WIMBO NA. 31
Tembea Pamoja na Mungu!
(Mika 6:8)
- 1. Utembee kwa kiasi; - Pamoja na Yehova. - Uwe mshikamanifu kwake, - Ili akupe nguvu. - Na ukitii Neno lake, - Hutakengeuka; - Mungu na akuongoze, - Mtii sikuzote. 
- 2. Utembee kwa usafi; - Pamoja na Yehova. - Ujapokabili majaribu, - Atakusaidia. - Yote yaliyo safi, mema; - Tafakari hayo. - Na ili uvumilie, - Mtumaini Mungu. 
- 3. Utembee kwa furaha; - Pamoja na Yehova. - Uthamini akufanyiayo; - Baraka akupazo. - Utembee naye kwa shangwe. - Imba sifa zake. - Wote wataona wazi, - Wamwabudu Yehova. 
(Ona pia Mwa. 5:24; 6:9; Flp. 4:8; 1 Tim. 6:6-8.)