Zaburi
Nililemewa na taabu na huzuni.+
4 Lakini nikaliita jina la Yehova:+
“Ee, Yehova, niokoe!”*
6 Yehova anawalinda wasio na uzoefu.+
Nilishushwa chini, akaniokoa.
7 Acha nafsi* yangu ipumzike tena,
Kwa maana Yehova amenitendea kwa fadhili.
9 Nitatembea mbele za Yehova katika nchi ya walio hai.
10 Nilikuwa na imani, ndio maana niliongea;+
Niliteseka sana.
11 Basi nikashikwa na hofu na kusema:
“Kila mwanadamu ni mwongo.”+
12 Nitamlipa Yehova nini
Kwa mema yote aliyonitendea?
13 Nitakiinua kikombe cha wokovu,*
Nami nitaliitia jina la Yehova.
14 Nitamtimizia Yehova nadhiri zangu
Mbele ya watu wake wote.+
16 Ninakusihi, Ee Yehova,
Kwa maana mimi ni mtumishi wako.
Mimi ni mtumishi wako, mwana wa kijakazi wako.
Umezifungua pingu zangu.+
17 Nitakutolea dhabihu ya shukrani;+
Nitaliitia jina la Yehova.