Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 5
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Isaya—Yaliyomo

      • Wimbo kuhusu shamba la Yehova la mizabibu (1-7)

      • Ole kwa shamba la Yehova la mizabibu (8-24)

      • Hasira ya Mungu dhidi ya watu wake (25-30)

Isaya 5:1

Marejeo

  • +Zb 80:8; Isa 5:7; Yer 2:21; Lu 20:9

Isaya 5:2

Marejeo

  • +Mt 21:33; Mk 12:1
  • +Ho. 10:1

Isaya 5:3

Marejeo

  • +Mik 6:2

Isaya 5:4

Marejeo

  • +2Nya 36:15; Eze 24:13

Isaya 5:5

Marejeo

  • +Law 26:31, 33; Ne 2:3; Zb 79:1

Isaya 5:6

Marejeo

  • +Kum 29:22, 23; Yer 25:11; 45:4
  • +Isa 32:13
  • +Kum 11:16, 17

Isaya 5:7

Marejeo

  • +Zb 80:8; Yer 12:10
  • +Mik 6:8
  • +Kum 15:9

Isaya 5:8

Marejeo

  • +Mik 2:1, 2
  • +1Fa 21:15, 16

Isaya 5:9

Marejeo

  • +2Nya 36:20, 21; Isa 27:10

Isaya 5:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “viganja kumi vya”

  • *

    Angalia Nyongeza B14.

  • *

    Angalia Nyongeza B14.

  • *

    Angalia Nyongeza B14.

Marejeo

  • +Kum 28:15, 17; Yoe 1:17

Isaya 5:11

Marejeo

  • +Lu 21:34; Ro 13:13

Isaya 5:13

Marejeo

  • +Isa 27:11; Yer 8:7; Ho. 4:6
  • +Omb 4:9

Isaya 5:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

  • *

    Au “limepanua nafsi yake.”

  • *

    Au “wakuu wake.”

Marejeo

  • +Kum 28:63

Isaya 5:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “haki yake.”

Marejeo

  • +Isa 6:3; Ufu 4:8
  • +Kum 32:4

Isaya 5:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Uamuzi wa; Shauri la.”

Marejeo

  • +Yer 5:12; 17:15; Eze 12:22

Isaya 5:20

Marejeo

  • +Met 17:15; Mal 2:17

Isaya 5:21

Marejeo

  • +Met 3:7; Ro 12:16

Isaya 5:22

Marejeo

  • +Met 23:20; 31:4, 5

Isaya 5:23

Marejeo

  • +Kum 16:19; Isa 1:23; Mik 3:11
  • +1Fa 21:13; Met 17:15

Isaya 5:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mafundisho.”

Marejeo

  • +Kum 31:20; 2Fa 17:13, 14; Ne 9:26; Isa 1:4

Isaya 5:25

Marejeo

  • +Kum 31:16, 17; 2Nya 36:15, 16; Omb 2:2
  • +Yer 16:4

Isaya 5:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nguzo ya ishara.”

Marejeo

  • +Yer 52:4
  • +Kum 28:49, 50; Yer 5:15
  • +Yer 4:13

Isaya 5:28

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ziko tayari kupiga mshale.”

Marejeo

  • +Hab 1:8

Isaya 5:29

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”

Marejeo

  • +Yer 50:17

Isaya 5:30

Marejeo

  • +Yer 6:23
  • +Yer 4:23

Jumla

Isa. 5:1Zb 80:8; Isa 5:7; Yer 2:21; Lu 20:9
Isa. 5:2Mt 21:33; Mk 12:1
Isa. 5:2Ho. 10:1
Isa. 5:3Mik 6:2
Isa. 5:42Nya 36:15; Eze 24:13
Isa. 5:5Law 26:31, 33; Ne 2:3; Zb 79:1
Isa. 5:6Kum 29:22, 23; Yer 25:11; 45:4
Isa. 5:6Isa 32:13
Isa. 5:6Kum 11:16, 17
Isa. 5:7Zb 80:8; Yer 12:10
Isa. 5:7Mik 6:8
Isa. 5:7Kum 15:9
Isa. 5:8Mik 2:1, 2
Isa. 5:81Fa 21:15, 16
Isa. 5:92Nya 36:20, 21; Isa 27:10
Isa. 5:10Kum 28:15, 17; Yoe 1:17
Isa. 5:11Lu 21:34; Ro 13:13
Isa. 5:13Isa 27:11; Yer 8:7; Ho. 4:6
Isa. 5:13Omb 4:9
Isa. 5:14Kum 28:63
Isa. 5:16Isa 6:3; Ufu 4:8
Isa. 5:16Kum 32:4
Isa. 5:19Yer 5:12; 17:15; Eze 12:22
Isa. 5:20Met 17:15; Mal 2:17
Isa. 5:21Met 3:7; Ro 12:16
Isa. 5:22Met 23:20; 31:4, 5
Isa. 5:23Kum 16:19; Isa 1:23; Mik 3:11
Isa. 5:231Fa 21:13; Met 17:15
Isa. 5:24Kum 31:20; 2Fa 17:13, 14; Ne 9:26; Isa 1:4
Isa. 5:25Kum 31:16, 17; 2Nya 36:15, 16; Omb 2:2
Isa. 5:25Yer 16:4
Isa. 5:26Yer 52:4
Isa. 5:26Kum 28:49, 50; Yer 5:15
Isa. 5:26Yer 4:13
Isa. 5:28Hab 1:8
Isa. 5:29Yer 50:17
Isa. 5:30Yer 6:23
Isa. 5:30Yer 4:23
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Isaya 5:1-30

Isaya

5 Tafadhali, acha nimwimbie mpenzi wangu

Wimbo kuhusu mpenzi wangu na shamba lake la mizabibu.+

Mpenzi wangu alikuwa na shamba la mizabibu kwenye kilima kinachozaa sana.

 2 Akalilima na kuondoa mawe ndani yake.

Akapanda mzabibu bora mwekundu,

Akajenga mnara katikati yake,

Naye akachimba shinikizo la divai ndani yake.+

Kisha akaendelea kutumaini kwamba litazaa zabibu,

Lakini lilizaa zabibu za mwituni peke yake.+

 3 “Na sasa, enyi wakaaji wa Yerusalemu na watu wa Yuda,

Tafadhali hukumuni kati yangu na shamba langu la mizabibu.+

 4 Ningelifanyia nini kingine shamba langu la mizabibu

Ambacho bado sijafanya?+

Kwa nini, nilipotumaini kwamba litazaa zabibu,

Lilizaa zabibu za mwituni peke yake?

 5 Sasa, tafadhali, acheni niwaambie

Kile nitakacholifanyia shamba langu la mizabibu:

Nitaondoa uzio wake,

Nalo litateketezwa kabisa.+

Nitaubomoa ukuta wake wa mawe,

Nalo litakanyagwa-kanyagwa.

 6 Nami nitalifanya liwe ukiwa;+

Halitapunguzwa matawi wala kulimwa.

Litamea vichaka vya miiba na magugu,+

Nami nitayaamuru mawingu yasinyeshe mvua yoyote juu yake.+

 7 Kwa maana shamba la mizabibu la Yehova wa majeshi ni nyumba ya Israeli;+

Watu wa Yuda ndilo shamba alilolipenda sana.

Aliendelea kutumaini haki itendwe,+

Lakini tazama! kulikuwa na ukosefu wa haki;

Alitumaini uadilifu ufanywe,

Lakini tazama! kulikuwa na kilio cha huzuni.”+

 8 Ole wao wanaounganisha nyumba moja na nyingine+

Na wanaounganisha shamba moja na lingine+

Mpaka nafasi inapokosekana kabisa

Nanyi mnaishi peke yenu nchini!

 9 Yehova wa majeshi ameapa masikioni mwangu

Kwamba nyumba nyingi, ingawa ni kubwa na maridadi,

Zitakuwa kitu cha kutisha,

Bila mkaaji.+

10 Kwa maana ekari kumi za* shamba la mizabibu zitazaa kipimo kimoja tu cha bathi,*

Na kipimo kimoja cha homeri* ya mbegu kitazaa efa* moja tu.+

11 Ole wao wanaoamka asubuhi na mapema ili wanywe kileo,+

Wanaokawia hadi giza linapoingia jioni mpaka divai inapowawasha!

12 Wana kinubi na kinanda,

Tari, filimbi, na divai katika karamu zao;

Lakini hawafikirii utendaji wa Yehova,

Wala hawaioni kazi ya mikono yake.

13 Kwa hiyo watu wangu wataenda uhamishoni

Kwa sababu ya kukosa ujuzi;+

Wanaume wao wenye utukufu watakuwa na njaa,+

Na watu wao wote watakauka kwa kiu.

14 Kwa hiyo Kaburi* limejipanua*

Nalo limefungua kinywa chake bila kikomo;+

Na fahari yake,* umati wake wenye kelele, na watu wake wanaosherehekea

Hakika watashuka na kuingia ndani yake.

15 Na mwanadamu atainama,

Mwanadamu atashushwa,

Na macho ya wenye majivuno yatashushwa.

16 Yehova wa majeshi atakwezwa kupitia hukumu yake;*

Mungu wa kweli, Aliye Mtakatifu,+ atajitakasa mwenyewe kupitia uadilifu.+

17 Na wanakondoo watalisha kama katika malisho yao;

Wakaaji wageni watakula katika maeneo yenye ukiwa ya wanyama waliolishwa vizuri.

18 Ole wao wanaokokota hatia yao kwa kamba za udanganyifu

Na dhambi yao kwa kamba za gari la kukokotwa;

19 Wale wanaosema: “Na aharakishe kazi yake;

Na ije upesi ili tuione.

Kusudi la* Mtakatifu wa Israeli na litimizwe

Ili tulijue!”+

20 Ole wao wanaosema kwamba wema ni uovu na uovu ni wema,+

Wale wanaoweka giza badala ya nuru na nuru badala ya giza,

Wale wanaoweka uchungu badala ya utamu na utamu badala ya uchungu!

21 Ole wao walio na hekima katika macho yao wenyewe

Na walio na busara machoni pao wenyewe!+

22 Ole wao walio hodari katika kunywa divai

Na wanaume walio stadi katika kuchanganya vileo,+

23 Wale wanaomwondolea mwovu hatia kwa rushwa+

Na wanaomnyima haki mwadilifu!+

24 Kwa hiyo, kama mwali wa moto unavyoteketeza majani makavu

Na majani makavu yanavyonyauka katika moto,

Mizizi yao wenyewe itaoza,

Na maua yao yatatawanyika kama ungaunga,

Kwa sababu walikataa sheria* ya Yehova wa majeshi,

Na kulidharau neno la Mtakatifu wa Israeli.+

25 Ndiyo sababu hasira ya Yehova inawaka dhidi ya watu wake,

Naye ataunyoosha mkono wake dhidi yao na kuwapiga.+

Milima itatetemeka,

Na maiti zao zitakuwa kama takataka barabarani.+

Kwa sababu ya hayo yote, hasira yake haijapoa,

Lakini mkono wake bado umenyooshwa ili kupiga.

26 Ameliinulia ishara* taifa lililo mbali;+

Amewapigia mluzi waje kutoka miisho ya dunia;+

Na tazama! wanakuja upesi sana.+

27 Hakuna yeyote kati yao aliyechoka wala kujikwaa.

Hakuna yeyote anayesinzia au kulala.

Mshipi ulio kwenye kiuno chao haujalegezwa,

Wala kamba za viatu vyao hazijakatika.

28 Mishale yao yote ni mikali,

Na pinde zao zote zimepindika.*

Kwato za farasi wao ni kama jiwe gumu lenye makali,

Na magurudumu yao kama upepo wa dhoruba.+

29 Mngurumo wao ni kama wa simba;

Wananguruma kama wanasimba.*+

Watanguruma na kukamata mawindo

Na kuyabeba bila mtu wa kuyaokoa.

30 Siku hiyo watanguruma juu yake

Kama mngurumo wa bahari.+

Mtu yeyote anayeitazama nchi ataona giza lenye kutaabisha;

Hata nuru imetiwa giza kwa sababu ya mawingu.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki