Zaburi
Kwa kiongozi wa Nehilothi.* Muziki wa Daudi.
5 Sikiliza maneno yangu, Ee Yehova;+
Sikiliza kwa makini kilio changu cha uchungu.
2 Sikiliza kilio changu cha kuomba msaada,
Ee Mfalme wangu na Mungu wangu, kwa sababu ninasali kwako.
3 Ee Yehova, utasikia sauti yangu asubuhi;+
Asubuhi nitakueleza mahangaiko yangu+ na kusubiri kwa hamu.
5 Hakuna mtu yeyote mwenye kiburi anayeweza kusimama mbele zako.*
Yehova anawachukia kabisa watu wakatili na wadanganyifu.*+
7 Lakini nitaingia katika nyumba yako+ kwa sababu ya upendo wako mwingi mshikamanifu;+
Nitainama chini kuelekea hekalu lako takatifu* nikiwa na heshima na woga kukuelekea.+
8 Niongoze, Ee Yehova, katika uadilifu wako kwa sababu ya maadui wangu;
Ifanye njia yako iwe wazi kwangu.+
9 Kwa maana hakuna lolote wanalosema linaloweza kutumainiwa;
Ndani yao hamna lolote isipokuwa nia ya kudhuru.
10 Lakini Mungu atawatangaza kuwa na hatia;
Njama zao wenyewe zitasababisha waanguke.+
Na wafukuzwe kwa sababu ya dhambi zao nyingi,
Kwa maana wamekuasi wewe.
11 Lakini wale wote wanaokukimbilia watashangilia;+
Watapaza sauti kwa shangwe daima.
Nawe utawakinga wasifikiwe,
Na wale wanaolipenda jina lako watashangilia kwa sababu yako.
12 Kwa maana utambariki yeyote aliye mwadilifu, Ee Yehova;
Utawazunguka kwa kibali kana kwamba kwa ngao kubwa.+