Zaburi
Wa Daudi.
28 Ninaendelea kukulilia wewe, Ee Yehova Mwamba wangu;+
Usiwe kama kiziwi kwangu.
2 Sikia sihi zangu ninapokulilia unisaidie
Ninapoinua mikono yangu kuelekea chumba cha ndani zaidi cha mahali pako patakatifu.+
3 Usinikokote pamoja na waovu, pamoja na wale wanaotenda mambo yanayodhuru,+
Wale wanaoongea na jirani yao maneno ya amani lakini uovu uko mioyoni mwao.+
4 Walipe kulingana na matendo yao,+
Kulingana na mazoea yao maovu.
Walipe kulingana na kazi ya mikono yao,
Kulingana na mambo waliyotenda.+
Atawabomoa kabisa naye hatawajenga.
6 Yehova na asifiwe,
Kwa maana amesikia sihi zangu za kuomba msaada.
Amenisaidia, na moyo wangu unashangilia,
Kwa hiyo nitamsifu kwa wimbo wangu.
8 Yehova ni nguvu kwa watu wake;
Yeye ni ngome, anamletea mtiwa-mafuta wake wokovu mkubwa.+
9 Waokoe watu wako, na uubariki urithi wako.+
Wachunge na kuwabeba mikononi mwako milele.+