Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Petro 2
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

2 Petro—Yaliyomo

      • Walimu wa uwongo watatokea (1-3)

      • Hukumu dhidi ya walimu wa uwongo ni hakika (4-10a)

        • Malaika watupwa ndani ya Tartaro (4)

        • Gharika; Sodoma na Gomora (5-7)

      • Tabia za walimu wa uwongo (10b-22)

2 Petro 2:1

Marejeo

  • +Mt 24:24; 1Ti 4:1
  • +1Ko 6:20

2 Petro 2:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ufidhuli; matendo yao ya kuchukiza yanayofanywa bila aibu.” Kigiriki, a·selʹgei·a. Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Yud 4
  • +Isa 52:5

2 Petro 2:3

Marejeo

  • +Yud 4
  • +2Pe 3:9

2 Petro 2:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi.

  • *

    Au labda, “mashimo.”

Marejeo

  • +Mwa 6:4; Efe 6:12
  • +1Pe 3:19, 20
  • +Yud 6

2 Petro 2:5

Marejeo

  • +Mwa 7:23
  • +Mwa 6:9; Ebr 11:7
  • +Mwa 8:18
  • +2Pe 3:6

2 Petro 2:6

Marejeo

  • +Mwa 19:24, 25
  • +Yud 7

2 Petro 2:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ufidhuli; matendo ya kuchukiza yanayofanywa bila aibu.” Kigiriki, a·selʹgei·a. Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Mwa 19:15, 16

2 Petro 2:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi.

2 Petro 2:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

  • *

    Angalia Kamusi.

  • *

    Tnn., “wakatiliwe mbali.”

Marejeo

  • +Zb 34:19; 1Ko 10:13; 2Ti 4:18; Ufu 3:10
  • +Ro 2:5; 2Pe 3:7

2 Petro 2:10

Marejeo

  • +Yud 7
  • +Kut 22:28; Yud 8

2 Petro 2:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wana heshima mbele za.”

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Marejeo

  • +Yud 9

2 Petro 2:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wanazaliwa kiasili.”

Marejeo

  • +Yud 10

2 Petro 2:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wanaojifurahisha bila kujizuia katika.”

Marejeo

  • +Ro 13:13
  • +Yud 12

2 Petro 2:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi zisizo imara.”

Marejeo

  • +Mt 5:28

2 Petro 2:15

Marejeo

  • +Hes 22:5, 6; Yud 11; Ufu 2:14
  • +Hes 22:7; Ne 13:2

2 Petro 2:16

Marejeo

  • +Hes 22:31, 34; 31:8
  • +Hes 22:28

2 Petro 2:17

Marejeo

  • +Yud 12, 13

2 Petro 2:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ufidhuli; matendo ya kuchukiza yanayofanywa bila aibu.” Kigiriki, a·selʹgei·a. Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Yud 16
  • +2Pe 2:14

2 Petro 2:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “anayeshindwa na kitu fulani, ni mtumwa wa kitu hicho.”

Marejeo

  • +1Pe 2:16
  • +Ro 6:16

2 Petro 2:20

Marejeo

  • +2Pe 1:4
  • +Ebr 6:4-6; 10:26

2 Petro 2:21

Marejeo

  • +Lu 12:47; Yoh 15:22

2 Petro 2:22

Marejeo

  • +Met 26:11

Jumla

2 Pet. 2:1Mt 24:24; 1Ti 4:1
2 Pet. 2:11Ko 6:20
2 Pet. 2:2Yud 4
2 Pet. 2:2Isa 52:5
2 Pet. 2:3Yud 4
2 Pet. 2:32Pe 3:9
2 Pet. 2:4Mwa 6:4; Efe 6:12
2 Pet. 2:41Pe 3:19, 20
2 Pet. 2:4Yud 6
2 Pet. 2:5Mwa 7:23
2 Pet. 2:5Mwa 6:9; Ebr 11:7
2 Pet. 2:5Mwa 8:18
2 Pet. 2:52Pe 3:6
2 Pet. 2:6Mwa 19:24, 25
2 Pet. 2:6Yud 7
2 Pet. 2:7Mwa 19:15, 16
2 Pet. 2:9Zb 34:19; 1Ko 10:13; 2Ti 4:18; Ufu 3:10
2 Pet. 2:9Ro 2:5; 2Pe 3:7
2 Pet. 2:10Yud 7
2 Pet. 2:10Kut 22:28; Yud 8
2 Pet. 2:11Yud 9
2 Pet. 2:12Yud 10
2 Pet. 2:13Ro 13:13
2 Pet. 2:13Yud 12
2 Pet. 2:14Mt 5:28
2 Pet. 2:15Hes 22:5, 6; Yud 11; Ufu 2:14
2 Pet. 2:15Hes 22:7; Ne 13:2
2 Pet. 2:16Hes 22:31, 34; 31:8
2 Pet. 2:16Hes 22:28
2 Pet. 2:17Yud 12, 13
2 Pet. 2:18Yud 16
2 Pet. 2:182Pe 2:14
2 Pet. 2:191Pe 2:16
2 Pet. 2:19Ro 6:16
2 Pet. 2:202Pe 1:4
2 Pet. 2:20Ebr 6:4-6; 10:26
2 Pet. 2:21Lu 12:47; Yoh 15:22
2 Pet. 2:22Met 26:11
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
2 Petro 2:1-22

Barua ya Pili ya Petro

2 Hata hivyo, kulikuwa pia na manabii wa uwongo miongoni mwa watu, kama vile pia kutakavyokuwa na walimu wa uwongo miongoni mwenu.+ Hawa wataingiza kimyakimya madhehebu yenye kuharibu, na hata watamkana bwana aliyewanunua,+ na kujiletea maangamizi ya haraka. 2 Zaidi ya hayo, wengi watafuata mwenendo wao mpotovu,*+ na kwa sababu yao ile njia ya kweli itatukanwa.+ 3 Pia, watawatumia ninyi vibaya kwa pupa wakisema maneno ya uwongo. Lakini hukumu yao iliyoamuliwa zamani za kale,+ haikawii, na maangamizi yao hayalali.+

4 Hakika Mungu hakujizuia kuwaadhibu malaika waliofanya dhambi,+ bali aliwatupa ndani ya Tartaro,*+ akiwaweka kwenye minyororo* ya giza zito ili wawekwe akiba kwa ajili ya hukumu.+ 5 Naye hakujizuia kuuadhibu ulimwengu wa kale,+ bali alimlinda salama Noa, mhubiri wa uadilifu,+ pamoja na wengine saba+ alipoleta gharika juu ya ulimwengu wa watu wasiomwogopa Mungu.+ 6 Na kwa kuyageuza majiji ya Sodoma na Gomora kuwa majivu, aliyahukumu+ akiweka kielelezo kwa watu wasiomwogopa Mungu kuhusu mambo yatakayokuja.+ 7 Naye alimwokoa Loti mwadilifu,+ aliyetaabishwa sana na mwenendo mpotovu* wa waasi sheria— 8 kwa maana siku baada ya siku mtu huyo mwadilifu alikuwa akiitesa nafsi* yake yenye uadilifu kwa sababu ya matendo ya kuasi sheria aliyoona na kusikia alipokuwa akiishi miongoni mwao. 9 Hivyo basi, Yehova* anajua jinsi ya kuwakomboa kutoka kwenye jaribu watu wenye ujitoaji-kimungu,*+ lakini kuwaweka akiba watu wasio waadilifu ili waangamizwe* katika siku ya hukumu,+ 10 hasa wale wanaotaka kutia unajisi miili ya wengine+ na ambao hudharau mamlaka.+

Wana ujasiri na ushupavu, hawaogopi kuwatukana watukufu, 11 lakini malaika, ingawa ni wakuu zaidi katika nguvu na uwezo, hawawashtaki kwa matukano, kwa sababu wanamheshimu* Yehova.*+ 12 Lakini watu hawa, kama wanyama wanaotenda kwa silika na wanaozaliwa* ili kukamatwa na kuangamizwa, wanayatukana mambo wasioyajua.+ Watapata maangamizo yanayoletwa na mwendo wao wenyewe wa maangamizi, 13 wakipata madhara kama thawabu ya mwendo wao wenye madhara.

Wanafurahia kuishi maisha ya anasa,+ hata mchana. Wao ni madoa na dosari, wanafurahia* mafundisho yao ya udanganyifu huku wakila karamu pamoja nanyi.+ 14 Macho yao yamejaa uzinzi+ na hawawezi kuachana na dhambi, nao huwashawishi wasio imara.* Moyo wao umezoezwa kuwa na pupa. Wao ni watoto waliolaaniwa. 15 Wameiacha njia iliyonyooka, wamepotoshwa. Wameifuata njia ya Balaamu+ mwana wa Beori, aliyependa thawabu ya kutenda makosa,+ 16 lakini akakaripiwa kwa sababu hakufanya yaliyo sawa.+ Mnyama wa kubeba mizigo asiye na sauti alizungumza kwa sauti ya mwanadamu na kuzuia mwendo wa kiwazimu wa nabii huyo.+

17 Hao ni chemchemi zisizo na maji na ukungu unaosukumwa na dhoruba kali, nao wamewekewa akiba giza zito kabisa.+ 18 Wao husema maneno ya kujigamba yasiyo na maana. Kwa kuvutia tamaa za mwili+ na kwa matendo ya upotovu wa maadili,* wanawashawishi watu waliotoka tu kuponyoka kutoka kwa watu wanaoishi katika kosa.+ 19 Wanawaahidi uhuru, huku wao wenyewe wakiwa watumwa wa uharibifu;+ kwa maana yeyote anayeshindwa na mwingine, ni mtumwa wake.*+ 20 Hakika ikiwa baada ya kuponyoka unajisi wa ulimwengu+ kupitia ujuzi sahihi kumhusu Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, wanajiingiza tena katika mambo haya na kushindwa, mwisho wao unakuwa mbaya zaidi kuliko mwanzo wao.+ 21 Ingekuwa afadhali kwao kama hawangejua kwa usahihi njia ya uadilifu kuliko baada ya kuijua wageuke kutoka kwenye amri takatifu waliyopokea.+ 22 Wamepatwa na ukweli wa methali inayosema: “Mbwa ameyarudia matapishi yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa amerudi kugaagaa kwenye matope.”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki