luka 18:28Mt 19:27
Luka 18:29Mt 19:28, 29; Mk 10:29, 30
Luka 18:30Ufu 2:10
Luka 18:31Mt 16:21; 20:17-19; Mk 10:32-34
Luka 18:32Mt 27:2; Mdo 3:13
Luka 18:32Zb 22:7
Luka 18:32Isa 50:6
Luka 18:33Isa 53:5, 7
Luka 18:33Mk 10:33, 34; Lu 9:22
Luka 18:35Mt 20:29-34; Mk 10:46-52
Luka 18:42Lu 7:50; 17:19
Luka 18:43Mt 20:34
Luka 18:43Lu 5:26
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
  • 41
  • 42
  • 43
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Luka 18:1-43

Kulingana na Luka

18 Kisha akawaambia mfano ili kuwaonyesha umuhimu wa kuendelea kusali bila kukata tamaa.+ 2 Akasema: “Katika jiji fulani kulikuwa na mwamuzi ambaye hakumwogopa Mungu wala hakumheshimu mtu yeyote. 3 Pia, katika jiji hilo kulikuwa na mjane ambaye alikuwa akienda kwake na kumwomba, ‘Hakikisha kwamba kesi yangu itaamuliwa kwa haki.’ 4 Kwa muda fulani yule mwamuzi alikataa, lakini baadaye akajiambia, ‘Ingawa simwogopi Mungu wala simheshimu mtu yeyote, 5 kwa sababu huyu mjane anaendelea kunisumbua, nitahakikisha amepata haki ili asiendelee kuja kunichosha na maombi yake.’”*+ 6 Kisha Bwana akasema: “Sikieni alichosema mwamuzi huyo ingawa si mwadilifu! 7 Kwa hakika, je, Mungu hatawatendea haki watu wake waliochaguliwa ambao wanamlilia mchana na usiku,+ huku akiwaonyesha subira?+ 8 Ninawaambia, atawatendea haki upesi. Hata hivyo, Mwana wa binadamu atakapofika, je, kweli ataipata imani hii* duniani?”

9 Pia, aliwaambia mfano huu wale waliojiona kuwa waadilifu na kuwadharau wengine: 10 “Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja alikuwa Farisayo na mwingine mkusanya kodi. 11 Yule Farisayo akasimama na kuanza kusali akisema moyoni, ‘Ee Mungu, ninakushukuru kwa sababu mimi si kama watu wengine—wanyang’anyi, wasio waadilifu, wazinzi—au hata kama mkusanya kodi huyu. 12 Mimi hufunga mara mbili kwa juma; ninatoa sehemu ya kumi ya mapato yangu yote.’+ 13 Lakini yule mkusanya kodi alikuwa amesimama mbali kidogo na hata hakutaka kutazama mbinguni, bali alijipigapiga kifuani akisema, ‘Ee Mungu, nihurumie* mimi mtenda dhambi.’+ 14 Ninawaambia, mtu huyu alishuka kwenda nyumbani akiwa mwadilifu mbele za Mungu kuliko yule Farisayo.+ Kwa sababu kila mtu anayejiinua atafedheheshwa, lakini yeyote anayejinyenyekeza atainuliwa.”+

15 Sasa watu wakamletea Yesu watoto wao wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi walipoona hivyo wakaanza kuwakemea.+ 16 Lakini Yesu akawaita wale watoto, akisema: “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, na msijaribu kuwazuia, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa wale walio kama wao.+ 17 Kwa kweli ninawaambia, yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hataingia kamwe ndani yake.”+

18 Mtawala fulani akamuuliza: “Mwalimu Mwema, ninapaswa kufanya nini ili niurithi uzima wa milele?”+ 19 Yesu akamwambia: “Kwa nini unaniita mwema? Hakuna aliye mwema, isipokuwa mmoja, Mungu.+ 20 Unazijua amri hizi: ‘Usifanye uzinzi,+ usiue,+ usiibe,+ usitoe ushahidi wa uwongo,+ mheshimu baba yako na mama yako.’”+ 21 Ndipo akasema: “Nimeyashika hayo yote tangu nilipokuwa kijana.” 22 Baada ya kusikia hilo, Yesu akamwambia, “Bado kuna jambo unalokosa: Uza kila kitu ulicho nacho na uwagawie maskini pesa hizo, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha uje uwe mfuasi wangu.”+ 23 Aliposikia hivyo, akahuzunika sana, kwa sababu alikuwa tajiri sana.+

24 Yesu akamtazama na kusema: “Itakuwa vigumu sana kwa wale walio na pesa kuingia katika Ufalme wa Mungu!+ 25 Kwa kweli, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano ya kushonea kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”+ 26 Wale waliosikia hilo wakauliza: “Ni nani anayeweza kuokolewa?”+ 27 Akasema: “Mambo yasiyowezekana kwa wanadamu yanawezekana kwa Mungu.”+ 28 Lakini Petro akamwambia: “Tazama! Tumeacha vitu vyetu na kukufuata.”+ 29 Akawaambia: “Kwa kweli ninawaambia, hakuna yeyote ambaye ameacha nyumba, au mke, au ndugu, au wazazi, au watoto kwa ajili ya Ufalme wa Mungu+ 30 ambaye hatapata mara nyingi zaidi wakati huu, na katika mfumo wa mambo* unaokuja, uzima wa milele.”+

31 Ndipo akawaita kando wale 12 na kuwaambia: “Tazama! Tunapanda kwenda Yerusalemu, na mambo yote yaliyoandikwa kupitia manabii kuhusu Mwana wa binadamu yatatimia.*+ 32 Kwa mfano, atatiwa mikononi mwa watu wa mataifa+ naye atadhihakiwa,+ atatendewa kwa dharau, na kutemewa mate.+ 33 Watampiga mijeledi, kisha watamuua,+ lakini siku ya tatu atafufuka.”+ 34 Hata hivyo, hawakuelewa maana ya mambo hayo, kwa sababu walikuwa wamefichwa maneno hayo, nao hawakuelewa mambo yaliyosemwa.

35 Yesu alipokaribia Yeriko kipofu mmoja alikuwa ameketi kando ya barabara akiombaomba.+ 36 Aliposikia umati ukipita, akaanza kuuliza kilichokuwa kikiendelea. 37 Wakamjibu: “Yesu Mnazareti ndiye anayepita!”⁠ 38 Ndipo akasema kwa sauti kubwa: “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”* 39 Wale waliokuwa mbele wakaanza kumkemea wakimwambia anyamaze, lakini akazidi kusema kwa sauti kubwa: “Mwana wa Daudi, nihurumie!”* 40 Kisha Yesu akasimama na kuagiza mtu huyo aletwe kwake. Alipokaribia, Yesu akamuuliza: 41 “Unataka nikufanyie nini?” Akasema: “Bwana, naomba niweze kuona tena.” 42 Basi Yesu akamwambia: “Ona tena; imani yako imekuponya.”+ 43 Mara moja akaanza kuona tena, naye akaanza kumfuata Yesu+ huku akimtukuza Mungu. Pia, watu wote walipoona hayo, wakamsifu Mungu.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki