Waroma
12 Kwa sababu hiyo nawasihi ninyi kwa huruma za Mungu, akina ndugu, mtoe miili+ yenu iwe dhabihu+ iliyo hai,+ takatifu,+ yenye kukubalika kwa Mungu,+ utumishi mtakatifu+ pamoja na nguvu zenu za kufikiri.+ 2 Na acheni kufanyizwa+ kulingana na mfumo huu wa mambo, bali mgeuzwe kwa kufanya upya akili yenu,+ ili mjihakikishie wenyewe+ mapenzi+ ya Mungu yaliyo mema na yenye kukubalika na makamilifu.
3 Kwa maana kupitia fadhili zisizostahiliwa nilizopewa namwambia kila mtu hapo kati yenu asijifikirie mwenyewe zaidi kuliko ilivyo lazima kufikiri;+ bali kufikiri ili awe na akili timamu,+ kila mmoja kama Mungu alivyomgawia kipimo+ cha imani.+ 4 Kwa maana kama vile tulivyo na viungo vingi katika mwili mmoja,+ lakini viungo hivyo havifanyi kazi ileile, 5 ndivyo sisi, ingawa tuko wengi, ni mwili mmoja+ katika muungano na Kristo, lakini viungo ambavyo kila kimoja ni cha kile kingine.+ 6 Basi, kwa kuwa tuna zawadi zinazotofautiana+ kulingana na fadhili zisizostahiliwa+ tulizopewa, kama ni unabii, na tutoe unabii kulingana na imani tuliyogawiwa; 7 au ni huduma, na tuwe katika huduma+ hii; au yeye anayefundisha,+ na awe katika kufundisha+ kwake; 8 au yeye anayehimiza, na awe katika kuhimiza+ kwake; yeye anayegawa, na afanye hivyo kwa ukarimu;+ yeye anayesimamia,+ na afanye hivyo kwa bidii ya kweli; yeye anayeonyesha rehema,+ na afanye hivyo kwa uchangamfu.
9 Upendo+ wenu na uwe bila unafiki.+ Chukieni maovu,+ shikamaneni na mema.+ 10 Katika upendo wa kindugu+ iweni na upendo mwororo kwa mtu na mwenzake. Katika kuonyeshana heshima+ iweni wa kwanza. 11 Msiwe wavivu katika kazi zenu.+ Wakeni roho.+ Mtumikieni Yehova.+ 12 Shangilieni katika tumaini.+ Vumilieni chini ya dhiki.+ Dumuni katika sala.+ 13 Shirikini pamoja na watakatifu kulingana na mahitaji yao.+ Fuateni mwendo wa ukaribishaji-wageni.+ 14 Endeleeni kuwabariki wale wanaowatesa;+ muwe mkibariki+ wala msiwe mkilaani.+ 15 Shangilieni pamoja na watu wanaoshangilia;+ lieni pamoja na watu wanaolia. 16 Mwafikirie wengine kama vile mnavyojifikiria wenyewe;+ msiwe mkikaza akili juu ya mambo makuu,+ bali mwongozwe na mambo ya hali ya chini.+ Msiwe wenye busara machoni penu wenyewe.+
17 Msimlipe yeyote uovu kwa uovu.+ Fanyeni mambo mema machoni pa watu wote. 18 Ikiwezekana, kwa kadiri inavyowategemea ninyi, iweni wenye kufanya amani+ na watu wote. 19 Wapendwa, msijilipizie kisasi+ wenyewe bali iachieni nafasi ghadhabu;+ kwa maana imeandikwa: “Kisasi ni changu; mimi nitalipa, asema Yehova.”+ 20 Lakini, “ikiwa adui yako ana njaa, mlishe; ikiwa ana kiu, mpe kitu anywe;+ kwa maana kwa kufanya hivyo utakusanya makaa yenye moto juu ya kichwa chake.”+ 21 Usiache ushindwe na uovu, bali endelea kuushinda uovu kwa wema.+