Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Waebrania 3
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Waebrania—Yaliyomo

      • Yesu ni mkuu kuliko Musa (1-6)

        • Vitu vyote vilitengenezwa na Mungu (4)

      • Onyo dhidi ya kukosa imani (7-19)

        • “Leo ikiwa mtaisikiliza sauti yake” (7, 15)

Waebrania 3:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mwaliko.”

  • *

    Au “tunayemkiri.”

Marejeo

  • +Flp 3:14; 1Th 2:12
  • +Ebr 8:1

Waebrania 3:2

Marejeo

  • +Yoh 8:29
  • +Hes 12:7

Waebrania 3:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, Yesu.

Marejeo

  • +Mt 17:1, 2

Waebrania 3:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ushahidi.”

Waebrania 3:6

Marejeo

  • +Mt 17:5
  • +1Pe 2:5

Waebrania 3:7

Marejeo

  • +2Sa 23:2; Mdo 1:16

Waebrania 3:8

Marejeo

  • +Kut 17:7

Waebrania 3:9

Marejeo

  • +Kut 16:35; Hes 32:13; Zb 95:9

Waebrania 3:11

Marejeo

  • +Hes 14:22, 23; Zb 95:7-11

Waebrania 3:12

Marejeo

  • +Ebr 2:1

Waebrania 3:13

Marejeo

  • +Zb 95:7

Waebrania 3:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “tunakuwa na ushirika na.”

Marejeo

  • +Ufu 2:10

Waebrania 3:15

Marejeo

  • +Zb 95:7, 8

Waebrania 3:16

Marejeo

  • +Kut 17:1-3; Hes 14:2, 4

Waebrania 3:17

Marejeo

  • +Hes 14:11; Kum 32:21
  • +Hes 14:22, 23, 28-30; Yud 5

Waebrania 3:19

Marejeo

  • +Ebr 4:6

Jumla

Ebr. 3:1Flp 3:14; 1Th 2:12
Ebr. 3:1Ebr 8:1
Ebr. 3:2Yoh 8:29
Ebr. 3:2Hes 12:7
Ebr. 3:3Mt 17:1, 2
Ebr. 3:6Mt 17:5
Ebr. 3:61Pe 2:5
Ebr. 3:72Sa 23:2; Mdo 1:16
Ebr. 3:8Kut 17:7
Ebr. 3:9Kut 16:35; Hes 32:13; Zb 95:9
Ebr. 3:11Hes 14:22, 23; Zb 95:7-11
Ebr. 3:12Ebr 2:1
Ebr. 3:13Zb 95:7
Ebr. 3:14Ufu 2:10
Ebr. 3:15Zb 95:7, 8
Ebr. 3:16Kut 17:1-3; Hes 14:2, 4
Ebr. 3:17Hes 14:11; Kum 32:21
Ebr. 3:17Hes 14:22, 23, 28-30; Yud 5
Ebr. 3:19Ebr 4:6
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Waebrania 3:1-19

Kwa Waebrania

3 Kwa hiyo, ndugu watakatifu, washiriki wa mwito* wa mbinguni,+ mfikirieni mtume na kuhani mkuu tunayemkubali*—Yesu.+ 2 Alikuwa mwaminifu kwa Yule aliyemchagua,+ kama vile Musa alivyokuwa pia katika nyumba yote ya Mungu.+ 3 Kwa maana huyo* anastahili utukufu zaidi+ kuliko Musa, kwa kuwa yule anayejenga nyumba ana heshima kuliko nyumba yenyewe. 4 Bila shaka, kila nyumba hujengwa na mtu fulani, lakini yule aliyevijenga vitu vyote ni Mungu. 5 Sasa Musa alikuwa mtumishi mwaminifu katika nyumba yote ya Huyo akiwa ushuhuda* wa mambo ambayo yangesemwa baadaye, 6 lakini Kristo alikuwa mwaminifu akiwa mwana+ juu ya nyumba ya Mungu. Sisi ni nyumba Yake,+ ikiwa kwa kweli tunashikilia imara uhuru wetu wa kusema na tumaini ambalo tunajisifia mpaka mwisho.

7 Kwa hiyo, kama vile roho takatifu inavyosema,+ “Leo ikiwa mtaisikiliza sauti yake, 8 msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama ule wakati wa kusababisha hasira kali, kama siku ile ya jaribu nyikani,+ 9 ambayo mababu zenu waliniweka kwenye jaribu, na kunipima, ingawa waliona matendo yangu kwa miaka 40.+ 10 Ndiyo sababu nilichukizwa na kizazi hiki, nikasema: ‘Wao hupotoka sikuzote katika mioyo yao, nao hawazijui njia zangu.’ 11 Kwa hiyo niliapa kwa hasira yangu: ‘Hawataingia katika pumziko langu.’”+

12 Jihadharini, akina ndugu, ili moyo mwovu unaokosa imani usisitawi ndani ya yeyote kati yenu kwa kujiondoa kwa Mungu aliye hai;+ 13 lakini endeleeni kutiana moyo kila siku, maadamu inaitwa “Leo,”+ ili yeyote kati yenu asifanywe kuwa mgumu kwa nguvu za udanganyifu za dhambi. 14 Kwa maana kwa kweli tunakuwa washiriki wa* Kristo ikiwa tu tunashikilia imara mpaka mwisho uhakika tuliokuwa nao mwanzoni.+ 15 Kama inavyosemwa, “Leo ikiwa mtaisikiliza sauti yake, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama ule wakati wa kusababisha hasira kali.”+

16 Kwa maana ni nani waliosikia na bado wakamchochea kuwa na hasira kali? Kwa kweli, je, si wale wote waliotoka Misri chini ya Musa?+ 17 Zaidi ya hayo, Mungu alichukizwa na akina nani kwa miaka 40?+ Je, si wale waliotenda dhambi, ambao maiti zao zilianguka nyikani?+ 18 Naye aliapa kwa akina nani kwamba hawataingia katika pumziko lake? Je, si wale waliotenda kwa kutotii? 19 Kwa hiyo tunaona kwamba hawakuingia kwa sababu walikosa imani.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki