Methali
3 Ujinga wa mtu ndio unaopotosha njia yake,
Kisha moyo wake unamkasirikia vikali Yehova.
4 Mali huwavuta marafiki wengi,
Lakini maskini ataachwa hata na rafiki yake.+
5 Shahidi anayesema uwongo hatakosa kuadhibiwa,+
Na yule anayesema uwongo kila anapopumua hataponyoka.+
6 Wengi hujipendekeza kwa mtu maarufu,*
Na kila mtu ni rafiki ya yule anayetoa zawadi.
Huwafuatia ili awasihi, lakini hakuna yeyote anayemsikiliza.
8 Yeyote anayepata busara* anajipenda mwenyewe.*+
Yeyote anayethamini utambuzi kama hazina atapata mafanikio.*+
9 Shahidi anayesema uwongo hatakosa kuadhibiwa,
Na yule anayesema uwongo kila anapopumua ataangamia.+
10 Mjinga hastahili kuishi maisha ya anasa;
Sembuse mtumishi kuwatawala wakuu!+
13 Mwana mpumbavu humletea shida baba yake,+
14 Nyumba na mali hurithiwa kutoka kwa akina baba,
Lakini mke mwenye busara hutoka kwa Yehova.+
15 Uvivu huleta usingizi mzito,
Na mtu mzembe atakaa njaa.+
19 Mtu mwenye hasira kali atalipia adhabu;
Ukijaribu kumwokoa, utalazimika kufanya hivyo tena na tena.+
22 Kinachomfanya mtu awe mwenye kutamanika ni upendo wake mshikamanifu;+
Na ni afadhali kuwa maskini kuliko kuwa mwongo.
23 Kumwogopa Yehova huongoza kwenye uzima;+
Yule aliye na woga huo atakuwa na pumziko jema, hatapatwa na madhara.+
24 Mvivu huutumbukiza* mkono wake katika bakuli la karamu,
Lakini hata hashughuliki kuurudisha kinywani mwake.+
26 Yule anayemtendea vibaya baba yake na kumfukuza mama yake
Ni mwana anayeleta aibu na fedheha.+
27 Mwanangu, ukiacha kusikiliza nidhamu,
Utatangatanga mbali na maneno ya ujuzi.