WIMBO NA. 15
Msifuni Mzaliwa wa Kwanza wa Yehova!
- 1. Tumsifu Mwana, - Wa kwanza wa Yehova. - Mfalme mteule, - Baraka ataleta. - Atawala kwa haki, - Fahari, heshima. - Naye atatetea, - Enzi ya Yehova. - (KORASI) - Tumsifu Mwana, - Wa kwanza wa Yehova! - Kristo ametawazwa, - Naye anatawala! 
- 2. Tumsifu Mwana, - Wa kwanza wa Yehova. - Alilipa fidia; - Tupate msamaha. - Bibi-harusi wake, - Ametayarishwa. - Utawala wa Mungu, - Ushike hatamu. - (KORASI) - Tumsifu Mwana, - Wa kwanza wa Yehova! - Kristo ametawazwa, - Naye anatawala!