Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 25
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Isaya—Yaliyomo

      • Baraka nyingi kwa watu wa Mungu (1-12)

        • Karamu ya Yehova ya divai bora (6)

        • Kifo hakitakuwepo tena (8)

Isaya 25:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Mashauri ya.”

Marejeo

  • +Zb 40:5; 98:1; 107:8; 145:1, 4
  • +Zb 33:11
  • +Kum 32:4; Ne 9:33

Isaya 25:3

Marejeo

  • +Zb 46:10; 66:3; Eze 38:23

Isaya 25:4

Marejeo

  • +Zb 46:1; Nah 1:7; Sef 3:12
  • +Zb 91:1; 121:5-7; Isa 49:10

Isaya 25:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “divai iliyowekwa kwenye machicha.”

Marejeo

  • +Isa 11:9; 65:25
  • +Zb 72:16; 85:11, 12; Yer 31:12

Isaya 25:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “atameza.”

  • *

    Au “shela iliyosokotwa.”

Isaya 25:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Ataondoa.”

Marejeo

  • +Ho. 13:14; 1Ko 15:54; 2Ti 1:10; Ufu 20:14
  • +Isa 35:10; Ufu 7:17; 21:4

Isaya 25:9

Marejeo

  • +Isa 25:1
  • +Zb 37:34; 146:5
  • +Mik 7:7
  • +Zb 20:5; Sef 3:14, 15

Isaya 25:10

Marejeo

  • +Zb 132:13, 14; Isa 12:6
  • +Isa 15:1; Sef 2:9

Isaya 25:11

Marejeo

  • +Yer 48:29; Yak 4:6

Jumla

Isa. 25:1Zb 40:5; 98:1; 107:8; 145:1, 4
Isa. 25:1Zb 33:11
Isa. 25:1Kum 32:4; Ne 9:33
Isa. 25:3Zb 46:10; 66:3; Eze 38:23
Isa. 25:4Zb 46:1; Nah 1:7; Sef 3:12
Isa. 25:4Zb 91:1; 121:5-7; Isa 49:10
Isa. 25:6Isa 11:9; 65:25
Isa. 25:6Zb 72:16; 85:11, 12; Yer 31:12
Isa. 25:8Ho. 13:14; 1Ko 15:54; 2Ti 1:10; Ufu 20:14
Isa. 25:8Isa 35:10; Ufu 7:17; 21:4
Isa. 25:9Isa 25:1
Isa. 25:9Zb 37:34; 146:5
Isa. 25:9Mik 7:7
Isa. 25:9Zb 20:5; Sef 3:14, 15
Isa. 25:10Zb 132:13, 14; Isa 12:6
Isa. 25:10Isa 15:1; Sef 2:9
Isa. 25:11Yer 48:29; Yak 4:6
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Isaya 25:1-12

Isaya

25 Ee Yehova, wewe ni Mungu wangu.

Ninakukweza, ninalisifu jina lako,

Kwa maana umetenda mambo yanayostaajabisha,+

Mambo yaliyokusudiwa* tangu nyakati za kale,+

Kwa uaminifu,+ kwa kutegemeka.

 2 Kwa maana umelifanya jiji kuwa rundo la mawe,

Mji wenye ngome kuwa magofu yanayoporomoka.

Mnara wa wageni si jiji tena;

Halitajengwa tena kamwe.

 3 Ndiyo sababu watu wenye nguvu watakutukuza;

Jiji la mataifa yenye uonevu litakuogopa.+

 4 Kwa maana umekuwa ngome kwa mtu wa hali ya chini,

Ngome kwa maskini katika taabu yake,+

Kimbilio kutokana na dhoruba ya mvua,

Na kivuli wakati wa joto.+

Wakati mlipuko wa waonevu ni kama dhoruba ya mvua inayopiga ukuta,

 5 Kama joto katika nchi iliyokauka,

Unazikomesha ghasia za wageni.

Kama joto linavyokomeshwa na kivuli cha wingu,

Ndivyo wimbo wa waonevu unavyonyamazishwa.

 6 Katika mlima huu+ Yehova wa majeshi atawaandalia watu wa mataifa yote

Karamu ya vyakula vinono,+

Karamu ya divai bora,*

Ya vyakula vinono vilivyojazwa urojorojo,

Ya divai bora, iliyochujwa.

 7 Katika mlima huu ataondoa* kifuniko kinachowafunika watu wote

Na kifuniko kilichosokotwa* juu ya mataifa yote.

 8 Atameza* kifo milele,+

Na Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova atafuta kabisa machozi katika nyuso zote.+

Shutuma ya watu wake ataiondoa katika dunia yote,

Kwa maana Yehova mwenyewe amesema hayo.

 9 Siku hiyo watasema:

“Tazama! Huyu ndiye Mungu wetu!+

Tumemtumaini yeye,+

Naye atatuokoa.+

Huyu ndiye Yehova!

Tumemtumaini yeye.

Na tufurahi na kushangilia katika wokovu wake.”+

10 Kwa maana mkono wa Yehova utatulia juu ya mlima huu,+

Na Moabu itakanyagwa-kanyagwa mahali pake+

Kama nyasi zinavyokanyagwa-kanyagwa na kuwa rundo la mbolea.

11 Atapigapiga mikono yake ndani yake

Kama mwogeleaji anavyopigapiga mikono yake ili kuogelea,

Naye atakishusha kiburi chake+

Kwa mwendo stadi wa mikono yake.

12 Na jiji lenye ngome, pamoja na kuta zako ndefu za usalama,

Ataziangusha chini;

Atazibomoa na kuziangusha ardhini, mpaka mavumbini kabisa.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki