Zaburi
99 Yehova amekuwa Mfalme.+ Mataifa na yatetemeke.
Anaketi kwenye kiti cha ufalme juu ya* makerubi.+ Dunia na itikisike.
2 Yehova ni mkuu Sayuni,
Naye yuko juu ya mataifa yote.+
3 Na walisifu jina lako kuu,+
Kwa maana linaogopesha, nalo ni takatifu.
4 Yeye ni mfalme hodari anayependa haki.+
Umeimarisha kabisa mambo manyoofu.
Umetekeleza haki na uadilifu+ katika Yakobo.
6 Musa na Haruni walikuwa miongoni mwa makuhani wake,+
Na Samweli alikuwa miongoni mwa wale walioliita jina lake.+
Walikuwa wakimwita Yehova,
Naye alikuwa akiwajibu.+
7 Alikuwa akiongea nao kutoka katika nguzo ya wingu.+
Walishika vikumbusho vyake na amri aliyowapa.+
8 Ee Yehova Mungu wetu, uliwajibu.+