WIMBO NA. 32
Simama Upande wa Yehova!
- 1. Tulichanganyikiwa mwanzoni, - Tulinyweshwa uwongo wa dini. - Tulipopata habari njema, - Tulifurahi sana. - (KORASI) - Simama upande, Wake Yehova. - Yah hatakuacha; Nenda nuruni. - Na habari njema, Kote tangaza. - Ufalme wa Kristo, Hautakoma. 
- 2. Bega kwa bega twatumikia, - Twautangaza Ufalme kote. - Watu wote wajiamulie, - Kuwa upande Wake. - (KORASI) - Simama upande, Wake Yehova. - Yah hatakuacha; Nenda nuruni. - Na habari njema, Kote tangaza. - Ufalme wa Kristo, Hautakoma. 
- 3. Hatutamwogopa Ibilisi, - Tunamtegemea Yehova. - Japo ni wengi, sisi wachache, - Mungu ni ngome yetu. - (KORASI) - Simama upande, Wake Yehova. - Yah hatakuacha; Nenda nuruni. - Na habari njema, Kote tangaza. - Ufalme wa Kristo, Hautakoma. 
(Ona pia Zab. 94:14; Met. 3:5, 6; Ebr. 13:5.)