HABARI YA KUJIFUNZA YA 31
Uone Sala Kuwa Pendeleo ya Maana Sana
“Sala yangu ikuwe kama uvumba wenye kutayarishwa mbele yako.”—ZB. 141:2.
WIMBO 47 Usali kwa Yehova Kila Siku
KIFUPI YA HABARIa
1. Namna gani tunapaswa kuona pendeleo yenye tuko nayo ya kusali kwa Yehova?
MUUMBAJI wa mbingu na dunia ametupatia pendeleo ya muzuri sana: Ameturuhusu kuzungumuza naye katika sala. Waza kidogo: Tunaweza kumuambia Yehova mambo yote yenye iko mu moyo wetu kila wakati, mu kila luga, bila kukamata naye programu. Tunaweza kusali kwa Baba yetu wa mbinguni wakati tuko ku hopitale ao mu chumba ya gereza, na kuwa hakika kama atatusikiliza. Hatuone ile pendeleo kuwa ya hivi-hivi tu.
2. Mufalme Daudi alionyesha namna gani kama aliona sala kuwa pendeleo ya maana sana?
2 Mufalme Daudi aliona sala kuwa pendeleo ya maana sana. Alimuimbia Yehova hivi: “Sala yangu ikuwe kama uvumba wenye kutayarishwa mbele yako.” (Zb. 141:1, 2) Mu siku za Daudi, makuhani walikuwa natayarisha kwa uangalifu sana uvumba mutakatifu wenye ulikuwa natumiwa mu ibada safi. (Kut. 30:34, 35) Sawa vile wale wenye walikuwa natayarisha uvumba walifanya vile kwa uangalifu sana, Daudi pia alifikiri sana juu ya mambo yenye angesema wakati angezungumuza na Yehova. Na siye pia tunapenda kufanya vile. Tunapenda sala zetu zimufurahishe Yehova.
3. Tunapaswa kujiendesha namna gani wakati tunasali kwa Yehova, na juu ya nini?
3 Wakati tunasali kwa Yehova, hatupaswe kuzungumuza naye sawa vile tunazungumuzaka na mutu mwenye tunazoeana naye sana. Lakini, tunapaswa kufanya vile kwa heshima sana. Fikiria maono ya ajabu yenye Isaya, Ezekieli, Danieli, na Yohana waliona. Ile maono ilikuwa tofauti, lakini ilifanana mu njia moya. Wote walionyesha namna Yehova ni Mufalme mwenye utukufu sana. Isaya ‘alimuona Yehova akiwa amekaa kwenye kiti cha ufalme chenye kuwa juu na chenye kuinuliwa.’ (Isa. 6:1-3) Ezekieli alimuona Yehova na anaikala ku gari yake ya mbinguni, na kulikuwa “mwangaza kumuzunguka pande zote kama mwangaza wa upinde wa mvua.” (Eze. 1:26-28) Danieli aliona “Muzee wa Siku” mwenye alikuwa navala nguo za mweupe, na mwangaza wa moto ulikuwa natoka ku kiti yake ya ufalme. (Da. 7:9, 10) Na Yohana alimuona Yehova ameikala ku kiti ya Ufalme yenye kuzungukwa na kitu fulani sawa vile upinde-mvua wenye kupendeza sana na wa rangi ya zumaridi. (Ufu. 4:2-4) Wakati tunafikiria utukufu wa Yehova wenye hauwezi kulinganishwa, tunaona kama ni pendeleo kubwa sana kumukaribia katika sala, na ni jambo ya maana kufanya vile kwa heshima kubwa. Lakini tunapaswa kusali juu ya mambo gani?
“BASI NINYI MUNAPASWA KUSALI HIVI”
4. Maneno ya utangulizi ya sala ya mufano yenye kuwa mu Matayo 6:9, 10 inatufundisha nini?
4 Soma Matayo 6:9, 10. Mu mahubiri yake ya ku mulima, Yesu alifundisha wanafunzi wake namna ya kusali mu njia yenye inamupendeza Mungu. Kisha kusema “basi ninyi munapaswa kusali hivi,” Yesu alionyesha mambo ya maana zaidi yenye tunapaswa kutanguliza mu sala yetu. Alisali jina ya Yehova itakaswe, Ufalme wake ukuye, wenye utaharibu maadui wote wa Mungu, na alisali juu ya mambo ya muzuri yenye Yehova atafanyia dunia na pia wanadamu. Wakati tunatia ile mambo mu sala zetu, tunaonyesha kama mapenzi ya Mungu ni ya maana kwetu.
5. Ni mubaya kusali juu ya mahitaji yetu ya kipekee?
5 Mu sehemu yenye kufuata ya ile sala, Yesu alionyesha kama haiko mubaya kusali juu ya mahitaji yetu ya kipekee. Tunaweza kumuomba Yehova atupatie chakula, asamehe zambi zetu, atulinde juu tusiangukie mu majaribu, na atuokoe katika mukono wa ule muovu. (Mt. 6:11-13) Wakati tunasali kwa Yehova juu ya ile mambo, tunaonyesha kama tunajua kuwa tuko na lazima ya musaada wake na kama tunapenda kumufurahisha.
Wakati bwana iko nasali pamoya na bibi yake, anaweza kusali juu ya mambo gani? (Ona fungu ya 6)b
6. Ni mubaya kusali juu ya mambo ingine tofauti na ile yenye kuzungumuziwa mu sala ya mufano? Fasiria.
6 Yesu hapendi wanafunzi wake wakuwe narudilia neno kwa neno ile sala ya mufano. Mu sala zingine zenye Yesu alitoa, alizungumuzia mambo ingine yenye ilikuwa ya lazima kwake ile wakati. (Mt. 26:39, 42; Yoh. 17:1-26) Vilevile, tunaweza kusali juu ya mambo ingine yenye inatuhangaisha. Wakati tunataka kukamata uamuzi fulani, tunaweza kusali Yehova atupatie hekima na uelewaji. (Zb. 119:33, 34) Wakati tunapewa mugao fulani wa nguvu, tunaweza kusali Yehova atusaidie tujue namna tunaweza kutimiza ule mugao. (Mez. 2:6) Wazazi wanaweza kusali kwa ajili ya watoto wao, watoto wanaweza kusali kwa ajili ya wazazi wao, na siye wote tunaweza na tunapaswa kusali kwa ajili ya wanafunzi wetu wa Biblia na kwa ajili ya wale wenye tunahubiria. Lakini, hatupaswe kusali kwa Yehova juu tu ya kumuomba mambo fulani.
Tunaweza kumusifu na kumushukuru Yehova juu ya mambo gani mu sala zetu? (Ona fungu ya 7-9)c
7. Juu ya nini tunapaswa kumusifu Yehova katika sala?
7 Hatupaswe kusahau kumusifu Yehova katika sala zetu. Hakuna mwenye anastahili kusifiwa sana sawa vile Mungu wetu. ‘Iko mwema na iko tayari kusamehe.’ Tena, iko ‘mwenye rehema na huruma, hakasirike haraka na iko mwenye upendo mwingi mushikamanifu na uaminifu.’ (Zb. 86:5, 15) Tuko kabisa na sababu za kumusifu Yehova juu ya sifa zake na juu ya mambo yenye anafanyaka.
8. Tunaweza kumushukuru Yehova juu ya mambo gani? (Zaburi 104:12-15, 24)
8 Zaidi ya kumusifu Yehova katika sala, tunapaswa kumushukuru juu ya mambo yote ya muzuri yenye anatutolea. Kwa mufano, tunaweza kumushukuru juu ya rangi za muzuri za maua, chakula mbalimbali ya butamu, na juu ya marafiki wenye kutia moyo wenye tuko nao. Baba yetu mwenye upendo anatupatia ile mambo yote, na mambo ingine ya mingi, juu tu tufurahi. (Soma Zaburi 104:12-15, 24.) Na zaidi sana, tunamushukuru sana Yehova juu ya chakula mingi ya kiroho yenye anatupatia, na juu ya tumaini ya muzuri ya wakati yenye kuya.
9. Nini njo inaweza kutusaidia tusisahau kumushukuru Yehova? (1 Watesalonike 5:17, 18)
9 Inaweza kuwa mwepesi sana kusahau kumushukuru Yehova juu ya mambo yote yenye anatufanyiaka. Nini njo inaweza kutusaidia tusisahau kumushukuru? Unaweza kufanya liste ya mambo yenye umemuomba Yehova na kuchunguza mara kwa mara ili kuona ni mambo gani yenye Yehova amejibia. Kisha usali kwake juu ya kumushukuru. (Soma 1 Watesalonike 5:17, 18.) Waza kidogo: Tunafurahiaka sana wakati wengine waanatushukuru. Vilevile, wakati tunakumbuka kumushukuru Yehova juu ya kujibia sala zetu, naye anafurahiaka sana. (Kol. 3:15) Lakini, kuko sababu ingine ya maana ya kumushukuru Yehova.
UMUSHUKURU YEHOVA JUU YA MWANA WAKE MUPENDWA
10. Kulingana na 1 Petro 2:21, juu ya nini tunapaswa kumushukuru Yehova kwa kutuma Yesu ku dunia?
10 Soma 1 Petro 2:21. Tunapaswa kumushukuru Yehova juu alituma Mwana wake mupendwa ili atufundishe. Tunajifunza mambo mingi juu ya Yehova na juu ya namna ya kumufurahisha wakati tunajifunza maisha ya Yesu. Kama tunaamini bei ya ukombozi ya Yesu, tunaweza kuwa na urafiki wa karibu na wenye amani na Yehova Mungu.—Ro. 5:1.
11. Juu ya nini tunapaswa kusali mu jina ya Yesu?
11 Tunamushukuru Yehova juu tunaweza kusali kwake kupitia Mwana wake. Yehova anatumiaka Yesu juu ya kujibia sala zetu. Yehova anasikilizaka na kujibia sala zenye zinatolewa mu jina ya Yesu. Yesu alisema hivi: “Kila jambo lenye munaomba katika jina langu, nitalifanya, ili Baba atukuzwe kuhusiana na Mwana. Mukiomba jambo lolote katika jina langu, nitalifanya.”—Yoh. 14:13, 14.
12. Tuko na sababu gani ingine ya kumushukuru Yehova juu ya Mwana wake?
12 Yehova anasamehe zambi zetu juu Yesu alishakakufa kwa ajili yetu. Biblia inaita Yesu kuwa “kuhani [wetu] mukubwa [mwenye kukaa] kwenye mukono wa kuume wa kiti cha ufalme cha Ukubwa mbinguni.” (Ebr. 8:1) Yesu ni “musaidizi [wetu] kwa Baba.” (1 Yo. 2:1) Tuko wenye shukrani sana kwa Yehova juu ametupatia kuhani mukubwa mwenye anaelewa uzaifu wetu, na anakuwaka “anatuombea!” (Ro. 8:34; Ebr. 4:15) Tuko wanadamu wenye hawakamilike. Njo maana, bila bei ya ukombozi ya Yesu, haiwezekane tumukaribie Yehova katika sala. Hatuwezi kupata maneno yenye inaweza kabisa kuonyesha shukrani yetu yote juu ya zawadi ya maana sana yenye Yehova ametupatia, ni kusema, Mwana wake mupendwa!
SALI JUU YA NDUGU NA DADA ZAKO
13. Usiku mbele ya kifo yake, namna gani Yesu alionyesha kama anapenda wanafunzi wake?
13 Usiku mbele ya kifo yake, Yesu alitoa sala ya murefu kwa ajili ya wanafunzi wake ili kumuomba Baba yake ‘awalinde kwa sababu ya ule muovu.’ (Yoh. 17:15) Ile inaonyesha kama Yesu alikuwa nawapenda sana! Hata ikiwa alijua kama alikuwa karibu kuteswa sana, aliendelea kuhangaikia mitume wake.
Wakati tunasali juu ya ndugu na dada zetu, tunaweza kumuambia Yehova nini? (Ona fungu ya 14-16)d
14. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunapenda ndugu na dada zetu?
14 Juu ya kumuiga Yesu, hatupaswe tu kuhangaikia mahitaji yetu wenyewe. Kuliko kufanya vile, tunapaswa kusali kwa ukawaida juu ya ndugu na dada zetu. Wakati tunafanya vile, tunatii amri ya Yesu ya kupendana, na tunamuonyesha Yehova ni kwa kiasi gani tunapenda ndugu na dada zetu. (Yoh. 13:34) Kusali juu ya ndugu na dada zetu haiko kupoteza wakati. Neno ya Mungu inatuambia kama “sala ya kumulilia Mungu ya mwenye haki iko na nguvu nyingi.”—Yak. 5:16.
15. Sababu gani tunapaswa kusali juu ya ndugu na dada zetu?
15 Tunapaswa kusali juu ya ndugu na dada zetu juu wako navumilia magumu mingi. Tunaweza kumuomba Yehova awasaidie kuvumilia ugonjwa, misiba ya asili, vita, mateso na magumu ingine. Tunaweza pia kusali juu ya ndugu na dada wenye wanajitolea ili kusaidia wale wenye kuwa mu uhitaji. Pengine unajua ndugu na dada fulani wenye wako na magumu ya vile. Hauone kama inaweza kuwa muzuri kutaya majina yao mu sala zako za kipekee? Tunaonyesha kama tunapenda kabisa ndugu na dada zetu wakati tunamuomba Yehova awasaidie kuvumilia.
16. Sababu gani tunapaswa kusali juu ya wale wenye kutuongoza?
16 Wale wenye kuongoza katika kutaniko wanafurahiaka sana wakati wengine wanasali juu yao, na zile sala zinawaleteaka faida. Mutume Paulo alijua kama alikuwa na lazima ya sala za wengine. Aliandika hivi: “Musali pia kwa ajili yangu, kwamba nipewe maneno ya kusema wakati ninafungua kinywa, ili niweze kusema bila woga wakati ninajulisha siri takatifu ya habari njema.” (Efe. 6:19) Leo pia, tuko na ndugu wengi wenye kutuongoza, na wenye kutumika kwa bidii. Tunaonyesha kama tunawapenda kwa kumuomba Yehova abariki kazi yao.
WAKATI TUNAWAKILISHA WENGINE MU SALA
17-18. Ni wakati gani tunaweza kuombwa tuwakilishe wengine mu sala, na ni mambo gani tunapaswa kukumbuka?
17 Wakati fulani, tunaweza kuombwa tuwakilishe wengine mu sala. Kwa mufano, dada mwenye iko naongoza funzo ya Biblia anaweza kuomba dada mwenye alimusindikiza atoe sala. Pengine ule dada mwenye alimusindikiza hajue mwanafunzi muzuri. Kwa hiyo, anaweza kupendelea kutoa sala ya mwisho. Ile itamusaidia aweze kutoa sala yenye inapatana na mahitaji ya mwanafunzi.
18 Ndugu anaweza kuombwa atoe sala ku mukutano wa mahubiri, ao ku mukutano wa kutaniko. Wakati ndugu anapewa ile pendeleo, hapaswe kusahau kusudi ya mukutano ni nini. Sala haipaswe kutumiwa juu ya kushauria kutaniko, ao kufanya matangazo. Kwa ujumla, dakika tano zinatumiwaka kwa ajili ya wimbo na sala. Kwa hiyo, ndugu mwenye kutoa sala hapaswe kutumia “maneno mengi,” zaidi sana ku mwanzo wa mukutano.—Mt. 6:7.
FANYA SALA KUWA JAMBO YA MAANA SANA MU MAISHA YAKO
19. Tunapaswa kufanya nini juu siku ya hukumu ya Yehova isitukute na hatuko tayari?
19 Juu siku ya hukumu ya Yehova inakaribia sana, tunapaswa kufanya sala kuwa jambo ya maana sana mu maisha yetu. Kuhusu ile, Yesu alisema hivi: “Muendelee kukesha, mukimulilia Mungu kila wakati ili muweze kuponyoka mambo haya yote yenye yanapaswa kutokea.” (Lu. 21:36) Kusali kwa ukawaida kutatusaidia tuendelee kuwa macho kiroho juu siku ya hukumu ya Yehova isitukute na hatuko tayari.
20. Tunapaswa kufanya nini juu sala zetu zikuwe sawa vile uvumba wenye harufu ya muzuri?
20 Tumejifunza nini? Tumeona kama sala ni pendeleo ya maana sana. Mambo ya maana sana yenye tunapaswa kutia mu sala yetu ni ile yenye inahusiana kabisa na mapenzi ya Yehova. Tunapaswa pia kumushukuru Yehova juu ya Mwana wake, juu ya Ufalme wake, na tunapaswa kusali juu ya ndugu na dada zetu. Tunapaswa pia kusali juu ya mahitaji yetu ya kimwili na ya kiroho. Wakati tunafikiri kwa uangalifu juu ya mambo yenye tutasema mu sala zetu, tunaonyesha kama tunaona sala kuwa pendeleo ya maana sana. Maneno yetu itakuwa sawa vile uvumba wenye harufu ya muzuri kwa Yehova, ni kusema, ‘itamufurahisha yeye.’—Mez. 15:8.
WIMBO 45 Mawazo ya Moyo Wangu
a Tunafurahia sana pendeleo ya kuzungumuza na Yehova katika sala. Tunapenda sala zetu zikuwe sawa vile uvumba wenye harufu ya muzuri sana, ni kusema, zimufurahishe Yehova. Mu hii habari, tutazungumuzia mambo yenye tunaweza kutia mu sala zetu. Tutazungumuzia pia mawazo fulani yenye hatupaswe kusahau wakati tunaombwa kuwakilisha wengine mu sala.
b MAFASIRIO YA PICHA: Bwana anasali na bibi yake, anamuomba Yehova alinde mutoto wao ku masomo, alinde wazazi wao wenye kuzeeka, na asaidie mwanafunzi fulani wa Biblia afanye maendeleo ya kiroho.
c MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu kijana anamushukuru Yehova juu ya bei ya ukombozi ya Yesu, juu ya dunia yetu ya muzuri, na juu ya chakula ya muzuri.
d MAFASIRIO YA PICHA: Dada fulani anasali kwa Yehova apatie Baraza Yenye Kuongoza roho yake takatifu, na asaidie wale wenye kuteseka juu ya misiba na mateso.