Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ijwyp habari 69
  • Sababu Gani Napaswa Kusali?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Sababu Gani Napaswa Kusali?
  • Vijana Wanauliza
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Sala ni nini?
  • Mungu anasikia?
  • Naweza kusali kuhusu nini?
  • Go Rapela Modimo go Nyoko go Šutetsa Thina Naye
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Sala Ni Zawadi Kutoka kwa Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Namna ya Kumukaribia Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Uone Sala Kuwa Pendeleo ya Maana Sana
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
Ona Habari Zaidi
Vijana Wanauliza
ijwyp habari 69
Kijana mwanamuke anakaa pembeni ya bahari

VIJANA WANAULIZA

Sababu Gani Napaswa Kusali?

Kulingana na uchunguzi mumoja, 80% ya vijana katika Amerika wanatoa sala, lakini ni nusu tu ya wale wenye wanatoa sala ndio wanafanya hivyo kila siku. Bila shaka, wamoja kati yao wanajiuliza: ‘Mutu anatoa sala ili ajisikie muzuri tu, ao ni zaidi ya hilo?’

  • Sala ni nini?

  • Mungu anasikia?

  • Naweza kusali kuhusu nini?

  • Mambo vijana wenzako wanasema

Sala ni nini?

Sala ni mazungumuzo ya kweli pamoja na Muumbaji wa vitu vyote. Fikiria jambo hilo! Yehova ni mukubwa kuliko wanadamu katika njia zote, lakini ‘haiko mbali sana na kila mumoja wetu.’ (Matendo 17:27) Kwa kweli, Biblia inatutolea mualiko huu wenye kupendeza: ‘Mukaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.’​—Yakobo 4:8.

Namna gani unaweza kumukaribia Mungu?

  • Njia moja ni kupitia sala; unatumia njia hiyo kusema na Mungu.

  • Njia ingine ni kupitia funzo la Biblia; Mungu “anasema” na wewe kupitia njia hiyo.

Mazungumuzo hayo kati ya mwanadamu na Mungu, ni kusema, sala na funzo la Biblia, yatakusaidia kukomalisha urafiki wa sana pamoja na Mungu.

“Kusema na Yehova​—kuzungumuza na Mwenye Kuwa Juu Zaidi​—ni moja kati ya mapendeleo makubwa zaidi yenye wanadamu wako nayo.”​—Jeremy.

“Kuambia Yehova namna najisikia kabisa katika moyo wangu kunanifanya nijisikie kuwa karibu naye.”​—Miranda.

Mungu anasikia?

Hata kama unaamini Mungu, na hata kama unatoa sala kwake, inaweza kuwa nguvu kukubali kwamba anasikia sala kabisa. Hata hivyo, Biblia inaita Yehova kuwa ‘Musikiaji wa sala.’ (Zaburi 65:2) Inakualika hata ‘kumutupia mahangaiko yako yote.’ Sababu gani? “Kwa sababu yeye anawajali ninyi.”​—1 Petro 5:7.

Jambo la kufikiria: Unajikaza kupata wakati wa kuzungumuza kwa ukawaida na marafiki wako wa sana? Unaweza kufanya hivyo pia na Mungu. Uzungumuze naye kikawaida katika sala, na ufanye hivyo kwa kutumia jina lake, Yehova. (Zaburi 86:​5-7; 88:9) Kwa kweli Biblia inakutia moyo ‘kusali bila kuacha.’​—1 Wathesalonike 5:​17.

“Sala ni mazungumuzo kati yangu na Baba yangu wa mbinguni, mwenye ninamufungulia moyo wangu wote.”​—Moises.

“Nazungumuza na Yehova kuhusu mambo ya ndani, kama vile naweza kuzungumuza na mama yangu ao na rafiki wa sana.”​—Karen.

Naweza kusali kuhusu nini?

Biblia inasema hivi: “Katika kila jambo kwa sala na dua pamoja na kutoa shukrani maombi yenu na yajulishwe Mungu.”​—Wafilipi 4:6.

Hilo linamaanisha kwamba ni muzuri kutoa sala kuhusu magumu yako? Ndiyo! Kwa kweli, Biblia inasema hivi: ‘Mutupie Yehova muzigo wako, naye mwenyewe atakutegemeza.’​—Zaburi 55:22.

Bila shaka, katika sala zako kwa Mungu hautazungumuzia tu magumu yako. Kijana mumoja mwanamuke mwenye kuitwa Chantelle anasema hivi: “Haiwezi kuwa urafiki wa muzuri kama tu naomba Yehova anisaidie. Nawaza kama kuonyesha shukrani kunapaswa kuwa jambo la kutia pa nafasi ya kwanza, na liste ya mambo ya kutolea shukrani inapaswa kuwa ya murefu.”

Jambo la kufikiria: Unatoa shukrani kwa ajili ya mambo gani katika maisha yako? Unaweza kufikiria mambo tatu ya kumutolea Yehova shukrani kwa ajili ya leo?

“Hata jambo fulani la kawaida, kama vile kufurahia maua yenye kupendeza, kunaweza kutuchochea kutoa sala ya shukrani kwa Yehova.”​—Anita.

“Uwaze sana juu ya jambo fulani lenye kukupendeza katika uumbaji ao juu ya andiko moja la Biblia lenye linagusa kabisa moyo wako, na kisha ushukuru Yehova kwa jambo hilo.”​—Brian.

Mambo vijana wenzako wanasema

Moises

“Undani wa sala unapaswa kuwa kama vile bahari, hapana kama maji yenye kuwa katika barabara. Yehova anapenda kutusaidia, na hata kama anajua kwamba tuko na lazima ya nini hata mbele ya kuomba, tunaweza kuonyesha ni kwa kiasi gani tunamutumainia kupitia undani wa sala zetu.”​—Moises.

Miranda

“Sala ni kama kamba yenye Yehova anakamata sehemu moja ya mwisho na mimi sehemu ingine ya mwisho. Wakati natoa sala kuhusu mambo yenye kuwa ndani ya moyo wangu, najisikia kama nashika sana sehemu yangu ya kamba na Yehova anafanya hivyo pia, na hilo linafanya uhusiano wetu ukuwe nguvu zaidi.”​—Miranda.

Jeremy

“Kama hatuko waangalifu, sala zetu zinaweza kuwa liste ya mambo yenye tunataka. Lakini, kwa kushukuru Yehova, tunafikia kufurahia mambo mengi yenye ametupatia na tunakazia sala zetu juu ya jambo fulani kuliko kujikazia sisi wenyewe tu.”​—Jeremy.

Shelby

“Kadiri tunashukuru Yehova ndio tunaendelea kuwa wenye shukrani zaidi. Kushukuru Yehova katika sala kunatusaidia kukazia akili baraka zenye tunapata kuliko kukazia akili magumu yenye tunapambana nayo.”​—Shelby.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine