Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 29
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Yeremia—Yaliyomo

      • Barua ya Yeremia kwa watu walio uhamishoni Babiloni (1-23)

        • Waisraeli watarudi baada ya miaka 70 (10)

      • Ujumbe kwa Shemaya (24-32)

Yeremia 29:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “wajenzi wa maboma ya ulinzi.”

Marejeo

  • +2Fa 24:8; Yer 22:24
  • +Yer 22:26
  • +2Fa 24:15, 16; Yer 24:1

Yeremia 29:3

Marejeo

  • +2Fa 22:8; Yer 26:24; 39:13, 14; Eze 8:11
  • +2Fa 24:18

Yeremia 29:7

Marejeo

  • +1Ti 2:1, 2

Yeremia 29:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wabashiri.”

Marejeo

  • +Yer 14:14; 27:14

Yeremia 29:9

Marejeo

  • +Yer 23:21; 28:15

Yeremia 29:10

Marejeo

  • +2Nya 36:20, 21; Ezr 1:1-3; Da 9:2; Zek 1:12
  • +Kum 30:3; Ezr 2:1; Yer 24:6

Yeremia 29:11

Marejeo

  • +Sef 3:15
  • +Yer 31:17

Yeremia 29:12

Marejeo

  • +Da 9:3

Yeremia 29:13

Marejeo

  • +Law 26:40
  • +Kum 4:29; 30:1-4; 1Fa 8:47, 48; Yer 24:7

Yeremia 29:14

Marejeo

  • +Isa 55:6
  • +Isa 49:25; Yer 30:3; Eze 39:28
  • +Zb 126:1; Ho. 6:11; Amo 9:14; Sef 3:20

Yeremia 29:16

Marejeo

  • +Yer 28:1

Yeremia 29:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “zilizopasuka.”

Marejeo

  • +Yer 24:10
  • +Yer 24:2, 8

Yeremia 29:18

Marejeo

  • +Law 26:33
  • +Kum 28:25; Yer 34:17
  • +1Fa 9:8; 2Nya 29:8; Yer 25:9; Omb 2:15
  • +Yer 24:9

Yeremia 29:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “nikiamka mapema na kuwatuma.”

Marejeo

  • +Yer 7:13
  • +Yer 6:19

Yeremia 29:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.

Marejeo

  • +Yer 14:14; 29:8; Omb 2:14

Yeremia 29:23

Marejeo

  • +Yer 23:14
  • +Yer 7:9, 10; 27:15
  • +Yer 16:17; 23:24

Yeremia 29:24

Marejeo

  • +Yer 29:31, 32

Yeremia 29:25

Marejeo

  • +2Fa 25:18, 21; Yer 21:1, 2; 37:3; 52:24, 27

Yeremia 29:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “vyuma vya shingoni.”

Marejeo

  • +Yer 20:2

Yeremia 29:27

Marejeo

  • +Yer 1:1
  • +Yer 43:2

Yeremia 29:28

Marejeo

  • +Yer 29:5

Yeremia 29:29

Marejeo

  • +2Fa 25:18, 21

Yeremia 29:31

Marejeo

  • +Yer 14:14; 28:15, 16; Eze 13:8, 9

Jumla

Yer. 29:22Fa 24:8; Yer 22:24
Yer. 29:2Yer 22:26
Yer. 29:22Fa 24:15, 16; Yer 24:1
Yer. 29:32Fa 22:8; Yer 26:24; 39:13, 14; Eze 8:11
Yer. 29:32Fa 24:18
Yer. 29:71Ti 2:1, 2
Yer. 29:8Yer 14:14; 27:14
Yer. 29:9Yer 23:21; 28:15
Yer. 29:102Nya 36:20, 21; Ezr 1:1-3; Da 9:2; Zek 1:12
Yer. 29:10Kum 30:3; Ezr 2:1; Yer 24:6
Yer. 29:11Sef 3:15
Yer. 29:11Yer 31:17
Yer. 29:12Da 9:3
Yer. 29:13Law 26:40
Yer. 29:13Kum 4:29; 30:1-4; 1Fa 8:47, 48; Yer 24:7
Yer. 29:14Isa 55:6
Yer. 29:14Isa 49:25; Yer 30:3; Eze 39:28
Yer. 29:14Zb 126:1; Ho. 6:11; Amo 9:14; Sef 3:20
Yer. 29:16Yer 28:1
Yer. 29:17Yer 24:10
Yer. 29:17Yer 24:2, 8
Yer. 29:18Law 26:33
Yer. 29:18Kum 28:25; Yer 34:17
Yer. 29:181Fa 9:8; 2Nya 29:8; Yer 25:9; Omb 2:15
Yer. 29:18Yer 24:9
Yer. 29:19Yer 7:13
Yer. 29:19Yer 6:19
Yer. 29:21Yer 14:14; 29:8; Omb 2:14
Yer. 29:23Yer 23:14
Yer. 29:23Yer 7:9, 10; 27:15
Yer. 29:23Yer 16:17; 23:24
Yer. 29:24Yer 29:31, 32
Yer. 29:252Fa 25:18, 21; Yer 21:1, 2; 37:3; 52:24, 27
Yer. 29:26Yer 20:2
Yer. 29:27Yer 1:1
Yer. 29:27Yer 43:2
Yer. 29:28Yer 29:5
Yer. 29:292Fa 25:18, 21
Yer. 29:31Yer 14:14; 28:15, 16; Eze 13:8, 9
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Yeremia 29:1-32

Yeremia

29 Haya ndiyo maneno ya barua ambayo nabii Yeremia aliwatumia kutoka Yerusalemu wazee waliobaki miongoni mwa watu waliopelekwa uhamishoni, makuhani, manabii, na watu wote, ambao Nebukadneza alikuwa amewatoa Yerusalemu na kuwapeleka uhamishoni Babiloni, 2 baada ya Mfalme Yekonia+ na mama malkia,+ maofisa wa makao ya mfalme, wakuu wa Yuda na Yerusalemu, na mafundi na wahunzi* kuondoka Yerusalemu.+ 3 Aliituma barua hiyo kwa mkono wa Elasa mwana wa Shafani+ na Gemaria mwana wa Hilkia, ambao Mfalme Sedekia+ wa Yuda aliwatuma kwenda Babiloni kwa Mfalme Nebukadneza wa Babiloni. Barua hiyo ilisema hivi:

4 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anawaambia hivi watu wote waliohamishwa, ambao aliwafanya wapelekwe uhamishoni Babiloni kutoka Yerusalemu, 5 ‘Jengeni nyumba mkae ndani yake. Pandeni bustani na mle matunda yake. 6 Oeni wake mzae wana na mabinti; wachukulieni wana wenu wake na kuwaoza mabinti wenu, ili wao pia wazae wana na mabinti. Muwe wengi huko, msipungue. 7 Nanyi tafuteni amani kwa ajili ya jiji ambamo nimewapeleka uhamishoni, nanyi msali kwa Yehova kwa ajili ya jiji hilo, kwa maana jiji hilo likiwa na amani mtakuwa na amani.+ 8 Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Msiwaruhusu manabii wenu na waaguzi* wenu walio miongoni mwenu wawadanganye,+ nanyi msisikilize ndoto wanazoota. 9 Kwa maana ‘wanawatabiria uwongo katika jina langu. Mimi sijawatuma,’+ asema Yehova.”’”

10 “Kwa maana Yehova anasema hivi: ‘Miaka 70 itakapotimia huko Babiloni nitawakazia ninyi fikira,+ nami nitatimiza ahadi yangu kwa kuwarudisha mahali hapa.’+

11 “‘Kwa maana ninajua vizuri mawazo ninayofikiria kuwaelekea ninyi,’ asema Yehova, ‘mawazo ya amani, wala si ya msiba,+ ili niwape ninyi wakati ujao na tumaini.+ 12 Nanyi mtaniita na kuja na kusali kwangu, nami nitawasikiliza.’+

13 “‘Mtanitafuta na kunipata,+ kwa maana mtanitafuta kwa moyo wenu wote.+ 14 Nami nitawaruhusu mnipate,’+ asema Yehova. ‘Nami nitawakusanya mateka wenu na kuwakusanya ninyi pamoja kutoka katika mataifa yote na sehemu zote nilizowatawanya,’+ asema Yehova. ‘Nami nitawarudisha mahali nilipowatoa nikawapeleka uhamishoni.’+

15 “Lakini ninyi mmesema, ‘Yehova ametuinulia manabii katika Babiloni.’

16 “Kwa maana Yehova anamwambia hivi mfalme anayeketi kwenye kiti cha ufalme cha Daudi+ na watu wote wanaokaa katika jiji hili, ndugu zenu ambao hawakwenda pamoja nanyi uhamishoni, 17 ‘Yehova wa majeshi anasema hivi: “Tazameni, ninatuma dhidi yao upanga, njaa kali, na ugonjwa hatari,+ nami nitawafanya kuwa kama tini zilizooza* ambazo ni mbaya sana hivi kwamba haziwezi kuliwa.”’+

18 “‘Nami nitawafuatia kwa upanga,+ kwa njaa kali, na kwa ugonjwa hatari, nami nitawafanya wawe kitu cha kutisha kwa falme zote za dunia,+ na laana, na kitu cha kushangaza, kitu cha kupigiwa mluzi,+ na shutuma miongoni mwa mataifa yote ambako nitawatawanya,+ 19 kwa sababu hawakuyasikiliza maneno yangu niliyowapa kupitia watumishi wangu manabii,’ asema Yehova, ‘ambao niliwatuma tena na tena.’*+

“‘Lakini hamkusikiliza,’+ asema Yehova.

20 “Kwa hiyo, sikieni neno la Yehova, ninyi nyote mliopelekwa uhamishoni, niliowatoa Yerusalemu na kuwapeleka Babiloni. 21 Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi kuhusu Ahabu mwana wa Kolaya na kuhusu Sedekia mwana wa Maaseya, wanaowatabiria uwongo katika jina langu:+ ‘Nitawatia mikononi mwa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni, naye atawaua mbele ya macho yenu. 22 Na kile kitakachowapata kitakuwa laana itakayosemwa na watu wote wa Yuda walio uhamishoni Babiloni: “Yehova na akutendee kama Sedekia na kama Ahabu, ambao mfalme wa Babiloni aliwateketeza motoni!” 23 kwa maana wametenda kwa aibu katika Israeli,+ wakifanya uzinzi na wake za majirani wao na kusema maneno ya uwongo katika jina langu, maneno ambayo sikuwaamuru.+

“‘“Mimi Ndiye ninayejua, nami ni shahidi,”+ asema Yehova.’”

24 “Nawe utamwambia hivi Shemaya+ wa Nehelamu: 25 ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Kwa sababu ulituma barua katika jina lako kwa watu wote walio Yerusalemu, kwa Sefania+ mwana wa Maaseya, kuhani, na kwa makuhani wote, ukisema, 26 ‘Yehova amekuweka kuwa kuhani badala ya kuhani Yehoyada, ili uwe mwangalizi wa nyumba ya Yehova, uwe msimamizi wa mwendawazimu yeyote anayetenda kama nabii na kumweka katika mikatale na katika kongwa;*+ 27 basi, kwa nini hujamkemea Yeremia wa Anathothi,+ anayetenda kama nabii wenu?+ 28 Kwa maana hata alitutumia ujumbe Babiloni, akisema: “Muda mrefu utapita! Jengeni nyumba na mkae ndani yake. Pandeni bustani na mle matunda yake,+—”’”’”

29 Kuhani Sefania+ alipoisoma barua hiyo mbele ya nabii Yeremia, 30 Neno la Yehova likamjia Yeremia likisema: 31 “Watumie ujumbe watu wote waliopelekwa uhamishoni, ukisema, ‘Yehova anasema hivi kumhusu Shemaya wa Nehelamu: “Kwa sababu Shemaya aliwatabiria, ingawa sikumtuma, naye akajaribu kuwafanya mtumaini uwongo,+ 32 kwa hiyo Yehova anasema hivi: ‘Ninamkazia fikira Shemaya wa Nehelamu na wazao wake. Hakuna yeyote miongoni mwa watu wake atakayeokoka kati ya watu hawa, naye hataona mema nitakayowatendea watu wangu,’ asema Yehova, ‘kwa maana amewachochea watu wamwasi Yehova.’”’”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki