Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Tanzanian sign language publications (2020-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Ijumaa, Septemba 12

Tamasha ya ulimwengu huu inabadilika.—1 Kor. 7:31.

Ujulikane kuwa mtu mwenye usawaziko. Jiulize hivi: ‘Je, watu wananiona kuwa mwenye usawaziko, mwenye kukubali sababu, na kuwavumilia wengine? Au je, wanaona kwamba ninashikilia maoni yangu, ni mkali, au mwenye kichwa kigumu? Je, ninawasikiliza wengine na kukubaliana na maoni yao inapofaa?’ Kadiri tunavyozidi kuwa wenye usawaziko, ndivyo tunavyoonyesha kwamba tunamwiga Yehova na Yesu. Usawaziko unahusisha kunyumbulika hali zetu zinapobadilika. Mabadiliko hayo yanaweza kutusababishia matatizo tusiyotarajia. Huenda ukapatwa na ugonjwa ghafla. Au mabadiliko ya ghafla ya hali ya kiuchumi au ya kisiasa yanapotokea mahali tunapoishi yanaweza kuvuruga kabisa maisha yetu. (Mhu. 9:11) Huenda hata tukakabili hali ngumu tunapopata badiliko la mgawo wa kitheokrasi. Tunaweza kufanikiwa kunyumbulika hali zinapobadilika ikiwa tutachukua hatua nne zifuatazo: (1) kubali kwamba mambo yamebadilika, (2) fikiria kuhusu wakati ujao, (3) kazia fikira mambo yanayojenga, na (4) uwasaidie wengine. w23.07 32:7-8

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumamosi, Septemba 13

Wewe ni mtu mwenye thamani sana.—Dan. 9:23.

Nabii Danieli alikuwa kijana Wababiloni walipomfanya kuwa mfungwa na kumpeleka nchi ya mbali huko Babiloni. Lakini ni wazi kwamba Danieli aliwafurahisha wale waliomchukua mateka. Waliona kile “kinachoonekana kwa macho”—kwamba Danieli ‘hakuwa na kasoro yoyote, alikuwa mzuri kwa umbo’ na alitoka kwenye familia mashuhuri. (1 Sam. 16:7) Kutokana na sababu hizo, Wababiloni walimzoeza ili atumikie kwenye makao ya mfalme. (Dan. 1:​3, 4, 6) Yehova alimpenda Danieli kwa sababu ya sifa alizoamua kusitawisha. Kwa kweli, huenda Danieli alikuwa mwishoni mwa miaka yake ya utineja au mwanzoni mwa miaka yake ya 20, Yehova alipomtaja kwa njia nzuri pamoja na Noa na Ayubu, wanaume ambao walikuwa wamemtumikia Mungu kwa uaminifu kwa miaka mingi. (Mwa. 5:32; 6:​9, 10; Ayu. 42:​16, 17; Eze. 14:14.) Na Yehova aliendelea kumpenda Danieli katika maisha yake yote marefu yenye mambo ya kustaajabisha.—Dan. 10:​11, 19. w23.08 33:1-2

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumapili, Septemba 14

Kufahamu kikamili upana na urefu na kimo na kina.—Efe. 3:18.

Unapotaka kununua nyumba, ungependa kuichunguza kwa kina nyumba hiyo wewe mwenyewe. Tunaweza kufanya jambo kama hilo tunaposoma na kujifunza Biblia. Ikiwa utaisoma haraka-haraka, huenda ukajifunza habari za msingi tu, yaani, “mambo ya msingi ya maneno matakatifu ya Mungu.” (Ebr. 5:12) Badala yake, kama ilivyokuwa kwa ile nyumba, unapaswa kuingia “ndani” na kuichunguza Biblia kwa makini ili uielewe kikamili zaidi. Njia bora ya kujifunza Biblia ni kuona jinsi sehemu mbalimbali za ujumbe wake zinavyohusiana. Jitahidi kuelewa ni kweli gani ambazo unaamini na kwa nini unaamini kweli hizo. Ili kuelewa kikamili Neno la Mungu, tunapaswa kujifunza kweli zenye kina za Biblia. Mtume Paulo aliwahimiza ndugu na dada zake Wakristo wajifunze Neno la Mungu kwa bidii ili “[wafahamu] kikamili upana na urefu na kimo na kina” cha ile kweli, kisha wangekuwa na “mizizi na kuimarishwa” katika imani yao. (Efe. 3:​14-19) Sisi tunahitaji kufanya hivyo pia. w23.10 44:1-3

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki