Methali
18 Yeyote anayejitenga na wengine anafuatia tamaa zake mwenyewe za kichoyo;
Hukataa* hekima yote inayotumika.
2 Mtu mpumbavu hapendezwi na uelewaji;
Anaona ni afadhali afunue yaliyo moyoni mwake.+
3 Mtu mwovu anapokuja, dharau huja pia,
Na aibu huja pamoja na fedheha.+
4 Maneno ya kinywa cha mtu ni maji yenye kina.+
Chemchemi ya hekima ni kijito kinachobubujika.
9 Yeyote aliye mvivu katika kazi yake
Ni ndugu ya mtu mharibifu.+
10 Jina la Yehova ni mnara wenye nguvu.+
Mwadilifu hukimbilia humo na kupata ulinzi.*+
11 Mali ya tajiri ni jiji lake lenye ngome;
Ni kama ukuta wa ulinzi katika mawazo yake.+
12 Kabla ya kuanguka kwa kishindo moyo wa mtu huwa na kiburi,+
Na kabla ya utukufu kuna unyenyekevu.+
13 Yeyote anayejibu kabla ya kusikia ukweli wa mambo,
Huo ni upumbavu na aibu kwake.+
14 Roho ya mtu inaweza kumtegemeza anapokuwa mgonjwa,+
15 Moyo wa mtu mwenye uelewaji hupata ujuzi,+
Na sikio la mwenye hekima hujitahidi kupata ujuzi.
16 Zawadi ya mwanadamu humfungulia njia;+
Humwezesha kufika mbele ya watu mashuhuri.
17 Mtu wa kwanza kuwasilisha kesi yake huonekana kuwa sahihi,+
19 Ndugu aliyekosewa ni mgumu kuliko jiji lenye ngome,+
Na kuna mizozo ambayo ni kama makomeo ya ngome.+
23 Maskini husihi anapoongea,
Lakini tajiri hujibu kwa ukali.