Zaburi
Muziki wa Daudi.
29 Mpeni Yehova anachostahili, enyi wana wa watu hodari,
Mpeni Yehova anachostahili kwa sababu ya utukufu wake na nguvu zake.+
2 Mpeni Yehova utukufu ambao jina lake linastahili.
Mwinamieni* Yehova katika mapambo matakatifu.*
3 Sauti ya Yehova husikika juu ya maji;
Mungu mtukufu hunguruma.+
Yehova yuko juu ya maji mengi.+
4 Sauti ya Yehova ina nguvu;+
Sauti ya Yehova ina fahari.
5 Sauti ya Yehova inavunja mierezi;
Naam, Yehova anaipasua-pasua mierezi ya Lebanoni.+
7 Sauti ya Yehova hupiga kwa miali ya moto;+
8 Sauti ya Yehova huifanya nyika itetemeke;+
Yehova huifanya nyika ya Kadeshi+ itetemeke.
9 Sauti ya Yehova humfanya paa atetemeke na kuzaa
Nayo huivua kabisa misitu.+
Na wote walio katika hekalu lake husema: “Utukufu!”
10 Yehova huketi kwenye kiti cha ufalme juu ya mafuriko ya maji;*+
Yehova huketi kwenye kiti cha ufalme akiwa Mfalme milele.+
11 Yehova atawapa nguvu watu wake.+
Yehova atawabariki watu wake kwa amani.+