Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 36
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ezekieli—Yaliyomo

      • Unabii kuhusu milima ya Israeli (1-15)

      • Kurudishwa kwa Waisraeli (16-38)

        • “Nitalitakasa jina langu kuu” (23)

        • “Kama bustani ya Edeni” (35)

Ezekieli 36:2

Marejeo

  • +Yer 49:1; Eze 35:10

Ezekieli 36:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “waliobaki.”

Marejeo

  • +Kum 28:37; 1Fa 9:7; Omb 2:15; Da 9:16

Ezekieli 36:4

Marejeo

  • +Yer 25:9
  • +Zb 79:4; Eze 34:28

Ezekieli 36:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “dharau katika nafsi.”

Marejeo

  • +Sef 3:8
  • +Oba 12
  • +Eze 25:12, 13; 35:10, 11; Amo 1:11

Ezekieli 36:6

Marejeo

  • +Zb 74:10; 123:4

Ezekieli 36:7

Marejeo

  • +Yer 25:9; 49:17

Ezekieli 36:8

Marejeo

  • +Isa 44:23; 51:3; Eze 36:30

Ezekieli 36:10

Marejeo

  • +Zek 8:4
  • +Isa 51:3; Yer 30:18, 19; Amo 9:14

Ezekieli 36:11

Marejeo

  • +Yer 31:27
  • +Isa 54:7; Yer 30:18
  • +Hag 2:9
  • +Ho. 2:20; Yoe 3:17

Ezekieli 36:12

Marejeo

  • +Yer 32:44; Oba 17
  • +Isa 65:23

Ezekieli 36:15

Marejeo

  • +Isa 54:4; 60:14; Mik 7:8; Sef 2:8; 3:19

Ezekieli 36:17

Marejeo

  • +Zb 106:38; Isa 24:5; Yer 2:7; 16:18
  • +Law 12:2; Isa 64:6

Ezekieli 36:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.

Marejeo

  • +Isa 42:24, 25
  • +Eze 23:37

Ezekieli 36:19

Marejeo

  • +Law 26:38; Eze 22:15

Ezekieli 36:20

Marejeo

  • +Isa 52:5; Ro 2:24

Ezekieli 36:21

Marejeo

  • +Zb 74:18; Isa 48:9; Eze 20:9

Ezekieli 36:22

Marejeo

  • +Zb 106:7, 8

Ezekieli 36:23

Marejeo

  • +Isa 5:16; Eze 20:41
  • +Zb 102:13-15

Ezekieli 36:24

Marejeo

  • +Kum 30:3; Isa 43:5; Yer 23:3; Eze 34:13; Ho. 1:11

Ezekieli 36:25

Marejeo

  • +Hes 19:13; Zb 51:7
  • +Isa 4:4; Yer 33:8
  • +Eze 6:4

Ezekieli 36:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, moyo ulio mwepesi kutii mwongozo wa Mungu.

Marejeo

  • +Yer 32:39
  • +Zb 51:10; Eze 11:19, 20
  • +Zek 7:12

Ezekieli 36:27

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “maamuzi yangu ya hukumu.”

Marejeo

  • +Yer 31:33

Ezekieli 36:28

Marejeo

  • +Yer 30:22; Eze 37:25, 27

Ezekieli 36:29

Marejeo

  • +Eze 34:29

Ezekieli 36:30

Marejeo

  • +Eze 34:27

Ezekieli 36:31

Marejeo

  • +Ezr 9:6; Ne 9:26; Yer 31:18; Eze 6:9

Ezekieli 36:32

Marejeo

  • +Kum 9:5; Da 9:19

Ezekieli 36:33

Marejeo

  • +Zek 8:8
  • +Isa 58:12; Yer 33:10, 11; Amo 9:14

Ezekieli 36:35

Marejeo

  • +Mwa 2:8
  • +Isa 51:3

Ezekieli 36:36

Marejeo

  • +Eze 28:26; 37:14

Ezekieli 36:38

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “Kama makundi ya kondoo wa dhabihu huko Yerusalemu.”

Marejeo

  • +Kut 23:17
  • +Yer 30:18, 19

Jumla

Eze. 36:2Yer 49:1; Eze 35:10
Eze. 36:3Kum 28:37; 1Fa 9:7; Omb 2:15; Da 9:16
Eze. 36:4Yer 25:9
Eze. 36:4Zb 79:4; Eze 34:28
Eze. 36:5Sef 3:8
Eze. 36:5Oba 12
Eze. 36:5Eze 25:12, 13; 35:10, 11; Amo 1:11
Eze. 36:6Zb 74:10; 123:4
Eze. 36:7Yer 25:9; 49:17
Eze. 36:8Isa 44:23; 51:3; Eze 36:30
Eze. 36:10Zek 8:4
Eze. 36:10Isa 51:3; Yer 30:18, 19; Amo 9:14
Eze. 36:11Yer 31:27
Eze. 36:11Isa 54:7; Yer 30:18
Eze. 36:11Hag 2:9
Eze. 36:11Ho. 2:20; Yoe 3:17
Eze. 36:12Yer 32:44; Oba 17
Eze. 36:12Isa 65:23
Eze. 36:15Isa 54:4; 60:14; Mik 7:8; Sef 2:8; 3:19
Eze. 36:17Zb 106:38; Isa 24:5; Yer 2:7; 16:18
Eze. 36:17Law 12:2; Isa 64:6
Eze. 36:18Isa 42:24, 25
Eze. 36:18Eze 23:37
Eze. 36:19Law 26:38; Eze 22:15
Eze. 36:20Isa 52:5; Ro 2:24
Eze. 36:21Zb 74:18; Isa 48:9; Eze 20:9
Eze. 36:22Zb 106:7, 8
Eze. 36:23Isa 5:16; Eze 20:41
Eze. 36:23Zb 102:13-15
Eze. 36:24Kum 30:3; Isa 43:5; Yer 23:3; Eze 34:13; Ho. 1:11
Eze. 36:25Hes 19:13; Zb 51:7
Eze. 36:25Isa 4:4; Yer 33:8
Eze. 36:25Eze 6:4
Eze. 36:26Yer 32:39
Eze. 36:26Zb 51:10; Eze 11:19, 20
Eze. 36:26Zek 7:12
Eze. 36:27Yer 31:33
Eze. 36:28Yer 30:22; Eze 37:25, 27
Eze. 36:29Eze 34:29
Eze. 36:30Eze 34:27
Eze. 36:31Ezr 9:6; Ne 9:26; Yer 31:18; Eze 6:9
Eze. 36:32Kum 9:5; Da 9:19
Eze. 36:33Zek 8:8
Eze. 36:33Isa 58:12; Yer 33:10, 11; Amo 9:14
Eze. 36:35Mwa 2:8
Eze. 36:35Isa 51:3
Eze. 36:36Eze 28:26; 37:14
Eze. 36:38Kut 23:17
Eze. 36:38Yer 30:18, 19
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ezekieli 36:1-38

Ezekieli

36 “Nawe, mwana wa binadamu, tabiri kuhusu milima ya Israeli, nawe useme, ‘Enyi milima ya Israeli, lisikieni neno la Yehova. 2 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Adui amesema hivi dhidi yenu, ‘Aha! Hata mahali pa juu pa zamani pamekuwa mali yetu!’”’+

3 “Basi tabiri, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Kwa sababu wamekufanya uwe ukiwa na kukushambulia kutoka kila upande, ili uwe mali ya wale waliookoka* kutoka kati ya mataifa na watu wanaendelea kuzungumza kukuhusu na kukuchongea,+ 4 kwa hiyo, enyi milima ya Israeli, sikieni neno la Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anavyoiambia milima na vilima, vijito na mabonde, magofu yaliyofanywa ukiwa,+ na majiji yaliyoachwa ambayo yameporwa na kudhihakiwa na wale waliookoka kutoka katika mataifa yanayowazunguka;+ 5 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anawaambia hivi: ‘Katika moto wa bidii yangu+ nitawakemea wale waliookoka kutoka katika mataifa na nchi yote ya Edomu, wale ambao kwa shangwe nyingi na kwa dharau kubwa*+ wamechukua nchi yangu na kuifanya kuwa mali yao, ili wachukue malisho yake na kuipora.’”’+

6 “Basi tabiri kuhusu nchi ya Israeli, nawe uiambie milima na vilima, vijito na mabonde, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Tazama! Nitazungumza kwa bidii yangu na kwa ghadhabu yangu, kwa sababu mmefedheheshwa na mataifa.”’+

7 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Mimi mwenyewe ninainua mkono wangu na kuapa kwamba mataifa yanayozunguka yatabeba aibu yao wenyewe.+ 8 Lakini ninyi, enyi milima ya Israeli, mtachipusha matawi na kuzaa matunda yenu kwa ajili ya watu wangu Waisraeli,+ kwa maana watarudi hivi karibuni. 9 Kwa maana niko pamoja nanyi, nami nitawageukia, nanyi mtalimwa na kupandwa mbegu. 10 Nitazidisha idadi ya watu wako—nyumba yote ya Israeli, yote—nayo majiji yatakaliwa+ na magofu yatajengwa upya.+ 11 Naam, nitazidisha idadi ya watu wako na mifugo yako;+ wataongezeka na kuzaana. Nami nitafanya ukaliwe kama ilivyokuwa zamani,+ nami nitakufanya usitawi kuliko mwanzoni;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+ 12 Nitawafanya watu—watu wangu Waisraeli—watembee juu yako, nao watakumiliki.+ Utakuwa urithi wao, nawe hutawafanya wakose watoto tena kamwe.’”+

13 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Kwa kuwa wanawaambia ninyi, “Wewe ni nchi inayowameza watu na kuwaua watoto wa mataifa yako,”’ 14 ‘kwa hiyo, hutawameza tena watu wala kuyafanya mataifa yako yakose watoto,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 15 ‘Sitaruhusu tena utukanwe na mataifa au udhihakiwe na watu,+ nawe hutafanya tena mataifa yako yakwazike,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

16 Na neno la Yehova likanijia tena likisema: 17 “Mwana wa binadamu, watu wa nyumba ya Israeli walipokuwa wakiishi katika nchi yao, waliichafua kwa njia zao na matendo yao.+ Njia zao zilikuwa kama uchafu wa hedhi kwangu.+ 18 Basi nikawamwagia ghadhabu yangu kwa sababu ya damu waliyoimwaga juu ya nchi+ na kwa sababu waliichafua nchi kwa sanamu zao zinazochukiza.*+ 19 Basi nikawatawanya miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali.+ Niliwahukumu kulingana na njia yao na kulingana na matendo yao. 20 Lakini walipoingia katika mataifa hayo, watu walilichafua jina langu takatifu+ kwa kusema hivi kuwahusu: ‘Hawa ndio watu wa Yehova, lakini walilazimika kutoka katika nchi yake.’ 21 Basi nitalihangaikia jina langu takatifu, ambalo watu wa nyumba ya Israeli walilichafua miongoni mwa mataifa ambako walienda.”+

22 “Kwa hiyo, waambie watu wa nyumba ya Israeli, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Sifanyi jambo hili kwa ajili yenu, enyi watu wa nyumba ya Israeli, bali kwa ajili ya jina langu takatifu, ambalo ninyi mmelichafua miongoni mwa mataifa ambako mlienda.”’+ 23 ‘Kwa hakika nitalitakasa jina langu kuu,+ ambalo lilichafuliwa miongoni mwa mataifa, ambalo mlilichafua miongoni mwao; nayo mataifa yatalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘nitakapotakaswa miongoni mwenu mbele ya macho yao. 24 Nitawatoa kutoka kwa mataifa na kuwakusanya kutoka katika nchi zote na kuwaleta katika nchi yenu.+ 25 Nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi;+ nami nitawatakasa kutokana na uchafu wenu+ wote na kutokana na sanamu zenu zote zinazochukiza.+ 26 Nitawapa moyo mpya+ na kutia roho mpya ndani yenu.+ Nitauondoa moyo wa jiwe+ kutoka mwilini mwenu na kuwapa moyo wa nyama.* 27 Nitaitia roho yangu ndani yenu, nami nitawafanya mtembee katika masharti yangu,+ nanyi mtashika na kufuata sheria zangu.* 28 Kisha mtakaa katika nchi niliyowapa mababu zenu, nanyi mtakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wenu.’+

29 “‘Nitawaokoa kutokana na uchafu wenu wote na kuiita nafaka na kuifanya iwe tele, nami sitawaletea njaa kali.+ 30 Nitayafanya matunda ya mti na mazao ya shamba yawe tele, ili msipatwe tena na aibu ya njaa kali miongoni mwa mataifa.+ 31 Kisha mtakumbuka njia zenu ovu na matendo yenu mabaya, nanyi mtajichukia kwa sababu ya hatia yenu na matendo yenu yanayochukiza.+ 32 Lakini jueni jambo hili: Sifanyi hivyo kwa ajili yenu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. ‘Badala yake, aibikeni na kufedheheka kwa sababu ya njia zenu, enyi watu wa nyumba ya Israeli.’

33 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Siku nitakayowatakasa kutokana na hatia yenu yote, nitayafanya majiji yakaliwe+ na magofu yajengwe upya.+ 34 Nchi yenye ukiwa, iliyokuwa ukiwa ili kila mtu anayepita aione, italimwa. 35 Na watu watasema: “Nchi iliyokuwa ukiwa imekuwa kama bustani ya Edeni,+ na majiji yaliyokuwa magofu na yaliyokuwa ukiwa na kubomolewa sasa yana ngome na yanakaliwa na watu.”+ 36 Na mataifa yaliyobaki kukuzunguka yatalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimejenga kilichobomolewa, nami nimepanda kilichofanywa ukiwa. Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema, nami nimelitenda.’+

37 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Nitawaruhusu pia watu wa nyumba ya Israeli waniombe niwatendee jambo hili: Nitazidisha idadi ya watu wao kama kundi. 38 Kama kundi la watu watakatifu, kama kundi la Yerusalemu* wakati wa sherehe zake,+ majiji yaliyokuwa magofu yatajaa makundi ya watu;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki