Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Tanzanian sign language publications (2020-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Jumamosi, Septemba 13

Wewe ni mtu mwenye thamani sana.—Dan. 9:23.

Nabii Danieli alikuwa kijana Wababiloni walipomfanya kuwa mfungwa na kumpeleka nchi ya mbali huko Babiloni. Lakini ni wazi kwamba Danieli aliwafurahisha wale waliomchukua mateka. Waliona kile “kinachoonekana kwa macho”—kwamba Danieli ‘hakuwa na kasoro yoyote, alikuwa mzuri kwa umbo’ na alitoka kwenye familia mashuhuri. (1 Sam. 16:7) Kutokana na sababu hizo, Wababiloni walimzoeza ili atumikie kwenye makao ya mfalme. (Dan. 1:​3, 4, 6) Yehova alimpenda Danieli kwa sababu ya sifa alizoamua kusitawisha. Kwa kweli, huenda Danieli alikuwa mwishoni mwa miaka yake ya utineja au mwanzoni mwa miaka yake ya 20, Yehova alipomtaja kwa njia nzuri pamoja na Noa na Ayubu, wanaume ambao walikuwa wamemtumikia Mungu kwa uaminifu kwa miaka mingi. (Mwa. 5:32; 6:​9, 10; Ayu. 42:​16, 17; Eze. 14:14.) Na Yehova aliendelea kumpenda Danieli katika maisha yake yote marefu yenye mambo ya kustaajabisha.—Dan. 10:​11, 19. w23.08 33:1-2

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumapili, Septemba 14

Kufahamu kikamili upana na urefu na kimo na kina.—Efe. 3:18.

Unapotaka kununua nyumba, ungependa kuichunguza kwa kina nyumba hiyo wewe mwenyewe. Tunaweza kufanya jambo kama hilo tunaposoma na kujifunza Biblia. Ikiwa utaisoma haraka-haraka, huenda ukajifunza habari za msingi tu, yaani, “mambo ya msingi ya maneno matakatifu ya Mungu.” (Ebr. 5:12) Badala yake, kama ilivyokuwa kwa ile nyumba, unapaswa kuingia “ndani” na kuichunguza Biblia kwa makini ili uielewe kikamili zaidi. Njia bora ya kujifunza Biblia ni kuona jinsi sehemu mbalimbali za ujumbe wake zinavyohusiana. Jitahidi kuelewa ni kweli gani ambazo unaamini na kwa nini unaamini kweli hizo. Ili kuelewa kikamili Neno la Mungu, tunapaswa kujifunza kweli zenye kina za Biblia. Mtume Paulo aliwahimiza ndugu na dada zake Wakristo wajifunze Neno la Mungu kwa bidii ili “[wafahamu] kikamili upana na urefu na kimo na kina” cha ile kweli, kisha wangekuwa na “mizizi na kuimarishwa” katika imani yao. (Efe. 3:​14-19) Sisi tunahitaji kufanya hivyo pia. w23.10 44:1-3

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumatatu, Septemba 15

Akina ndugu, fuateni mfano wa manabii waliopatwa na uovu na kuonyesha subira na ambao walisema katika jina la Yehova.—Yak. 5:10.

Biblia ina mifano mingi ya watu walioonyesha subira. Kwa nini usijiwekee lengo la kufanya utafiti kuhusu mifano ambayo watu hao walituwekea? Kwa mfano, ingawa Daudi alitiwa mafuta alipokuwa na umri mdogo ili awe mfalme wa wakati ujao wa Israeli, alisubiri kwa miaka mingi kabla ya kuanza kutawala akiwa mfalme. Simeoni na Ana walimwabudu Yehova kwa uaminifu walipokuwa wakimsubiri Masihi aliyeahidiwa. (Luka 2:​25, 36-38) Unapochunguza masimulizi hayo, tafuta majibu ya maswali yafuatayo: Ni nini ambacho huenda kilimsaidia mtu huyo awe mwenye subira? Alinufaikaje kwa kuonyesha subira? Ninawezaje kumwiga? Huenda pia ukanufaika kwa kujifunza kutokana na wale ambao hawakuonyesha subira. (1 Sam. 13:​8-14) Unaweza kujiuliza hivi: ‘Ni nini kilichofanya wakose subira? Walipatwa na matokeo gani mabaya?’ w23.08 35:15

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki