SEPTEMBA 15-21
METHALI 31
Wimbo 135 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)
1. Masomo Tunayojifunza Kutokana na Maagizo ya Mama Mwenye Upendo
(Dak. 10)
Wafundishe watoto wako maoni ya Yehova kuhusu ngono na ndoa (Met 31:3, 10; w11 2/1 19 ¶7-8)
Wafundishe watoto wako wawe na maoni kama ya Yehova kuhusu kileo (Met 31:4-6; ijwhf makala ya 4 ¶11-13)
Wafundishe watoto wako kuwasaidia watu kama Yehova anavyofanya (Met 31:8, 9; g17.6 9 ¶5)
2. Hazina za Kiroho
(Dak. 10)
Met 31:10-31—Herufi za kialfabeti ni nini, na zilitumiwaje katika Maandiko ya Kiebrania? (w92 11/1 11 ¶7-8)
Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Met 31:10-31 (th somo la 10)
4. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 3) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Anzisha mazungumzo na mtu ambaye amesema au kutenda jambo fulani la fadhili. (lmd somo la 5 jambo kuu la 3)
5. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 4) NYUMBA KWA NYUMBA. Zungumzia moja ya “Kweli Tunazopenda Kufundisha” kutoka kwenye nyongeza A ya broshua Wapende Watu. (lmd somo la 1 jambo kuu la 4)
6. Kufuatia Upendezi
(Dak. 5) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwalike mwenye nyumba ambaye ulimwachia gazeti la Mnara wa Mlinzi Na. 1 2025 ahudhurie hotuba ya pekee. (lmd somo la 7 jambo kuu la 4)
Wimbo 121
7. Wafundishe Watoto Wako Kutumia Vifaa vya Kielektroni kwa Hekima
(Dak. 8) Mazungumzo.
Je, umewahi kumtazama mtoto mdogo akitumia programu za simu ya mkononi au tablet? Mara nyingi, inaonekana ni rahisi sana kwa watoto kutumia vifaa hivyo! Huenda wasihitaji msaada wa kujua jinsi ya kutumia vifaa, lakini sikuzote watahitaji kujifunza jinsi ya kuvitumia kwa hekima. Ikiwa wewe ni mzazi, unawezaje kumzoeza mtoto wako kutumia kifaa cha kielektroni kwa hekima?
Onyesha VIDEO Kutumia Wakati Vizuri. Kisha waulize wasikilizaji:
Kwa nini ni vizuri kujiwekea mipaka tunapotumia vifaa vya kielektroni?
Tunahitaji kutenga wakati kwa ajili ya mambo gani mengine?
Unapoweka sheria kwa ajili ya familia yako, tegemea kanuni za Biblia badala ya kutegemea kile ambacho wazazi wengine hufanya. (Gal 6:5) Kwa mfano, jiulize:
Je, mtoto wangu ameonyesha kwamba ana sifa ya kujizuia na kuwajibika kwa matendo yake vya kutosha hivi kwamba anaweza kutumia kifaa changu au hata kuwa na kifaa chake cha kielektroni?—1Ko 9:25
Ninapaswa kumsimamia mtoto wangu kwa kadiri gani anapotumia kifaa cha kielektroni?—Met 18:1
Ni programu gani za simu au tovuti nitakazomruhusu mtoto wangu kutumia na ni zipi ambazo sitamruhusu atumie?—Efe 5:3-5; Flp 4:8, 9
Ninapaswa kumruhusu mtoto atumie muda gani kwenye kifaa cha kielektroni kwa siku, ili pia awe na muda wa kutosha wa kufanya mambo yenye kufurahisha na yaliyo muhimu?—Mhu 3:1
8. Mahitaji ya Kutaniko
(Dak. 7)
9. Funzo la Biblia la Kutaniko
(Dak. 30) lfb somo la 18-19