-
Wana-Farasi Wanne Katika Mwendo!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Sura ya 16
Wana-Farasi Wanne Katika Mwendo!
Njozi ya 3—Ufunuo 6:1-17
Habari: Upandaji wa wana-farasi wanne, mashahidi wafia imani walio chinichini ya madhabahu, na siku kubwa ya hasira-jeuri
Wakati wa utimizo: Kuanzia 1914 kufikia uharibifu wa huu mfumo wa mambo
1. Yehova anaonyeshaje Yohana vilivyomo ndani ya hati-kunjo yenye kuvutia ambayo Yesu anafungua?
KATIKA siku hii yenye hatari, je! sisi hatupendezwi sana na “vitu ambavyo lazima vitukie karibuni”? Hakika tunapendezwa, kwa kuwa sisi wenyewe tunahusika! Basi acheni sisi tuandamane na Yohana wakati Yesu anapofungua hati-kunjo yenye kuvutia. Kwa kustaajabisha, Yohana halazimiki kusoma. Kwa nini sivyo? Kwa sababu vitu vilivyomo vinatolewa kwake “kwa ishara” kwa mfululizo wa mandhari zenye nguvu-msukumo, na zinazojaa matendo.—Ufunuo 1:1, 10, NW.
2. (a) Yohana anaona na kusikia nini, na kuonekana kwa kerubi kunadokeza nini? (b) Amri ya huyo kerubi wa kwanza inatolewa kwa nani, na sababu gani wewe unajibu hivyo?
2 Msikilize Yohana wakati Yesu anapofungua kifungo cha kwanza cha hati-kunjo: “Na mimi nikaona wakati Mwana-Kondoo alipofungua mmoja wa vile vifungo saba, na mimi nikasikia mmoja wa wale viumbe hai wanne akisema kwa sauti kama ya ngurumo: ‘Njoo!’” (Ufunuo 6:1, NW) Hii ni sauti ya kerubi wa kwanza. Kuonekana kwake kama simba kungemdokezea Yohana kwamba tengenezo la Yehova litatenda kwa ujasiri katika kutekeleza hukumu Zake za uadilifu. Nayo amri hiyo inatolewa kwa nani? Hangeweza kuwa Yohana, kwa kuwa Yohana alikuwa amekwisha kualikwa ashiriki mandhari hizi za kiunabii. (Ufunuo 4:1) Hiyo “sauti ya ngurumo” inawaita wajitokeze washiriki wengine katika wa kwanza wa ule mfululizo wa vituko vinne vyenye kuamsha.
Farasi Mweupe na Mpandaji Wake Mashuhuri
3. (a) Sasa Yohana anaeleza nini? (b) Kupatana na mifananisho ya Biblia, ni lazima huyo farasi mweupe atoe picha ya nini?
3 Yohana, na pamoja naye ile jamii ya Yohana na waandamani wayo leo, wanapendelewa kuona drama yenye mwendo wa kasi sana! Yohana anasema hivi: “Na mimi nikaona, na, tazama! farasi mweupe; na mmoja aliyeketi juu yake alikuwa na upinde; na taji lilipewa kwa yeye, na yeye akatoka kwenda akishinda na kukamilisha ushindi wake.” (Ufunuo 6:2, NW) Ndiyo, katika kujibu sauti yenye mngurumo “Njoo!” farasi mweupe atokea. Katika Biblia, mara nyingi farasi hufananisha vita. (Zaburi 20:7; Mithali 21:31; Isaya 31:1) Farasi huyu, yaelekea ni farasi dume mwenye sura nzuri, anameta kwa weupe unaoonyesha utakatifu usio na ila. (Linga Ufunuo 1:14; 4:4; 7:9; 20:11.) Hiyo inafaa kama nini, kwa kuwa inaonyesha vita iliyo safi na ya uadilifu machoni pa Yehova!—Ona pia Ufunuo 19:11, 14.
4. Ni nani aliye Mpandaji-farasi mweupe? Eleza.
4 Ni nani aliye Mpandaji-farasi huyu? Yeye ana upinde, silaha ya vita ya kushambulia, lakini anapewa pia taji. Wale waadilifu pekee wanaoonekana wakivaa taji katika pindi ya ile siku ya Bwana ni Yesu na ile jamii inayowakilishwa na wale wazee 24. (Danieli 7:13, 14, 27; Luka 1:31-33; Ufunuo 4:4, 10; 14:14)a Haielekei kwamba mshiriki wa kile kikundi cha wazee 24 angeonyeshwa kuwa akipokea taji kwa ustahili wake mwenyewe. Kwa sababu hiyo, huyu mpanda-farasi aliye pekee lazima awe Yesu Kristo na si mwingine. Yohana anamwona katika mbingu wakati ule wa kihistoria wenye maana kubwa katika 1914 wakati Yehova anapotangaza “Mimi, hata mimi, nimeweka mfalme wangu,” na kumwambia kwamba hili ni kwa kusudi la “kwamba mimi nipate kukupa mataifa yawe urithi wako.” (Zaburi 2:6-8, NW)b Hivyo, katika kufungua kile kifungo cha kwanza Yesu anafunua jinsi yeye mwenyewe, akiwa Mfalme ambaye amevikwa taji sasa hivi, anatoka kwenda kupiga vita katika wakati wa Mungu uliowekwa.
5. Mwandikaji wa zaburi anaelezaje habari ya Mpandaji katika njia inayofanana na Ufunuo 6:2?
5 Mandhari hii inapatana vizuri na Zaburi 45:4-7, NW, inayoelekezwa kwa Mfalme aliyeketishwa na Yehova juu ya kiti cha ufalme: “Na katika umaridadi wako songa mbele ukapate fanikio; panda kwa sababu ya ukweli na unyenyekevu na uadilifu, na mkono wa kulia wako utakufunza wewe katika vitu vyenye kuvuvia hofu. Mishale yako ni mikali—chini yako vikundi vya watu vinafuliza kuanguka—katika moyo wa maadui wa mfalme. Mungu ndiye kiti cha ufalme chako kwa wakati usio dhahiri, hata milele; fimbo ya umaliki wako ni fimbo ya unyoofu. Wewe umependa uadilifu na wewe wachukia uovu. Hiyo ndiyo sababu Mungu, Mungu wako, amepaka wewe mafuta ya mchachawo zaidi ya washirika wako.” Akiwa anazoelea elezo hili la kiunabii, Yohana anathamini kwamba linatumika kuhusu utendaji wa Yesu akiwa Mfalme.—Linga Waebrania 1:1, 2, 8, 9.
Kutoka Kwenda Akishinda
6. (a) Ni kwa nini lazima Mpandaji atoke aende akishinda? (b) Ni kupitia miaka ipi upandaji wa ushindi unaendelea?
6 Ingawa hivyo, ni kwa nini lazima huyo Mfalme mvikwa-taji sasa hivi apande hali akienda kwenye vita? Ni kwa sababu umaliki wake unasimamishwa kukiwa na upinzani mkali kutoka kwa yule hasimu mkuu wa Yehova, Shetani Ibilisi, na wale walio juu ya dunia ambao—wakijua au pasipo kujua—wanatumikia makusudi ya Shetani. Uzawa wa Ufalme wenyewe wataka kuwe vita kuu katika mbingu. Akipiga vita kwa jina Mikaeli (linalomaanisha “Ni Nani Aliye Kama Mungu?”), Yesu anamshinda Shetani na roho waovu wake na kuwavurumisha chini kwenye dunia. (Ufunuo 12:7-12) Upandaji wenye ushindi wa Yesu unaendelea kupitia miongo ya kufungua ya siku ya Bwana wakati binadamu wenye mfano wa kondoo wanakusanywa. Ijapokuwa ulimwengu kwa ujumla ungali unalala “katika uwezo wa yule mwovu,” kwa upendo Yesu anaendelea kuchunga ndugu zake wapakwa-mafuta na waandamani wenzao, akisaidia kila mmoja apate ushindi wa imani.—1 Yohana 5:19, NW.
7. Ni ushindi gani ambao Yesu amepata katika miongo ya kwanza-kwanza ya siku ya Bwana, na azimio letu lapasa liwe nini?
7 Yesu amepata ushindi gani mwingine wakati wa miaka 90 na zaidi ya siku ya Bwana? Kuzunguka tufe lote, watu wa Yehova wakiwa mmoja mmoja na wakiwa kundi, wamepatwa na magumu mengi, mikazo, na minyanyaso, inayofanana na ile aliyoieleza mtume Paulo katika kutoa ithibati ya huduma yake. (2 Wakorintho 11:23-28) Mashahidi wa Yehova wamehitaji “nguvu zinazopita zilizo za kawaida,” ili wavumilie, hasa katika sehemu za vita na jeuri. (2 Wakorintho 4:7, NW) Lakini hata katika hali zenye kujaribu zaidi Mashahidi waaminifu wameweza kusema kama alivyosema Paulo: “Bwana alisimama karibu na mimi na akatia nguvu ndani ya mimi, kwamba kupitia mimi kuhubiri kupate kutimizwa kikamili.” (2 Timotheo 4:17, NW) Ndiyo, Yesu alishinda kwa niaba yao. Naye ataendelea kwenda akishinda kwa niaba yetu, maadamu sisi tunaazimia kukamilisha ushindi wetu wa imani.—1 Yohana 5:4.
8, 9. (a) Ni ushindi gani ambao kundi la Mashahidi wa Yehova la pote katika tufe limeshiriki? (b) Ni wapi ambako ukuzi wa Mashahidi wa Yehova umekuwa wenye kutokeza kweli kweli?
8 Kundi la Mashahidi wa Yehova la pote katika tufe limeshiriki ushindi mwingi chini ya mwongozo wa Mfalme walo mwenye kushinda. Kwa kutokeza sana, yeye aliwapa himaya hawa Wanafunzi wa Biblia wasipatwe na utowesho katika 1918, wakati wao wenyewe ‘waliposhindwa’ kwa muda na tengenezo la Shetani la kisiasa. Hata hivyo, katika 1919, alivunja mapingo ya gereza awaache huru, kisha akawahuisha ili wapige mbiu ya habari njema “mpaka kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.”—Ufunuo 13:7; Matendo 1:8, NW.
9 Kabla na wakati wa Vita ya Ulimwengu 2, yale Mataifa Mhimili ya kidikteta yalijaribu kufutilia mbali Mashahidi wa Yehova katika mabara mengi ambako viongozi wa kidini, hasa mapadri wa Roma Katoliki, walitoa uungaji-mkono wa waziwazi au usio wa waziwazi kwa madikteta waonezi. Lakini Mashahidi 71,509 waliokuwa wakihubiri wakati vita ilipoanza katika 1939 wakawa 141,606 kufikia mwisho wayo katika 1945, hata ingawa zaidi ya 10,000 walikuwa wametumia miaka mirefu katika magereza na kambi za mateso, na 2,000 hivi walikuwa wameuawa. Hesabu ya Mashahidi watendaji duniani pote imepanuka kuwa zaidi ya milioni sita leo. Ukuzi umekuwa wenye kutokeza katika mabara ya Kikatoliki na katika nchi ambako minyanyaso ilikuwa mikali zaidi sana—kama Ujeremani, Italia, na Japani, ambamo Mashahidi wanaripoti jumla ya wahudumu wa shamba watendaji zaidi ya 600,000.—Isaya 54:17; Yeremia 1:17-19.
10. Ni kwa ushindi gani yule Mfalme mwenye kushinda amebariki watu wake “katika kutetea na kuthibitisha kisheria habari njema”?
10 Mfalme wetu mwenye kushinda amebariki pia watu wake wenye bidii kwa kuwaongoza kwenye ushindi mwingi “katika kutetea na kuthibitisha kisheria habari njema” katika mahakama ya sheria na mbele ya watawala. (Wafilipi 1:7; Mathayo 10:18; 24:9, NW) Hiyo imekuwa katika mataifa yote—katika Australia, Ajentina, Kanada, Ugiriki, India, Swazilandi, Swizalandi, Uturuki na mabara mengineyo. Miongoni mwa ushindi mbalimbali 50 wa kisheria waliopata Mashahidi wa Yehova katika Mahakama Kuu Zaidi Sana ya United States umekuwa ule unaohakikishia haki ya kujulisha wazi habari njema “peupe na nyumba kwa nyumba” na kutofanya sherehe za kuabudu sanamu za kizalendo. (Matendo 5:42; 20:20, NW; 1 Wakorintho 10:14) Hivyo, njia imeachwa wazi kwa ajili ya kupanua kazi ya kutoa ushahidi katika tufe lote.
11. (a) Yule Mpandaji ‘anakamilishaje ushindi wake’? (b) Kufunguliwa kwa kifungo cha pili, cha tatu, na cha nne kwapasa kuwe na tokeo gani juu yetu?
11 Yesu ‘anakamilishaje ushindi wake’?c Yeye anafanya hivyo, kama tutakavyoona, kwa kukomesha dini bandia na kisha kuvurumisha kila kisehemu kinachobaki cha tengenezo linaloonekana la Shetani ndani ya “ziwa la moto” la ufananisho wa uharibifu, katika kutetea enzi kuu ya Yehova. Kwa uhakika, sasa sisi tunatazamia siku hiyo kwenye Har–Magedoni wakati “Mfalme wa wafalme” wetu atajipatia ushindi juu ya tengenezo la Shetani la kisiasa lenye uonevu! (Ufunuo 16:16; 17:14; 19:2, 14-21; Ezekieli 25:17) Kwa wakati uliopo, Mshindi huyo asiyeshindika akiwa juu ya farasi mweupe anaendelea kupanda akisonga mbele kadiri Yehova anavyoongeza watu wenye mioyo minyofu kwenye taifa Lake lenye uadilifu duniani. (Isaya 26:2; 60:22) Je! wewe unashiriki pamoja na jamii ya Yohana iliyopakwa mafuta katika upanuzi huo wa Ufalme wenye shangwe? Ikiwa ndivyo, anachoona Yohana wakati vile vifungo vitatu vinavyofuata vinapofunguliwa bila shaka kitakuchochea wewe kwenye ushiriki mkubwa hata zaidi katika kazi ya Yehova kwa ajili ya siku hii.
Ona, Farasi wa Rangi-Moto!
12. Yesu alisema ni nini kingetia alama kuwapo kwake kusikoonekana akiwa Mfalme?
12 Kuelekea mwisho wa huduma ya Yesu duniani, wanafunzi wake walimuuliza faraghani hivi: “Ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mfumo wa mambo?” Katika kujibu, yeye alitabiri maafa ambayo yangekuwa “mwanzo wa maumivu makali ya ghafula ya taabu.” Akasema Yesu: “Taifa litainuka dhidi ya taifa, na ufalme dhidi ya ufalme; na kutakuwa na matetemeko ya dunia makubwa, na katika mahali pamoja baada ya pengine magonjwa ya kipuku na upungufu wa chakula; na kutakuwa na maono ya kutia hofu na kutoka mbinguni ishara kubwa.” (Mathayo 24:3, 7, 8; Luka 21:10, 11, NW) Vitu ambavyo Yohana anaona wakati vifungo vinavyobaki vya hati-kunjo vinapofunguliwa huandaa ulingano wa kustaajabisha wa unabii huo. Angalia sasa Yesu aliyetukuzwa afunguapo kifungo cha pili!
13. Ni tofauti gani inayokaribia kuwa wazi kwa Yohana?
13 “Na wakati yeye alipofungua kifungo cha pili, mimi nikasikia kiumbe hai wa pili akisema: ‘Njoo!’” (Ufunuo 6:3, NW) Ni yule kerubi wa pili, aliye na mwonekano wa fahali, anayetoa amri. Hapa nguvu ndiyo sifa inayofananishwa, lakini ni nguvu iliyotumiwa kwa uadilifu. Ingawa hivyo, kwa kutofautisha, sasa Yohana ataona wonyesho wenye kukirihisha sana wa nguvu, wenye kuleta kifo.
14. Ni farasi na mpandaji gani anayefuata kuonwa na Yohana, nayo njozi hii inatoa picha ya nini?
14 Basi, mwito huu “Njoo!” unajibiwaje? Katika njia hii: “Na mwingine akatokea, farasi wa rangi-moto; na yule mmoja aliyeketi juu yake alipewa ruhusa ya kuondolea mbali amani kutoka dunia ili wao wapaswe kuchinja mmoja na mwenzake; na upanga mkubwa akapewa yeye.” (Ufunuo 6:4, NW) Ni njozi ya kutia hofu kweli kweli! Na hakuna shaka juu ya inachotolea picha: vita! Si vita ya uadilifu, yenye ushindi wa Mfalme wa Yehova mwenye kushinda bali ni vita yenye ukatili ya kimataifa, yenye kufanyizwa na binadamu, yenye umwagaji-damu na maumivu ya bure. Inafaa kama nini kwamba mpandaji huyu anampanda farasi wa rangi-nyekundu kama moto!
15. Ni kwa nini haitupasi sisi tutake sehemu yoyote ya upandaji wa yule mwana-farasi wa pili?
15 Kwa hakika, Yohana hangetaka sehemu yoyote ya mwana-farasi na upandaji wake wenye haraka isiyo na akili, kwa kuwa unabii ulitolewa kuhusu watu wa Mungu hivi: “Wala hawatajifunza vita tena kamwe.” (Isaya 2:4) Ingawa wangali “katika ulimwengu,” Yohana na, kwa upanuzi, ile jamii ya Yohana na umati mkubwa leo wao “si sehemu” ya huu mfumo wenye madoa ya damu. Silaha zetu ni za kiroho na “zinajaa nguvu kwa njia ya Mungu” kwa ajili ya kupiga mbiu ya ukweli kwa bidii, bila vita ya kimwili.—Yohana 17:11, 14; 2 Wakorintho 10:3, 4, NW.
16. Ni lini na jinsi gani mpandaji-farasi mwekundu alipewa “upanga mkubwa”?
16 Kulikuwa kumekuwa na vita vingi kabla ya 1914, ule mwaka Mpandaji-farasi mweupe alipopokea taji lake. Lakini sasa mpandaji-farasi mwekundu anapewa “upanga mkubwa.” Hiyo inadokeza nini? Kwa mlipuko wa Vita ya Ulimwengu 1, vita vya binadamu vimekuwa vyenye umwagaji-damu mwingi zaidi, vyenye uharibifu mwingi zaidi ya vilivyopata kuwa kabla ya hapo. Wakati wa mwosho-damu wa 1914-18, matanki, gesi zenye sumu, eropleni, sabmarini, mizinga mikubwa, na silaha za otomatiki zilitumiwa ama kwa mara ya kwanza ama kwa kadiri isiyotangulia kufanywa. Katika mataifa yapata 28, idadi ya watu wa nchi kwa ujumla, si wale tu ambao kazi yao ya maisha ni askari-jeshi, walisukumizwa kwenye jitihada za vita. Majeruhi walikuwa kadiri ya kuogopesha. Askari-jeshi zaidi ya milioni tisa walichinjwa, na majeruhi ya raia walikuwa wengi mno. Hata ilipokwisha vita, hakukuwa na kurudia amani halisi duniani. Zaidi ya miaka 50 baada ya vita, Konrad Adenauer waziri wa serikali Mjeremani alitoa elezo hili: “Usalama na utulivu vimetoweka katika maisha ya watu tangu 1914.” Kweli kweli yule mpandaji-farasi wa rangi-moto alipewa ruhusa aondolee mbali amani duniani!
17. Utumizi wa huo “upanga mkubwa” umeendeleaje, kufuata Vita ya Ulimwengu 1?
17 Halafu, kiu yake ya kutaka kuona damu ikimwagwa ikiwa imechochewa, yule mpandaji-farasi mwekundu alijitumbukiza ndani ya Vita ya Ulimwengu 2. Zana za uchinjaji zilizidi kuwa za kishetani zaidi, nayo majeruhi yakapanda juu kuwa mara nne ya yale ya Vita ya Ulimwengu 1. Katika 1945 bomu mbili za atomu zililipuka juu ya Japani, kila mojapo ilifutilia mbali—kwa dharuba moja—makumi ya maelfu ya majeruhi. Katika pindi ya vita ya pili ya ulimwengu, yule mpandaji-farasi mwekundu alivuna mavuno makubwa ya maisha zapata milioni 55, na hata wakati huo yeye hakutosheka. Imeripotiwa kwa njia yenye kuaminika kwamba nafsi zaidi ya milioni 20 zimeanguka chini ya ule “upanga mkubwa” tangu Vita ya Ulimwengu 2.
18, 19. (a) Badala ya huo kuwa ushindi wenye shangwe wa tekinolojia ya kivita, lile chinjo tangu Vita ya Ulimwengu 2 ni uhakika wa ushuhuda gani? (b) Ni hatari gani inayokabili aina ya binadamu, lakini yule Mpandaji-farasi mweupe atafanya nini kuisawazisha?
18 Je! sisi tungeweza kuita huu kuwa ushindi wenye shangwe wa tekinolojia ya kivita? Badala ya hivyo, huo ni ushuhuda wa kwamba yule farasi mwekundu asiye na rehema yuko katika mwendo. Na mwendo huo utaishia wapi? Baadhi ya wanasayansi wanasema kwamba kuna uwezekano wa vita ya nyukilia kutokea kiaksidenti—achia mbali mteketezo mkubwa wa kinyukilia uliopangwa! Lakini kwa furaha yule Mpandaji-farasi mweupe mwenye kushinda ana fikira tofauti juu ya jambo hili.
19 Maadamu msingi wa jamii ya watu ni kiburi cha kitaifa na chuki, lazima aina ya binadamu iendelee kukalia kipipa cha hatari ya nyukilia. Hata kama mataifa yangekwangulia mbali silaha zayo za nyukilia kwa kutamauka, yangebaki na huo ujuzi. Kwa muda mfupi sana, wangeunda tena vidude vyao vya nyukilia vya uuaji-makusudi; kwa sababu hiyo, vita yoyote ikitumia silaha za kadiri ingevuvumuka upesi kama uyoga na kuwa maangamizi makubwa. Kile kiburi na chuki inayofunika mataifa leo lazima viongoze kwenye ujiuaji wa binadamu, isipokuwa—aha, ndiyo, isipokuwa yule Mpandaji-farasi mweupe ageuzie mbali mwendo wa kichaa wa yule mpandwaji wa rangi-moto. Acheni sisi tuwe na uhakika kwamba Kristo Mfalme atapanda, ili akamilishe ushindi wake juu ya ulimwengu wenye kudhibitiwa na Shetani na pia ili asimamishe jamii mpya ya kidunia ambayo msingi wayo ni upendo—upendo kwa Mungu na kwa jirani—kani kwa ajili ya amani, iliyo ya juu zaidi ya ile yenye kutikisika ya mazuio ya vita ya nyakati zetu zenye kichaa.—Zaburi 37:9-11; Marko 12:29-31; Ufunuo 21:1-5.
Farasi Mweusi Aruka Kuja Mbele
20. Sisi tuna uhakikisho gani kwamba Mpandaji-farasi mweupe ataiweza hali yoyote yenye balaa?
20 Yesu anafungua sasa kifungo cha tatu! Yohana, unaona nini? “Na wakati yeye alipofungua kifungo cha tatu, mimi nikasikia kiumbe hai wa tatu akisema: ‘Njoo!’” (Ufunuo 6:5a, NW) Kwa furaha kerubi huyu wa tatu “ana uso kama wa binadamu,” kuonyesha sifa ya upendo. Upendo wenye kuongozwa na kanuni utakuwa mwingi sana katika ulimwengu mpya wa Mungu, hata kama vile sifa hiyo nzuri sana inavyoenea katika tengenezo lote la Yehova leo. (Ufunuo 4:7; 1 Yohana 4:16) Sisi tunaweza kuwa na hakika kwamba Mpandaji-farasi mweupe, ambaye “lazima atawale akiwa mfalme mpaka Mungu awe ameweka maadui wote chini ya nyayo zake,” kwa upendo ataondoa ile hali yenye maafa ambayo inafuata kuletwa kwenye uchunguzi wa Yohana.—1 Wakorintho 15:25, NW.
21. (a) Ni nini kinachotolewa picha na yule farasi mweusi na mpandaji wake? (b) Ni nini kinachothibitisha kwamba huyo farasi mweusi angali katika mwendo wake wenye ukali?
21 Basi, Yohana anaona nini, wakati ule mwito wa tatu “Njoo!” unapojibiwa? “Na mimi nikaona, na, tazama! farasi mweusi ti; na mmoja aliyeketi juu yake alikuwa na jozi ya mizani katika mkono wake.” (Ufunuo 6:5b, NW) Njaa tupu! Huo ndio ujumbe wa kutisha wa mandhari hii ya kiunabii. Unaelekeza mbele kwenye hali za mapema katika siku ya Bwana wakati lazima chakula kipimwe kwa mizani. Tangu 1914 njaa imekuwa tatizo la ulimwenguni pote lenye kuendelea. Vita vya ki-siku-hizi huleta njaa ikifuatana navyo, kwa kuwa rasilimali ambazo kwa kawaida hutumiwa kulisha watu wenye njaa mara nyingi hugeuzwa na kutumiwa kutoa ugavi wa silaha za vita. Wafanya kazi wa mashamba wanaingizwa jeshini kwa nguvu, nazo sera zinazokataza kulima nyanja zenye makovu ya vita na dunia iliyounguzwa hupunguza uzalishaji wa chakula. Hiyo ilikuwa kweli kama nini wakati wa vita ya kwanza ya ulimwengu, mamilioni yalipotaabishwa na njaa na wakafa! Zaidi ya hilo, yule mpandaji-farasi mweusi wa njaa hakuacha ilipoisha vita. Wakati wa muda wa tangu 1930, milioni tano walipotea katika njaa moja tu katika Ukraine. Ile vita ya pili ya ulimwengu ilileta pamoja nayo upungufu zaidi wa chakula na njaa. Kadiri yule farasi mweusi alivyoendelea na mwendo wake, Baraza la Chakula Ulimwenguni liliripoti katikati ya 1987 kwamba binadamu milioni 512 walikuwa wakifa njaa na kwamba watoto 40,000 wanakufa kila siku kwa visababishi vinavyohusiana na njaa.
22. (a) Sauti inasema nini, ikionyesha uhitaji gani? (b) Ni jambo gani linalodokezwa na bei ya kwarti moja ya ngano na kwarti tatu za shayiri?
22 Je! Yohana ana zaidi ya kutuambia sisi: “Na mimi nilisikia sauti kana kwamba ni katikati ya viumbe hai wanne ikisema: ‘Kwarti moja ya ngano kwa dinari moja, na kwarti tatu za shayiri kwa dinari moja; na usidhuru mafuta ya zeituni na divai.’” (Ufunuo 6:6, NW) Makerubi wote wanne wana umoja katika kuonyesha uhitaji wa kulinda ugavi wa chakula kwa uangalifu—kama vile watu walikuwa hawana budi ‘kula chakula kwa uzani na katika ujalifu wenye wasiwasi’ kabla ya uharibifu wa Yerusalemu katika 607 K.W.K. (Ezekieli 4:16, NW) Katika wakati wa Yohana, kwarti ya ngano ilihesabiwa kuwa ndiyo posho ya kila siku ya askari-jeshi. Posho kama hiyo ingegharimu kiasi gani? Dinari moja—mshahara wa siku nzima! (Mathayo 20:2)d Namna gani kama mtu alikuwa na jamaa? Basi, badala ya hiyo yeye angeweza kununua kwarti tatu za shayiri isiyosafishwa. Hata hiyo ingeweza kulisha jamaa ndogo tu. Na shayiri haikuonwa kuwa chakula bora kama vile ngano.
23. Ni nini kinachodokezwa na taarifa, “Usidhuru mafuta ya zeituni na divai”?
23 Ni nini kinachodokezwa na taarifa, “Usidhuru mafuta ya zeituni na divai”? Wengine wameiona kuwa ikimaanisha kwamba ingawa wengi wangepungukiwa na chakula na hata wafe njaa, vitu vya anasa vya matajiri havingedhuriwa. Lakini katika Mashariki ya Kati, mafuta na divai si vitu vya anasa kwa kweli. Katika nyakati za Biblia, mkate, mafuta, na divai vilionwa kuwa chakula kikuu. (Linga Mwanzo 14:18; Zaburi 104:14, 15.) Sikuzote maji hayakuwa safi, kwa hiyo divai ilitumiwa sana kwa kunywa na nyakati nyingine kwa makusudi ya kitiba. (1 Timotheo 5:23) Kwa habari ya mafuta, katika siku ya Eliya mjane wa Sarepta, ajapokuwa maskini, bado alikuwa amebakiza mafuta kiasi fulani ya kupikia unga wake uliobaki. (1 Wafalme 17:12) Kwa hiyo, amri “usidhuru mafuta ya zeituni na divai” inaonekana kuwa shauri la kutotumia bidhaa hizo za msingi kwa uharaka mno lakini kuzitumia kwa kulimbika. La sivyo, ‘zitadhuriwa,’ yaani, zitakwisha kabla ya njaa kwisha.
24. Ni kwa nini farasi mweusi hataendelea na mwendo wake kwa muda zaidi ulio mrefu?
24 Jinsi tunavyoweza kuwa na furaha kwamba yule Mpandaji-farasi mweupe karibuni atazuia kwa hatamu mwendo wa farasi huyo mweusi! Kwa maana imeandikwa kuhusu uandalizi Wake wa upendo kwa ajili ya ulimwengu mpya hivi: “Katika siku zake mwadilifu atachipuka, na wingi wa amani mpaka mwezi uwe haupo tena. . . . Kutakuja kuwa na utele wa nafaka juu ya dunia; juu ya kilele cha milima kutakuwa na mfuriko.”—Zaburi 72:7, 16, NW; ona pia Isaya 25:6-8.
Farasi Rangi Nyeupe-Nyeupe na Mpandaji Wake
25. Wakati Yesu anapofungua kifungo cha tatu, Yohana anasikia sauti ya nani, na hiyo inaonyesha nini?
25 Hadithi haijaisha kabisa kusimuliwa. Yesu anafungua kifungo cha nne, naye Yohana anatusimulia tokeo: “Na wakati yeye alipofungua kifungo cha nne, mimi nikasikia sauti ya kiumbe hai wa nne ikisema: ‘Njoo!’” (Ufunuo 6:7, NW) Hii ni sauti ya kerubi anayeshabihi tai arukaye. Hekima yenye kuona mbali ndiyo inayoonyeshwa hapa, na kweli kweli Yohana, jamii ya Yohana, na wengine wote wa watumishi wa Mungu duniani wamehitaji kuona na kutenda kwa muono-ndani kwa sababu ya kinachoonyeshwa na picha hapa. Kwa kufanya hivyo, sisi tunaweza kupata kadiri fulani ya himaya tusipatwe na mapigo yanayosumbua wenye hekima ya kilimwengu wa kizazi cha leo chenye kiburi na utovu wa maadili.—1 Wakorintho 1:20, 21.
26. (a) Mwana-farasi wa nne ni nani, na ni kwa nini rangi ya farasi wake inafaa? (b) Ni nani anayemfuata mwana-farasi wa nne, na ni nini kinachopata majeruhi wake?
26 Basi, ni hofu gani mpya zinazoachiliwa, wakati mwana-farasi wa nne anapoitikia mwito? Yohana anatusimulia hivi: “Na mimi nikaona, na, tazama! farasi rangi nyeupe-nyeupe; na mmoja aliyeketi juu yake alikuwa na jina Kifo. Na Hadesi alikuwa akifuata yeye karibu-karibu.” (Ufunuo 6:8a, NW) Mpandaji-farasi wa mwisho ana jina: Kifo. Ni yeye pekee kati ya hao wana-farasi wanne wa Apokalipsi ambaye amefunua jina lake hivyo moja kwa moja. Kwa kufaa, Kifo hupanda farasi ambaye ni rangi nyeupe-nyeupe, kwa kuwa neno -eupe-eupe (Kigiriki, khlo·rosʹ) hutumiwa katika fasihi za Kigiriki kueleza nyuso ambazo zimefanywa kuwa nyeupe, kana kwamba kwa kifo. Pia kwa kufaa, Kifo kinafuatwa karibu-karibu na Hadesi (kaburi kwa ujumla) kwa njia fulani isiyoelezwa, kwa kuwa Hadesi hupokea ndani yake idadi iliyo kubwa zaidi ya wale wanaokuwa majeruhi wa mikumbo ya huyo mwana-farasi wa nne. Kwa furaha, kwa hao kutakuwako ufufuo, wakati ‘kifo na Hadesi vinapotoa wafu walio ndani yavyo.’ (Ufunuo 20:13, NW) Lakini Kifo kinadaije hao majeruhi?
27. (a) Mpandaji Kifo anadaije majeruhi wake? (b) Ni nini kinachomaanishwa na “sehemu ya nne ya dunia” ambayo juu yayo Kifo ana mamlaka?
27 Njozi inataja baadhi ya njia hizo: “Na wao walipewa mamlaka juu ya sehemu ya nne ya dunia, kuua kwa upanga mrefu na kwa upungufu wa chakula na kwa tauni yenye kufisha na kwa hayawani-mwitu wa dunia.” (Ufunuo 6:8b, NW) La, hasha, si sehemu ya nne halisi ya idadi ya watu wa dunia lakini fungu kubwa la dunia, iwe inasongamana watu au inakaliwa na wachache, ingeathiriwa na upandaji huu. Mwana-farasi huyu anavuna majeruhi ya ule upanga mkubwa wa mwana-farasi wa pili na njaa na upungufu wa chakula wa yule wa tatu. Vilevile, anavuna vuno lake mwenyewe kutokana na tauni yenye kufisha na pia vuno kutokana na matetemeko ya dunia, kama inavyoelezwa kwenye Luka 21:10, 11, NW.
28. (a) Kumekuwaje na utimizo wa unabii kuhusu “tauni yenye kufisha”? (b) Watu wa Yehova wamepewaje himaya juu ya magonjwa mengi leo?
28 Lenye umaana wa kisasa hapa ni “tauni yenye kufisha.” Kufuata mikumbo ya Vita ya Ulimwengu 1, homa-mafua ya Hispania ilivuna maisha za binadamu milioni 20 katika miezi michache tu ya 1918-19. Eneo pekee duniani lililoepuka pigo hili ni kisiwa kidogo cha St. Helena. Katika mahali ambako idadi ya watu waliuawa sana na ugonjwa huu marundo ya kuni za maziko yaliwashwa ili kuchoma maiti chunguchungu. Na leo kuna tukio lenye kuogofya la ugonjwa wa moyo na kansa, na chenye kuyasababisha sana ni uchafuzi wa tumbako. Katika kile kilichoelezwa kuwa “mwongo wenye sura mbaya” wa miaka ya 1980, njia ya maisha ambayo ni ya uasi wa sheria kulingana na viwango vya Biblia iliongeza lile pigo la UKIMWI kwa ile “tauni yenye kufisha.” Katika mwaka wa 2,000, iliripotiwa kwamba daktari mkuu wa Marekani alisema kwamba “huenda [UKIMWI] ndio ugonjwa mbaya zaidi wenye kuambukiza uliopata kutokea ulimwenguni.” Alisema kwamba watu milioni 52 ulimwenguni pote walikuwa na virusi vya UKIMWI, na milioni 20 kati yao tayari walikuwa wamekufa. Jinsi watu wa Yehova walivyo wenye shukrani kwamba lile shauri la hekima la Neno lake linawaepusha na uasherati na tumizi baya la damu, ambalo kupitia kwalo magonjwa mengi sana yanapitishwa leo!—Matendo 15:28, 29, NW; linga 1 Wakorintho 6:9-11.
29, 30. (a) Kungekuwa na tumizi gani leo la yale ‘matendo manne yenye kudhuru’ ya Ezekieli 14:21? (b) Sisi tuelewe nini kwa usemi “hayawani-mwitu” wa Ufunuo 6:8? (c) Ni nini linaloonekana kuwa jambo kuu la mandhari hiyo ya kiunabii?
29 Njozi ya Yohana hutaja hayawani-mwitu kuwa kisababishi cha nne cha kifo cha mapema. Kweli kweli, hivyo vitu vinne vilivyoonyeshwa kwa kufunguliwa kwa kifungo cha nne—vita, njaa, ugonjwa, na hayawani-mwitu—vilionwa katika nyakati za kale kuwa visababishi vikuu vya kifo cha mapema. Hivyo vingetangulia kuweka kivuli cha visababishi vyote vya kifo cha mapema leo. Ni kama vile Yehova alivyoonya Israeli: “Ndivyo, vilevile, itakuwa wakati kutakuwa matendo yangu manne yenye kudhuru ya hukumu—upanga na njaa na hayawani-mwitu wenye kudhuru na ugonjwa wa kipuku—ambayo mimi hakika nitapeleka juu ya Yerusalemu ili kukatilia mbali kutoka hilo mwanadamu wa dunia na mnyama wa nyumbani.”—Ezekieli 14:21, NW.
30 Si mara nyingi ambapo vifo vinavyoletwa na hayawani-mwitu vimekuwa vichwa vikuu magazetini katika nyakati za ki-siku-hizi, ingawa katika nchi za kitropiki wanyama-mwitu wamezidi kudai majeruhi. Katika wakati ujao, huenda wakadai hata zaidi ikiwa mabara yanaachwa ukiwa kwa sababu ya vita au watu wanadhoofishwa mno na njaa wasiweze kufukuzia mbali wanyama wenye njaa. Kwa kuongezea, kuna binadamu wengi sana leo ambao, kama wanyama wasiofikiri, wanaonyesha mielekeo ya kihayawani tofauti kabisa na ile inayoelezwa kwenye Isaya 11:6-9. Watu hawa ndio sana sana walio na daraka la mweneo wa pote katika tufe wa uhalifu unaohusiana na ngono, uuaji-makusudi, uvamizi-haramu, na milipuko ya mabomu katika ulimwengu wa ki-siku-hizi. (Linga Ezekieli 21:31; Warumi 1:28-31; 2 Petro 2:12.) Yule mwana-farasi wa nne huvuna majeruhi wao vilevile. Kweli kweli, jambo kuu la mandhari hii ya kiunabii linaonekana kuwa kwamba yule mpandaji-farasi rangi nyeupe-nyeupe huvuna kwa njia nyingi kifo cha mapema cha aina ya binadamu.
31. Ijapokuwa mikumbo inayosababishwa na wale wapandaji-farasi mwekundu, mweusi, na mweupe-mweupe, ni kwa sababu gani sisi tunaweza kutiwa moyo?
31 Ile habari iliyofunuliwa kwa kufunguliwa vile vifungo vinne vya kwanza hutumainisha sisi kwa sababu inatufundisha kutotamaushwa na vita, njaa, magonjwa, na visababishi vingine vya kifo cha mapema ambavyo vinaenea sana leo; wala haitupasi kupoteza tumaini kwa sababu viongozi wa kibinadamu wameshindwa kutatua matatizo ya sasa. Ikiwa hali za ulimwengu zinaifanya iwe wazi kwamba wale wapandaji-farasi mwekundu, mweusi, na rangi nyeupe-nyeupe wako kotekote, usisahau kwamba Mpandaji-farasi mweupe alikuwa wa awali kuanza upandaji wake. Yesu amekuwa Mfalme, na tayari yeye ameshinda kwa kadiri ya kumtupa Shetani nje ya mbingu. Ushindi wake mwingine mbalimbali unatia ndani kukusanywa kwa mabaki ya wana wa Israeli wa kiroho na umati mkubwa wa kimataifa, unaofikia hesabu ya mamilioni, ili wakaokolewe kupitia ile dhiki kubwa. (Ufunuo 7:4, 9, 14) Upandaji wake lazima uendelee mpaka akamilishapo ushindi wake.
32. Ni nini kinachotofautisha kufunguliwa kwa kila kimoja cha vifungo vinne vya kwanza?
32 Kufunguliwa kwa kila kimoja cha hivyo vifungo vya kwanza kumefuatwa na ule mwito: “Njoo!” Kila wakati, farasi na mpandaji wake walitoka wakiwa katika mwendo. Kuanzia na kifungo cha tano, sisi hatusikii tena mwito kama huo. Lakini wana-farasi hao wangali wanapanda, nao wataendelea katika mwendo muda wote wa huu umalizio wa mfumo wa mambo. (Linga Mathayo 28:20.) Ni matukio gani mengine yenye maana kubwa ambayo Yesu anafunua anapofungua vifungo vitatu vinavyobaki? Baadhi ya matukio ni yasiyoonekana na macho ya kibinadamu. Mengine, ingawa ni yenye kuonekana, bado ni ya wakati ujao. Hata hivyo, utimizo wayo ni hakika. Acheni sisi tuone ni matukio gani hayo.
[Maelezo ya Chini]
a Hata hivyo, angalia kwamba “mwanamke” wa Ufunuo 12:1 ana “taji la nyota kumi na mbili” la kitamathali.
b Kupata ithibati yenye maelezo mengi ya kwamba Yesu aliingia katika Ufalme wake katika 1914, ona ukurasa wa 215-218 wa kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.
c Ingawa tafsiri nyingi hufasiri fungu hili la maneno “kushinda” (Swahili Union Version, Revised Standard, The New English Bible, King James Version) “akiwa amenuia kupata ushindi” (Phillips, New International Version), tumizi hapa la namna ya kitenzi katika Kigiriki asilia bila kuonyesha kukamilika au muda wa tendo hutoa maana ya ukamilisho au mwisho kabisa. Kwa sababu hiyo, Word Pictures in the New Testament cha Roberts hutoa elezo hili: “Kitenzi-wakati hapa cha kutoonyesha kukamilika au muda wa tendo huelekeza kwenye ushindi wa mwisho kabisa.”
d Ona New World Translation Reference Bible, kielezi cha chini.
-
-
Wana-Farasi Wanne Katika Mwendo!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
[Picha katika ukurasa wa 92]
Yule Mfalme Apanda kwa Ushindi
Katika Miaka ya 1930 na 1940, maadui wenye kujikaza walijaribu kufanya ionekane kwamba huduma ya Mashahidi wa Yehova ilikuwa haramu, yenye uhalifu, au hata yenye kufitini serikali. (Zaburi 94:20) Katika mwaka 1936 pekee, kulikuwako kutiwa mbaroni kulikorekodiwa 1,149 katika United States. Mashahidi walipiga vita ya kesi za kisheria mwendo wote kufikia ile Mahakama Kuu Zaidi Sana, na ufuatao ni baadhi ya ushindi wao mbalimbali wenye kutokeza.
Katika Mei 3, 1943, Mahakama Kuu Zaidi Sana katika kesi ya Murdock v. Pennsylvania iliamua kwamba Mashahidi hawakuhitaji leseni ili waangushe vitabu kwa pesa. Siku iyo hiyo, ule uamuzi katika kesi ya Martin v. City of Struthers ulishikilia kwamba si kinyume cha sheria kupiga kengele ya mlango wakati wa kushiriki kugawa karatasi na vitu vingine vya kuvumisha habari.
Katika Juni 14, 1943, Mahakama Kuu Zaidi Sana iliamua katika kesi ya Taylor v. Mississippi kwamba Mashahidi hawakutia moyo utovu wa ushikamanifu kwa serikali kwa kuhubiri kwao. Siku iyo hiyo, katika kesi ya West Virginia State Board of Education v. Barnette, Mahakama hiyo ilishikilia kwamba baraza la shule halikuwa na haki ya kufukuza kutoka shuleni watoto wa Mashahidi wa Yehova waliokataa kusalimu bendera. Kesho yake yenyewe, Mahakama Kuu ya Australia iliyojaa iliondoa marufuku ambayo nchi hiyo iliwekea Mashahidi wa Yehova, hiyo ikitangazwa kuwa “isiyo ya haki, bila sababu nzuri na yenye uonevu.”
[Picha katika ukurasa wa 94]
“Alipewa Ruhusa Kuondolea Mbali Amani Kutoka Dunia”
Tekinolojia inaongoza wapi? The Globe and Mail, Toronto, Kanada, Januari 22, 1987, iliripoti yafuatayo kutokana na hotuba ya Ivan L. Head, msimamizi wa International Development Research Centre:
“Inakadiriwa kwa njia yenye kutegemeka kwamba mmoja wa kila wanasayansi na wanatekinolojia wanne katika ulimwengu wanaofanya utafiti na usitawishi anafanya kazi ya kuunda silaha. . . . Kwa makadirio ya 1986, gharama ni zaidi ya dola milioni 1.5 kwa dakika. . . . Je! sisi sote ni wenye usalama zaidi kama tokeo la mkazo wa aina hii ya tekinolojia? Silaha za nyukilia yalizo nazo yale mataifa yenye nguvu zaidi zina kani ya baruti ya zana zote za vita zilizotumiwa na wapiganaji wote katika Vita ya Ulimwengu 2 yote—mara 6,000. Vita ya Ulimwengu 2 elfu sita. Tangu 1945, kumekuwa na [muda] ulio punde ya majuma saba wakati ulimwengu umekuwa bila utendaji wa kivita. Kumekuwako zaidi ya vita 150 vya asilia ya kimataifa au vya raia wenyewe kwa wenyewe, ambavyo vimekadiriwa kuwa vilidai maisha milioni 19.3, vingi vyavyo vikiwa ni tokeo la tekinolojia mpya zenye usahihi zaidi ambazo zimezuka katika wakati huu wa Umoja wa Mataifa.”
Kufikia 2005, utendaji wa kijeshi ulikuwa umesababisha vifo zaidi ya milioni 20.
-
-
‘Nafsi Zilizochinjwa’ ZathawabishwaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Sura ya 17
‘Nafsi Zilizochinjwa’ Zathawabishwa
1. Sisi tunaishi katika kipindi cha wakati gani, na kuna ithibati gani ya hili?
UFALME wa Mungu watawala! Yule Mpandaji-farasi mweupe anakaribia kukamilisha ushindi wake! Farasi mwekundu, farasi mweusi, na farasi rangi nyeupe-nyeupe wamo katika mwendo kotekote duniani! Pasipo kukanushika, unabii wa Yesu mwenyewe kuhusu kuwapo kwake kwa kifalme unatimizwa. (Mathayo, sura 24, 25; Marko, sura 13; Luka, sura 21) Ndiyo, sisi tunaishi katika siku za mwisho za huu mfumo wa mambo. (2 Timotheo 3:1-5) Kwa kuwa ndivyo, acheni sisi tutoe uangalifu wa makini wakati Mwana-Kondoo, Yesu Kristo, anapovunja na kufungua kifungo cha tano cha hati-kunjo. Sasa ni ufunuo gani zaidi ambao sisi tutashiriki?
2. (a) Yohana aliona nini wakati kifungo cha tano kilipofunguliwa? (b) Ni kwa nini haitupasi kushangaa kusoma juu ya madhabahu ya ufananisho katika mbingu?
2 Yohana anaeleza habari ya mandhari yenye kutoza huruma: “Na wakati alipofungua kifungo cha tano, mimi nikaona chini-chini ya madhabahu nafsi za wale waliochinjwa kwa sababu ya Neno la Mungu na kwa sababu ya kazi ya ushuhuda ambayo walizoea kuwa nayo.” (Ufunuo 6:9, NW) Ni nini hiyo? Madhabahu ya kidhabihu juu mbinguni? Ndiyo! Ndio wakati wa kwanza ambapo Yohana anataja madhabahu. Ingawa hivyo, Yohana amekwisha eleza habari za Yehova akiwa ameketi juu ya kiti cha ufalme Chake, makerubi wanaozunguka, bahari ya kioo, taa, na wazee 24 wanaopeleka uvumba—vyote hivyo vikiwa mshabaha wa vitu vya tabenakulo ya kidunia, patakatifu pa Yehova katika Israeli. (Kutoka 25:17, 18; 40:24-27, 30-32; 1 Nyakati 24:4) Basi, je! itushangaze kuona pia madhabahu ya ufananisho katika mbingu?—Kutoka 40:29.
3. (a) Kwenye tabenakulo ya Kiyahudi ya kale, nafsi zilimwagwaje “penye msingi wa madhabahu”? (b) Ni kwa nini Yohana aliona nafsi za mashahidi waliochinjwa zikiwa chini-chini ya madhabahu ya ufananisho katika mbingu?
3 Chini-chini ya madhabahu hii ziko “nafsi za wale waliochinjwa kwa sababu ya Neno la Mungu na kwa sababu ya kazi ya ushuhuda ambayo walizoea kuwa nayo.” Hii humaanisha nini? Hizi hazingekuwa nafsi zilizoachanishwa na mwili—kama zile walizoamini Wagiriki wapagani. (Mwanzo 2:7; Ezekieli 18:4, ZSB) Badala ya hivyo, Yohana anajua kwamba nafsi, au uhai, hufananishwa na damu, na wakati makuhani kwenye tabenakulo ya kale ya Kiyahudi walipochinja mnyama wa dhabihu, wao walinyunyiza damu “kuzunguka pande zote juu ya madhabahu” au “penye msingi wa madhabahu ya toleo la kuteketezwa.” (Walawi 3:2, 8, 13; 4:7; 17:6, 11, 12, NW) Kwa sababu hiyo, nafsi ya mnyama ilishirikishwa karibu-karibu na madhabahu. Lakini ni kwa sababu gani nafsi, au damu, za hawa watumishi wa Mungu hasa zionwe chini-chini ya madhabahu ya ufananisho katika mbingu? Ni kwa sababu kifo chao huonwa kuwa cha kidhabihu.
4. Ni katika njia gani kifo cha Wakristo waliozaliwa kwa roho ni cha kidhabihu?
4 Kweli kweli, wale wote wanaozaliwa kuwa wana wa roho wa Mungu wanakufa kifo cha kidhabihu. Kwa sababu ya daraka wanalopaswa kushiriki katika Ufalme wa Yehova wa kimbingu, ni mapenzi ya Mungu kwamba wakane kabisa kabisa na wadhabihu tumaini lolote la uhai wa milele duniani. Katika njia hii, wao wanajitiisha kwenye kifo cha kidhabihu kwa ajili ya enzi kuu ya Yehova. (Wafilipi 3:8-11; linga 2:17.) Hiyo ni kweli katika maana halisi kabisa kwa habari ya wale ambao Yohana aliona chini ya madhabahu. Wao walikuwa wapakwa-mafuta ambao katika siku yao walifia imani kwa ajili ya huduma yao ya bidii katika kutegemeza Neno na enzi kuu ya Yehova. ‘Nafsi zao zilichinjwa kwa sababu ya Neno la Mungu na kwa sababu ya kazi ya ushuhuda [mar·ty·riʹan] ambayo walizoea kuwa nayo.’
5. Ni kwa jinsi gani nafsi za waaminifu, zijapokuwa zimekufa, zinalia kwa sauti kubwa ili kisasi kilipwe?
5 Ule mfululizo wa mandhari waendelea kufunguka: “Na hizo zikalia kwa sauti kubwa, zikisema: ‘Ni mpaka lini, Bwana Mwenye Enzi Kuu mtakatifu na wa kweli, wewe unajizuia usihukumu na kulipiza kisasi damu yetu juu ya wale ambao wanakaa juu ya dunia?’” (Ufunuo 6:10, NW) Nafsi zao, au damu, zingeweza kuliaje kwa kutaka kisasi, kwa kuwa Biblia inaonyesha kwamba wafu hawana fahamu? (Mhubiri 9:5) Basi, je! damu ya Abeli mwadilifu haikulia kwa sauti kubwa wakati Kaini alipomwua kimakusudi? Ndipo Yehova alipomwambia Kaini hivi: “Wewe umefanya nini? Sikiliza! Damu ya ndugu yako inanililia mimi kwa sauti kubwa kutoka ardhi.” (Mwanzo 4:10, 11, NW; Waebrania 12:24) Si kwamba damu ya Abeli ilikuwa ikitamka maneno kihalisi. Badala ya hivyo, Abeli alikuwa amekufa akiwa jeruhi asiye na hatia, nayo haki ililia kwa sauti kubwa ikitaka mwuaji kimakusudi wake aadhibiwe. Hali moja na hiyo, Wakristo hao wafia-imani hawana hatia, na kwa haki lazima walipiwe kisasi. (Luka 18:7, 8) Kilio cha kutaka kisasi kilipwe ni kikuu kwa sababu maelfu wengi wamekufa.—Linga Yeremia 15:15, 16.
6. Ni umwagaji-damu gani usio na hatia uliolipizwa kisasi katika 607 K.W.K.?
6 Hali hiyo ingeweza kufananishwa pia na ile iliyokuwa Yuda yenye kuasi imani wakati Mfalme Manase alipokuja kukalia kiti cha ufalme katika 716 K.W.K. Yeye alimwaga damu nyingi isiyo na hatia, pengine ‘akimpasua vipande vipande kwa msumeno’ nabii Isaya. (Waebrania 11:37, NW; 2 Wafalme 21:16) Ijapokuwa baadaye Manase alitubu na akabadilika, hiyo hatia ya damu ilibaki. Katika 607 K.W.K., wakati Wababuloni walipouacha ukiwa ufalme wa Yuda, “ilikuwa tu kwa amri ya Yehova kwamba hilo likatukia dhidi ya Yuda, kuiondoa machoni pake kwa ajili ya madhambi ya Manase, kulingana na yale yote ambayo yeye alikuwa amefanya; na pia kwa ajili ya damu isiyo na hatia ambayo yeye alikuwa amemwaga, hivi kwamba yeye alijaza Yerusalemu damu isiyo na hatia, na Yehova hakuidhini kutoa msamaha.”—2 Wafalme 24:3, 4, NW.
7. Ni nani hasa mwenye hatia ya ‘umwagaji-damu ya watakatifu’?
7 Kama vile katika nyakati za Biblia, ndivyo na leo, wengi wa wale watu mmoja mmoja walioua mashahidi wa Mungu huenda wamekufa kitambo. Lakini tengenezo lililosababisha ufia-imani wao lingali hai sana na ni lenye hatia ya damu. Ni tengenezo la Shetani la kidunia, mbegu yake ya kidunia. Sehemu yenye kutokeza katika hiyo ni Babuloni Mkubwa, ile milki ya ulimwengu ya dini bandia.a Yeye anaelezwa kuwa ‘amelewa kwa damu ya watakatifu na kwa damu ya mashahidi wa Yesu.’ Ndiyo, “katika yeye ilipatikana damu ya manabii na ya watakatifu na ya wale wote ambao wamechinjwa juu ya dunia.” (Ufunuo 17:5, 6; 18:24; Waefeso 4:11; 1 Wakorintho 12:28, NW) Ni mzigo wa hatia ya damu kama nini! Maadamu Babuloni Mkubwa yupo, damu ya majeruhi wake italia kwa sauti kubwa kwa kutaka haki itekelezwe.—Ufunuo 19:1, 2.
8. (a) Ni mifano gani ya ufia-imani iliyokuwa imetukia wakati wa maisha ya Yohana? (b) Ni minyanyaso gani iliyochochewa na wamaliki Waroma?
8 Yohana mwenyewe alishuhudia ufia-imani katika karne ya kwanza wakati Nyoka mkatili na mbegu yake ya kidunia walipopiga vita juu ya kundi la Wakristo wapakwa-mafuta lililokuwa likikua. Yohana alikuwa ameona Bwana yetu akitundikwa juu ya nguzo na alikuwa ameishi kupitia vipindi vya kuuawa kwa Stefano, kwa ndugu yake mwenyewe Yakobo, na kwa Petro, kwa Paulo, na washiriki wengine wa karibu. (Yohana 19:26, 27; 21:15, 18, 19; Matendo 7:59, 60; 8:2; 12:2; 2 Timotheo 1:1; 4:6, 7) Katika 64 W.K., Nero, maliki Mroma alikuwa amelaumu bure Wakristo, akiwashtakia kuteketeza jiji, ili kukanusha uvumi wa kwamba ndiye aliyekuwa mwenye hatia. Mwanahistoria Takito anaripoti hivi: “Wao [Wakristo] walikufa kwa njia za dhihaka; baadhi yao walifunikwa ngozi za hayawani-mwitu kisha wakararuliwa na mbwa, baadhi yao [walitundikwa juu ya nguzo],b baadhi yao walichomwa kuwa mienge ya kunurisha usiku.” Wimbi zaidi la mnyanyaso chini ya Maliki Domitiano (81-96 W.K.) lilikuwa limetokeza kuhamishwa kwa Yohana kupelekwa kisiwa cha Patmosi. Kama Yesu alivyosema: “Ikiwa wao wamenyanyasa mimi, wao watanyanyasa nyinyi pia.”—Yohana 15:20; Mathayo 10:22, NW.
9. (a) Ni kipeo gani cha udanganyifu alichotokeza Shetani kufikia karne ya nne W.K., nacho ni sehemu kuu ya nini? (b) Baadhi ya watawala wa Jumuiya ya Wakristo waliwatendeaje Mashahidi wa Yehova wakati wa Vita ya Ulimwengu 1 na 2?
9 Kufikia karne ya nne W.K., yule nyoka wa zamani, Shetani Ibilisi, alikuwa ametokeza kipeo cha udanganyifu wake, ile dini yenye uasi-imani ya Jumuiya ya Wakristo—mfumo wa Kibabuloni uliofichwa chini ya kibandiko cha “Ukristo.” Ndiyo sehemu iliyo kuu ya mbegu ya yule Nyoka na imesitawi ikawa umati wa farakano zenye kuhitilafiana. Kama Yuda ya kale isiyo na imani, Jumuiya ya Wakristo inabeba hatia nzito ya damu, ikiwa imekwisha kujihusisha sana katika pande zote mbili za Vita ya Ulimwengu 1 na 2. Wengine wa watawala wa kisiasa wa Jumuiya ya Wakristo hata walitumia vita hivyo kuwa kisababu cha kuchinja watumishi wa Mungu. Likiripoti juu ya Hitla kunyanyasa Mashahidi wa Yehova, pitio la kitabu Kirchenkampf in Deutschland (Vita ya Makanisa Katika Ujeremani) lilitaarifu hivi: “Theluthi moja yao [Mashahidi] waliuawa, ama walifishwa kwa amri ya kiserikali, ama kwa matendo mengine ya jeuri, njaa, ugonjwa au kazi ngumu ya utumwa. Ukali wa utiisho huu ulikuwa bila kitangulizi na ulikuwa tokeo la imani thabiti ambayo haingeweza kupatanishwa na siasa ya Usoshalisti wa Kitaifa.” Kweli kweli, inaweza kusemwa juu ya Jumuiya ya Wakristo, kutia na upadri wayo: “Katika marinda yako zimepatikana alama za damu ya nafsi za maskini wasio na hatia.”—Yeremia 2:34, NW.c
10. Wanaume vijana wa ule umati mkubwa wamepatwa na minyanyaso gani katika mabara mengi?
10 Tangu 1935 wanaume vijana waaminifu wa ule umati mkubwa wamehimili ukali wa minyanyaso katika mabara mengi. (Ufunuo 7:9) Hata wakati Vita ya Ulimwengu 2 ilipokuwa ikiisha katika Ulaya, katika mji mmoja tu vijana Mashahidi wa Yehova 14 walifishwa kwa kunyongwa kwa amri ya kiserikali. Uhalifu wao? Kukataa ‘kujifunza vita tena.’ (Isaya 2:4) Karibuni zaidi, wanaume vijana katika Mashariki na katika Afrika wamepigwa mpaka kifo au wakauawa na kikosi cha wapiga risasi kwa amri ya kiserikali juu ya suala ilo hilo. Wafia-imani hawa vijana, wategemezaji wastahilifu wa ndugu za Yesu wapakwa-mafuta, hakika watapata ufufuo kuingia ndani ya ile dunia mpya iliyoahidiwa.—2 Petro 3:13; Linga Zaburi 110:3; Mathayo 25:34-40; Luka 20:37, 38.
Joho Jeupe
11. Ni katika maana gani Wakristo wapakwa-mafuta waliofia imani hupokea “joho jeupe”?
11 Baada ya kuthibiti kwa maandishi imani ya washika-ukamilifu wa nyakati za kale, mtume Paulo alisema: “Na hata hivyo wote hawa, ijapokuwa ushuhuda ulitolewa kwao kupitia imani yao, hawakupata utimizo wa ahadi, kwa kuwa Mungu alitangulia kuona kitu fulani kilicho bora kwa ajili yetu sisi, ili kwamba wao wasifanywe kuwa wakamilifu mbali na sisi.” (Waebrania 11:39, 40, NW) Ni nini hicho “kitu fulani kilicho bora” ambacho Paulo na Wakristo wengine wapakwa-mafuta walitarajia? Yohana anakiona hapa katika njozi: “Na joho jeupe lilipewa kwa kila mmoja wao; na wao waliambiwa wapumzike kwa kitambo kidogo zaidi, mpaka hesabu ilipokuwa imejazwa pia ya watumwa wenzao na ndugu zao ambao walikuwa karibu kuuawa kama wao pia walivyokuwa.” (Ufunuo 6:11, NW) Kupokea kwao “joho jeupe” kunahusiana na kufufuliwa kwao wakawe viumbe wa roho wasioweza kufa. Hawalali tena wakiwa nafsi zilizochinjwa chini-chini ya madhabahu, bali wanainuliwa wakawe sehemu ya kile kikundi cha wazee 24 ambao huabudu mbele ya kiti cha ufalme cha Mungu. Huko, wao wenyewe wamepewa viti vya ufalme, kuonyesha kwamba wao wamekwisha ingia katika mapendeleo ya kifalme. Na “wamevalia mavazi ya nje meupe,” kuashiria kwamba wao wamekwisha hukumiwa kuwa waadilifu, wastahilio mahali pa heshima mbele za Yehova katika kitala cha kifalme. Hilo pia ni katika utimizo wa ahadi ya Yesu kwa Wakristo wapakwa-mafuta waaminifu katika kundi la Sardisi: “Yeye ambaye hushinda atapambwa hivyo kwa mavazi ya nje meupe.”—Ufunuo 3:5; 4:4; 1 Petro 1:4, NW.
12. Ni katika njia gani Wakristo waliofufuliwa ‘hupumzika kwa kitambo kidogo zaidi,’ na mpaka lini?
12 Ithibati yote huonyesha kwamba ufufuo huu wa kimbingu ulianza katika 1918, baada ya Yesu kuketishwa juu ya kiti cha ufalme katika 1914 na kutoka kwake aende akipanda farasi kuanza ushindi wake wa kifalme kwa kuzisafisha mbingu watoke Shetani na roho waovu wake. Hata hivyo, wapakwa-mafuta hao waliofufuliwa wanaambiwa kwamba lazima “wapumzike kwa kitambo kidogo zaidi, mpaka hesabu . . . pia ya watumwa wenzao” ijazwe. Wale wa jamii ya Yohana ambao wangali duniani lazima wathibitishe ukamilifu wao chini ya jaribu na mnyanyaso, na huenda baadhi ya hawa bado wakauawa. Hata hivyo, mwishowe, damu yote yenye uadilifu iliyomwagwa na Babuloni Mkubwa na hawara zake wa kisiasa italipiwa kisasi. Kwa wakati uliopo, pasipo shaka wale waliofufuliwa wana shughuli wakiwa na wajibu mwingi wa kimbingu. Wao wanapumzika, si kwa kustarehe katika raha ya kutotenda, bali katika njia ya kwamba wao wanangojea kwa subira siku ya kisasi cha Yehova. (Isaya 34:8; Warumi 12:19) Pumziko lao litakwisha wakati wao watashuhudia uharibifu wa dini bandia na, wakiwa ‘walioitwa na waliochaguliwa na waaminifu,’ wao wanaandamana na Bwana Yesu Kristo katika kutekeleza hukumu hapa duniani juu ya sehemu nyingine zote za mbegu mbovu ya Shetani.—Ufunuo 2:26, 27; 17:14; Warumi 16:20.
‘Wale Ambao Wamekufa Wainuka Kwanza’
13, 14. (a) Kulingana na mtume Paulo, ufufuo wa kimbingu huanza lini, na ni nani wanaofufuliwa? (b) Wale wapakwa-mafuta wanaoendelea kuishi kufikia siku ya Bwana wanafufuliwa lini waende mbinguni?
13 Ule muono-ndani unaotolewa kwa kufunguliwa kwa kifungo cha tano unakubaliana kabisa kabisa na maandiko mengine yanayohusiana na ufufuo wa kimbingu. Mathalani, mtume Paulo aliandika hivi: “Kwa maana hili ndilo ambalo sisi tunaambia nyinyi kwa neno la Yehova, kwamba sisi tulio hai ambao twaishi kufikia kuwapo kwa Bwana hatutatangulia kwa vyovyote wale ambao wamelala usingizi katika kifo; kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni akiwa na mwito wa kuamuru, na sauti ya malaika mkuu na tarumbeta ya Mungu, na wale ambao wamekufa katika muungano pamoja na Kristo watainuka kwanza. Baadaye sisi tulio hai ambao twaendelea kuishi, pamoja nao, tutadakwa mbali katika mawingu ili kumkuta Bwana katika hewa; na hivyo sisi tutakuwa na Bwana sikuzote.”—1 Wathesalonike 4:15-17, NW.
14 Ni hadithi yenye kusisimua kama nini ambayo mistari hii inasimulia! Wale wa ndugu za Yesu wapakwa-mafuta ambao huendelea kuishi kufikia kuwapo kwa Yesu, yaani, ambao wangali hai duniani wakati wa kuwapo kwake, wanatanguliwa kuingia ndani ya mbingu na wale ambao tayari wamekufa. Hao, ambao wamekufa katika muungano pamoja na Kristo, huinuka kwanza. Yesu hushuka, yaani, huelekeza uangalifu kwao, na kuwafufua kwenye uhai wa roho, akiwapa “joho jeupe.” Baadaye, wale ambao wangali hai wakiwa binadamu wanamaliza mwendo wao wa kidunia, wengi wao wakifa kijeuri mikononi mwa wapinzani. Hata hivyo, wao hawalali usingizi katika kifo kama watangulizi wao walivyofanya. Badala ya hivyo, wanapokufa, wao huinuliwa mara hiyo—“katika kufumba na kufumbua jicho”—wakidakwa mbali kwenda katika mbingu wakawe pamoja na Yesu na washiriki wenzi wa mwili wa Kristo. (1 Wakorintho 15:50-52, NW; linga Ufunuo 14:13.) Hivyo, kufufuliwa kwa Wakristo wapakwa-mafuta huanza upesi baada ya wale wapandaji-farasi wanne wa Apokalipsi kuanza upandaji wao.
15. (a) Kufunguliwa kwa kifungo cha tano kumeandaa habari njema gani? (b) Kupanda kwa Mshindi aliye juu ya farasi mweupe hufikia upeo gani?
15 Kule kufunguliwa kwa kifungo hiki cha tano cha hati-kunjo kumeandaa habari njema kuhusu washika ukamilifu wapakwa-mafuta ambao wameshinda, wakiwa waaminifu mpaka kifo. Lakini hakuandai habari njema kwa Shetani na mbegu yake. Upandaji wa yule Mshindi aliye juu ya farasi mweupe unaendelea bila kukinzwa na hufikia upeo katika wakati wa kutozwa hesabu kwa ulimwengu ambao “unalala katika nguvu za yule mwovu.” (1 Yohana 5:19, NW) Hili linadhihirishwa wakati Mwana-Kondoo anapofungua kifungo cha sita.
[Maelezo ya Chini]
a Utambulisho wa Babuloni Mkubwa huzungumzwa kirefu katika Sura ya 33.
b Linganisha New World Translation Reference Bible, ukurasa 1577, nyongeza 5C, “Nguzo ya Mateso.”
c Ithibati ya hatia-damu ya dini imetolewa kirefu katika Sura ya 36.
-
-
Matetemeko ya Dunia Katika Siku ya BwanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Sura ya 18
Matetemeko ya Dunia Katika Siku ya Bwana
1, 2. (a) Ikoje kuishi kupitia tetemeko la dunia kali? (b) Yohana anaeleza habari ya nini wakati kifungo cha sita kinapofunguliwa?
JE! WEWE umewahi kuishi kupitia tetemeko la dunia kali? Si ono zuri. Mtetemeko mkubwa huenda ukaanza kwa msukosuko wenye kugonjwesha na kelele yenye mtutumo. Myumboyumbo huenda ukazidi kuwa mbaya vipindi kwa vipindi na huku wewe ukikimbilia usalama—pengine chini ya dawati. Au huenda likaja likiwa mshtuo wa ghafula, wenye kuvunjavunja, ukifuatwa na kuvunjikavunjika kwa vikombe na sahani, samani na hata majengo. Uharibifu huenda ukawa wenye kuleta hasara sana, kukiwa na mishtuo ya baadaye ikileta uharibifu zaidi na kuongezea janga.
2 Ukiwa na hayo akilini, fikiria yale ambayo Yohana anaeleza wakati wa kufunguliwa kwa kifungo cha sita: “Na mimi nikaona wakati yeye alipofungua kifungo cha sita, na tetemeko la dunia kubwa likatukia.” (Ufunuo 6:12a, NW) Lazima hili lianguke katika muda wa wakati ule ule wa kufunguliwa kwa vile vifungo vingine. Ni wakati gani hasa katika siku ya Bwana tetemeko la dunia hili linatukia, nalo ni tetemo la namna gani?—Ufunuo 1:10.
3. (a) Ni matukio gani aliyotabiri Yesu katika unabii juu ya ishara ya kuwapo kwake? (b) Matetemeko ya dunia halisi yahusianaje na tetemeko la dunia la ufananisho la Ufunuo 6:12?
3 Matetemeko ya dunia ya kihalisi na ya kitamathali yametajwa katika Biblia mara kadhaa. Katika unabii mkubwa juu ya ishara ya kuwapo kwake katika mamlaka ya Ufalme, Yesu alitabiri “matetemeko ya dunia katika mahali pamoja baada ya pengine.” Hayo yangekuwa sehemu ya “mwanzo wa maumivu makali ya ghafula ya taabu.” Tangu 1914, idadi ya watu wa dunia ikiwa inaongezeka ghafula sana kuwa maelfu ya mamilioni, mitetemo hiyo imechangia kwa kutokeza sana taabu za nyakati zetu. (Mathayo 24:3, 7, 8, NW) Hata hivyo, hata ingawa yanatimiza unabii, matetemeko ya dunia hayo yamekuwa misiba asilia, yenye kuonekana. Hayo ni utangulizi wa lile tetemeko la dunia kubwa la ufananisho la Ufunuo 6:12. Kweli kweli, hili laja likiwa ndiyo tamati yenye kukumba ya mfululizo wa mitetemo yenye kutangulia inayotikisa mpaka misingi yenyewe mfumo wa mambo ya kibinadamu wa kidunia wa Shetani.a
Mitetemo Katika Jamii ya Kibinadamu
4. (a) Ni tangu lini watu wa Yehova walikuwa wamekuwa wakitaraji kwamba matukio yenye kuleta uharibifu yangeanza katika 1914? (b) 1914 ungetia alama ya mwisho wa kipindi gani cha wakati?
4 Kuanzia miaka ya katikati ya 1870 watu wa Yehova walikuwa wamekuwa wakitaraji kwamba matukio yenye kuleta uharibifu yangeanza katika 1914 nayo yangeonyesha mwisho wa Majira ya Mataifa. Hiki ndicho kipindi cha “nyakati saba” (miaka 2,520) kikianza na kupinduliwa kwa ufalme wa Kidaudi katika Yerusalemu katika 607 K.W.K. hadi kuketishwa kwa Yesu juu ya kiti cha ufalme katika Yerusalemu la kimbingu katika 1914 W.K.—Danieli 4:24, 25; Luka 21:24.b
5. (a) Ni tangazo gani alilofanya C. T. Russell katika Oktoba 2, 1914? (b) Ni mabadiliko makubwa gani ya kisiasa ambayo yametukia tangu 1914?
5 Hivyo, wakati C. T. Russell alipoonekana kwa ajili ya ibada ya asubuhi pamoja na jamaa ya Betheli ya Brooklyn, New York, asubuhi ya Oktoba 2, 1914, yeye alifanya tangazo hili lenye kusisimua: “Majira ya Mataifa yamekwisha; siku ya wafalme wayo imekwisha.” Kweli kweli, lile badiliko kubwa lililoanza katika 1914 lilikuwa na matokeo makubwa sana hivi kwamba falme nyingi zilizokuwa zimesimama kwa muda mrefu zilitoweka. Lile angusho la utawala wa zari katika pinduzi la Bolsheviki la 1917 liliongoza kwenye mkabiliano wa muda mrefu kati ya Umarksizimu na ukapitalisti (ubepari). Mitetemo ya badiliko la kisiasa yaendelea kusumbua jamii ya kibinadamu duniani pote. Leo, serikali nyingi zinashindwa kuendelea kwa muda unaozidi mwaka mmoja au miwili. Ukosefu wa imara katika ulimwengu wa kisiasa unatolewa kielezi na kisa cha Italia, ambayo ilikuwa na serikali mpya 47 katika muda wa miaka 42 tu kufuatia Vita ya Ulimwengu 2. Lakini mitetemo hiyo ni utangulizi tu wa badiliko kubwa la kiserikali lenye kufikia upeo mkuu. Tokeo litakuwa nini? Ufalme wa Mungu utachukua utawala kamili wa dunia.—Isaya 9:6, 7.
6. (a) H. G. Wells alielezaje habari ya muhula mpya wenye maana kubwa? (b) Mwanafalsafa mmoja na waziri wa serikali mmoja waliandika nini juu ya muhula wa tangu 1914?
6 Wanahistoria, wanafalsafa, na viongozi wa kisiasa wameelekeza kwenye mwaka 1914 kuwa mwanzo wa muhula mpya na wenye maana kubwa. Miaka 17 ya kuingia katika muhula huo, mwanahistoria H. G. Wells alitoa elezo hili: “Kwa mteremo nabii angetoa unabii wa vitu vizuri. Lakini wajibu wake ni kusimulia anachoona. Yeye anaona ulimwengu ambao ungali unadhibitiwa kiimara na askari-jeshi, wazalendo, wala-riba, na mabarakala wa kifedha; ulimwengu uliojikabidhi kwenye shuku na chuki, ukipoteza kwa haraka sana mauhuru ya faragha yaliyobaki, ukijongeza ki-upofu-upofu kuelekea mapambano makali ya kitabaka, na kutayarisha kwa ajili ya vita vipya.” Katika 1953 mwanafalsafa Bertrand Russell aliandika: “Tangu 1914, kila mtu anayejua maelekeo yaliyo katika ulimwengu amesumbuliwa sana na ule ambao umeonekana kuwa kama mwendo wenye tukio baya na uliokusudiwa kimbele kuelekea msiba unaozidi kuwa mkubwa. . . . Wao wanaona jamii ya kibinadamu, kama shujaa wa hadithi yenye misiba ya Kigiriki, akiendeshwa na miungu wenye kasirani na yeye siye bwana-mkubwa tena wa tukio baya.” Katika 1980 waziri wa serikali Harold Macmillan, akirudisha fikira nyuma kwenye mwanzo wenye amani wa karne ya 20, alisema: “Kila kitu kingezidi kuwa bora na bora. Huu ndio ulimwengu nilimozaliwa mimi. . . . Ghafula, asubuhi moja katika 1914 kitu kizima chote kilikuja kwenye mwisho.”
7-9. (a) Ni mabadiliko makubwa gani ambayo yametikisa jamii ya kibinadamu tangu 1914? (b) Mabadiliko makubwa katika jamii ya kibinadamu wakati wa kuwapo kwa Yesu hatimaye yangetia ndani hali gani miongoni mwa wanadamu?
7 Vita ya Ulimwengu 2 ilileta wimbi jingine la mabadiliko makubwa. Na vita vidogo zaidi pamoja na ugaidi wa kimataifa vinaendelea kutikisa dunia. Lile tisho la magaidi au mataifa yanayotumia silaha za maangamizi makubwa linafanya watu wengi wawe na wasiwasi.
8 Ingawa hivyo, mambo mengine licha ya vita yametikisa jamii ya kibinadamu mpaka kwenye misingi yayo tangu 1914. Mojapo mabadiliko makubwa ambalo lilikuwa lenye kuumiza zaidi sana lilianzishwa na anguko la soko la rasilimali la U.S. la Oktoba 29, 1929. Hilo lilileta Ule Mshuko Mkubwa wa Thamani ya Pesa, ambao uliathiri nchi zote za ukapitalisti. Mshuko huo ulifikia upeo wa chini zaidi kati ya 1932 na 1934, lakini sisi tungali tunahisi matokeo yao. Tangu 1929 ulimwengu mgonjwa kiuchumi umetiwa-tiwa viraka kwa kutumia mipango-badala. Serikali zinajitia katika madeni ya kifedha. Ile shida kubwa ya mafuta ya 1973 na mshuko-ghafula wa 1987 wa soko la rasilimali viliongezea mitikiso ya milki ya kifedha. Kwa wakati uliopo, mamilioni ya watu hununua vitu kwa mkopo. Idadi zisizohesabika huwa majeruhi ya madanganyo ya kifedha, mipango ya kipiramidi, na hila za michezo ya bahati-nasibu na kamari, mingi yayo ikiwa inadhaminiwa na serikali ambazo zapaswa kuwa zikiwapa himaya watu. Hata waevanjeli wa televisheni wa Jumuiya ya Wakristo hunyoosha mikono yao wapate hisa yao ya mamilioni ya dola!—Linga Yeremia 5:26-31.
9 Mapema zaidi, shida za kiuchumi zilikuwa zimefungulia njia Mussolini na Hitla wanyakue mamlaka. Babuloni Mkubwa hakupoteza wakati wowote akitafuta kupendwa nao, na Vatikani iliingia katika mapatano na Italia katika 1929 na Ujeremani katika 1933. (Ufunuo 17:5) Zile siku zenye huzuni zilizofuata hakika zilikuwa sehemu ya utimizo wa unabii wa Yesu kuhusu kuwapo kwake, ambao ungetia ndani “huzuni kuu ya mataifa, yasijue njia ya kutokea . . . huku watu wakizirai kwa woga na taraja la vitu vinavyokuja juu ya dunia inayokaliwa.” (Luka 21:7-9, 25-31, NW)c Ndiyo, yale matetemeko yaliyoanza kutikisa jamii ya kibinadamu katika 1914 yameendelea, kukiwa na mishtuo ya baadaye yenye nguvu.
Yehova Atikisa
10. (a) Ni kwa nini kuna mitetemo mingi sana katika mambo ya kibinadamu? (b) Yehova anafanya nini, kwa kutayarishia nini?
10 Mitetemo hiyo katika mambo ya kibinadamu ni matokeo ya kutoweza kwa binadamu kuelekeza hatua zake mwenyewe. (Yeremia 10:23) Zaidi ya hilo, Shetani, nyoka wa zamani, “ambaye anaongoza vibaya dunia nzima yote inayokaliwa,” analeta ole katika jaribio lake la mwisho la kukengeua aina ya binadamu kutoka ibada ya Yehova. Tekinolojia ya ki-siku-hizi imeifanya dunia iwe ndogo kama ujirani mmoja tu, ambapo chuki za kitaifa na za kijamii zinatikisa jamii ya kibinadamu mpaka misingi yayo, nao ule unaoitwa eti Umoja wa Mataifa, hauwezi kupata ponyo lenye kuleta matokeo. Kama isivyopata kuwa hapo zamani, mwanadamu anatawala mwanadamu kwa umizo lake. (Ufunuo 12:9, 12; Mhubiri 8:9, NW) Hata hivyo, Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu, Mfanyiza mbingu na dunia, amekuwa akifanya aina yake mwenyewe ya utikisaji kwa karibu miaka 90, katika kujitayarishia kutatua matatizo ya dunia mara moja na kwa wakati wote. Jinsi gani hivyo?
11. (a) Ni mtikiso gani unaoelezwa katika Hagai 2:6, 7? (b) Unabii wa Hagai unatimizwaje?
11 Kwenye Hagai 2:6, 7, NW, tunasoma hivi: “Kwa kuwa hivi ndivyo Yehova wa majeshi amesema, ‘Bado mara moja—ni kitambo kidogo—na mimi ninatikisa mbingu na dunia na bahari na nchi kavu. Na mimi nitatikisa mataifa yote, na vitu vyenye kutamanika vya mataifa yote lazima vije ndani; na mimi nitajaza nyumba hii utukufu,’ Yehova wa majeshi amesema.” Tangu 1919 hasa, Yehova amefanya mashahidi wake wapige mbiu ya hukumu zake miongoni mwa elementi zote za jamii ya kibinadamu duniani. Mfumo wa ulimwengu wa Shetani umetahadharishwa kwa onyo la pote katika tufe.d Kadiri onyo hilo linavyopata nguvu, binadamu wenye kumhofu Mungu, vile “vitu vyenye kutamanika,” wamechochewa wajitenge na mataifa. Si kwamba wanatikiswa na kule kutetemeshwa katika tengenezo la Shetani. Lakini wanapotambua hali, wao wanafanya uamuzi wao wenyewe washiriki pamoja na jamii ya Yohana yenye kupakwa mafuta katika kuijaza utukufu nyumba ya Yehova ya ibada. Hilo linatimizwaje? Kwa kazi ya bidii ya kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu uliosimamishwa. (Mathayo 24:14) Ufalme huu, ambao washiriki wao ni Yesu na wafuasi wake wapakwa-mafuta, utaendelea kusimama daima kwa utukufu wa Yehova ukiwa “ufalme usioweza kutikiswa.”—Waebrania 12:26-29, NW.
12. Ikiwa wewe umeanza kuitikia kazi ya kuhubiri iliyotabiriwa kwenye Mathayo 24:14, inakupasa wewe ufanye nini kabla halijatokea lile tetemeko la dunia kubwa la Ufunuo 6:12?
12 Je! wewe ni mmoja ambaye ameanza kuitikia kuhubiri huko? Je! pengine wewe ni mmoja wa wale mamilioni ambao katika miaka ya karibuni wamehudhuria Ukumbusho wa kifo cha Yesu? Ikiwa ndivyo, zidi kufanya maendeleo katika funzo lako la ukweli wa Biblia. (2 Timotheo 2:15; 3:16, 17) Acha kabisa ule mtindo wa maisha wenye ufisadi wa jamii ya kidunia ya Shetani iliyohukumiwa maangamizi! Njoo na kuingia mpaka ndani ya jamii ya ulimwengu mpya ya Kikristo na ushiriki kikamili katika utendaji wayo kabla ya lile “tetemeko la dunia” la mwisho lenye kuleta uharibifu halijavunja vipande vipande ulimwengu wote wa Shetani. Lakini ni nini hilo tetemeko la dunia kubwa? Acheni tuone sasa.
Lile Tetemeko la Dunia Kubwa!
13. Ni kwa njia gani hilo tetemeko la dunia kubwa ni ono jipya kabisa kwa binadamu?
13 Ndiyo, hizi siku za mwisho zenye hatari zimekuwa wakati wa matetemeko ya dunia—halisi na ya kitamathali. (2 Timotheo 3:1) Lakini hapana mojapo matetemeko haya ambalo ndilo ule mtikiso mkubwa wa mwisho ambao Yohana anaona wakati wa kufunguliwa kwa kifungo cha sita. Wakati wa mitetemo ya utangulizi umekwisha. Linakuja sasa tetemeko la dunia kubwa ambalo ni jipya kabisa kuonwa na aina ya binadamu. Ni tetemeko kubwa sana hivi kwamba mitetemo na misukosuko linayosababisha haiwezi kupimwa kwa kipima-tetemeko cha Richter au kwa kipimo kinginecho cha kibinadamu. Hili si mshtuo wa mahali tu bali mtikiso wenye msiba mkubwa ambao unakumba “dunia” nzima yote, yaani, jamii yote ya kibinadamu iliyo fasiki.
14. (a) Ni unabii gani ambao hutabiri tetemeko la dunia kubwa na matokeo yalo? (b) Ni lazima unabii wa Yoeli na Ufunuo 6:12, 13 urejezee nini?
14 Wengine wa manabii wa Yehova walitabiri tetemeko la dunia kama hilo na matokeo yalo yenye kuleta uharibifu. Mathalani, yapata 820 K.W.K., Yoeli alisema juu ya “kuja kwa siku kuu na yenye kuvuvia hofu ya Yehova,” akitaarifu kwamba ndipo “jua lenyewe litageuzwa kuwa giza, na mwezi kuwa damu.” Baadaye, yeye anaongezea maneno haya: “Halaiki za watu, halaiki za watu zimo katika bonde la uamuzi, kwa kuwa siku ya Yehova i karibu katika uwanda-bonde wa uamuzi. Jua na mwezi vyenyewe kwa hakika vitakuwa vyenye giza, na nyota zenyewe hakika zitaondoa uangavu wazo. Na kutoka Sayuni Yehova mwenyewe atanguruma, na kutoka Yerusalemu yeye atatoa nje sauti yake. Na mbingu na dunia kwa hakika zitatikiswa; lakini Yehova atakuwa kimbilio kwa ajili ya watu wake, na ngome kwa ajili ya wana wa Israeli.” (Yoeli 2:31; 3:14-16, NW) Kutikiswa huku kungetumika kuhusu tu kutekelezwa kwa hukumu ya Yehova wakati wa dhiki kubwa. (Mathayo 24:21) Kwa hiyo lile simulizi mlingano kwenye Ufunuo 6:12, 13 kimantiki lingetumika jinsi iyo hiyo.—Ona pia Yeremia 10:10; Sefania 1:14, 15.
15. Ni mtikiso gani wenye nguvu aliotabiri nabii Habakuki?
15 Yapata miaka 200 baada ya Yoeli, nabii Habakuki alisema na Mungu katika sala hivi: “O Yehova mimi nimesikia ripoti juu yako wewe. Mimi nimeogopa, O Yehova, utendaji wako. Katikati ya miaka O ulete kwenye uhai! Katikati ya miaka wewe na uufanye ujulikane. Wakati wa msukosuko, kuonyesha rehema wewe na ukumbuke.” Huo “msukosuko” ungekuwa nini? Habakuki anaendelea kutoa elezo dhahiri sana la dhiki kubwa, akisema kwa habari ya Yehova: “Yeye alisimama tuli, ili apate kutikisa dunia. Yeye aliona, na kisha akasababisha mataifa kuruka. . . . Pamoja na shutumu wewe ulienda ukipiga miguu kupitia dunia. Katika kasirani wewe ulienda ukiyapura mataifa. Hata hivyo, kwa habari yangu mimi, mimi nitachachawa katika Yehova mwenyewe; mimi nitakuwa mwenye shangwe katika Mungu wa wokovu wangu.” (Habakuki 3:1, 2, 6, 12, 18, NW) Lo! ni mtikiso wenye nguvu kama nini ambao Yehova atasababisha katika dunia yote wakati yeye atakapoyapura mataifa!
16. (a) Ni nini analotabiri nabii Ezekieli kwa ajili ya wakati ambao Shetani anafanya shambulio lake la mwisho juu ya watu wa Mungu? (b) Ni nini linalotokana na tetemeko la dunia kubwa la Ufunuo 6:12?
16 Ezekieli alitabiri kwamba wakati Gogu wa Magogu (Shetani aliyetwezwa) anapofanya shambulio la mwisho juu ya watu wa Mungu, Yehova atasababisha “tetemeko kubwa” litukie “katika udongo wa Israeli.” (Ezekieli 38:18, 19, NW) Ingawa huenda matetemeko ya dunia halisi yakahusika, inatupasa sisi kukumbuka kwamba Ufunuo umetolewa kwa ishara. Unabii huu pamoja na unabii mwingine uliotajwa ni wa ufananisho kabisa. Kwa sababu hiyo, kufunguliwa kwa kifungo cha sita inaelekea kunafunua ule upeo wa mitikiso yote ya huu mfumo wa mambo wa kidunia—lile tetemeko la dunia kubwa ambalo katika hilo binadamu wote wanaopinga enzi kuu ya Yehova Mungu wanaharibiwa.
Wakati wa Giza
17. Hilo tetemeko la dunia kubwa linaathirije jua, mwezi, na nyota?
17 Kama vile Yohana aendeleavyo kuonyesha, tetemeko la dunia kubwa linaandamana na matukio yenye kuogofya ambayo yanahusu hata mbingu. Yeye anasema: “Nalo jua likawa jeusi kama gunia la nywele, na mwezi mzima wote ukawa kama damu, na nyota zote za mbingu zikaanguka kwenye dunia, kama vile wakati mtini unapotikiswa na upepo mkali hurusha tini zao zisizoiva.” (Ufunuo 6:12b, 13, NW) Ni kituko chenye kugutusha kama nini! Je! wewe unaweza kuwazia giza lenye kuogopesha ambalo lingetokea kama unabii huo ungetimizwa kihalisi? Hakungekuwa tena na nuru ya jua yenye joto na yenye kufariji mchana! Hakungekuwa tena na nuru ya mwezi ya kirafiki na yenye rangi ya fedha usiku! Na zile miriadi za nyota hazingemetameta dhidi ya kisetiri-nyuma cha kimahameli cha anga. Badala ya hivyo, kungekuwa na weusi ti, wenye baridi, usiokoma.—Linga Mathayo 24:29.
18. Ni katika njia gani ‘mbingu zilipata kuwa zenye giza’ kwa ajili ya Yerusalemu katika 607 K.W.K.?
18 Katika maana ya kiroho, giza kama hilo lilitolewa unabii kwa Israeli wa kale. Yeremia alionya hivi: “Ukiwa mtupu ndivyo bara kwa ujumla litakuja kuwa, na je! mimi sitatimiza uharibifu kabisa? Kwa sababu hiyo bara litaomboleza, na mbingu zilizo juu zitakuwa giza.” (Yeremia 4:27, 28, NW) Katika 607 K.W.K. wakati unabii huo ulipotimizwa, mambo yalikuwa yenye giza kweli kweli kwa watu wa Yehova. Yerusalemu, jiji lao kuu, lilianguka kwa Wababuloni. Hekalu lao liliharibiwa, na bara lao likaachwa ukiwa. Kwa wao, hakukuwa na nuru yenye kufariji kutoka mbingu. Badala, ilikuwa kama vile Yeremia alivyoambia Yehova kwa kuomboleza: “Wewe umeua; wewe hukuonyesha huruma. Umefunga ufikio kwako wewe kwa tungamo la wingu, kwamba sala isipate kupenya.” (Maombolezo 3:43, 44, NW) Kwa Yerusalemu, giza hilo la kimbingu lilimaanisha kifo na uharibifu.
19. (a) Isaya, nabii wa Mungu anaelezaje habari ya giza katika mbingu juu ya Babuloni wa kale? (b) Ni wakati gani na jinsi gani unabii wa Isaya ulitimizwa?
19 Baadaye, giza linalofanana na hilo katika mbingu liliashiria uharibifu kwa Babuloni wa kale. Kwa habari ya hilo, nabii wa Mungu alivuviwa aandike hivi: “Tazama! Siku ya Yehova yenyewe inakuja, katili kwa kiruu na kasirani yenye kuwaka pia, ili kufanya bara liwe kitu cha mshangao, na kwamba iweze kutowesha wafanya dhambi wa bara kutoka kwayo. Kwa kuwa nyota zenyewe za zile mbingu na makundi ya Kesili yazo hazitameremesha nuru yazo; kwa hakika jua litakuwa giza wakati wa kutokea kwalo, na mwezi wenyewe hautafanya nuru yao kuangaza. Na mimi kwa hakika nitaonyesha wazi ubaya walo lenyewe juu ya bara lenye kuzaa, na kosa lao wenyewe juu ya waovu wenyewe.” (Isaya 13:9-11, NW) Unabii huu ulitimizwa katika 539 K.W.K. wakati Babuloni ilipoanguka kwa Wamedi na Waajemi. Unaeleza vizuri ule weusi ti, ule utotumaini, ule ukosefu wa nuru ya faraja kwa Babuloni ilipokuwa ikianguka milele kutoka cheo chayo cha kuwa serikali kuu ya ulimwengu.
20. Ni tokeo gani lenye kuhofisha linalongojea huu mfumo wa mambo wakati tetemeko la dunia kubwa linapopiga?
20 Kwa njia iyo hiyo, wakati tetemeko la dunia kubwa linapopiga, mfumo wote huu wa ulimwengu utagharikishwa katika tamausho la giza tititi. Vile vimeti viangavu, vyenye kung’aa vya mfumo wa kidunia wa Shetani havitatoa miale ya tumaini. Tayari leo, viongozi wa kisiasa wa dunia, hasa katika Jumuiya ya Wakristo, wana sifa mbaya sana kwa sababu ya ufisadi wao, kusema uwongo na mtindo wao wa maisha wa utovu wa adili. (Isaya 28:14-19) Hawawezi kuitibariwa tena. Nuru yao yenye kusinzia itapatwa na giza kabisa Yehova atekelezapo hukumu. Uvutano wao ulio kama mwezi juu ya mambo ya dunia utafunuliwa kuwa umetiwa damu, wenye kuleta kifo. Nyota zao mashuhuri za kilimwengu zitazimwa kama vimondo viangukavyo ghafula na zitatawanywa kama tini zisizoiva katika upepo-dhoruba wenye kuvuma. Tufe letu lote litatetemeka chini ya “dhiki kubwa kama ambayo haijapata kutukia tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka sasa, la, wala haitatukia tena.” (Mathayo 24:21, NW) Lo! ni tazamio lenye kujaa hofu kama nini!
“Mbingu” Yaondoka
21. Katika njozi yake, Yohana anaona nini kuhusu “mbingu” na “kila mlima na kila kisiwa”?
21 Njozi ya Yohana inaendelea: “Na mbingu ikaondoka kama hati-kunjo inayokunjwa, na kila mlima na kila kisiwa viliondolewa mahali pavyo.” (Ufunuo 6:14, NW) Kwa wazi hizi si mbingu halisi au milima na visiwa halisi. Lakini hizo zinafananisha nini?
22. Katika Edomu ni aina gani za “mbingu” ‘zilizokunjwa, kama hati-kunjo’?
22 Kwa habari ya “mbingu,” sisi tunasaidiwa katika uelewevu wetu na unabii unaofanana na huo unaosema juu ya hasira kali ya Yehova dhidi ya mataifa: “Na wale wote wa lile jeshi la zile mbingu lazima waozee mbali. Na zile mbingu lazima zikunjwe kama hati-kunjo.” (Isaya 34:4, NW) Hasa Edomu lazima akione. Jinsi gani? Alishambuliwa na Wababuloni muda mfupi baada ya uharibifu wa Yerusalemu katika 607 K.W.K. Wakati huo, hakuna matukio yenye kutokeza yaliyorekodiwa kuwa yakitukia katika mbingu halisi. Lakini yalikuwako matukio yenye kuleta uharibifu katika “mbingu” za Edomu.e Mamlaka zake za serikali za kibinadamu zilishushwa kutoka cheo chazo kilichoinuliwa, mfano wa mbingu. (Isaya 34:5) ‘Zilikunjwa’ zikawa kana kwamba zimewekwa kando, kama hati-kunjo kuukuu ambayo haina matumizi yoyote tena kwa yeyote.
23. Ni “mbingu” gani ‘itakayoondoka kama hati-kunjo,’ nayo maneno ya Petro yanathibitishaje uelewevu huu?
23 Hivyo, “mbingu” inayopaswa ‘kuondoka kama hati-kunjo’ hurejeza kwenye serikali zinazopinga Mungu ambazo hutawala juu ya dunia hii. Hizo zitaondolewa kwa ukomo na yule Mpandaji-farasi mweupe. (Ufunuo 19:11-16, 19-21) Hilo linathibitishwa na aliyosema mtume Petro wakati alipotazama mbele kwenye matukio yaliyoashiriwa na kule kufunguliwa kwa kifungo cha sita: “Mbingu na dunia zilizopo sasa zimewekwa akiba kwa moto na zimehifadhiwa kwa ajili ya siku ya hukumu na ya uharibifu wa watu wasiohofu Mungu.” (2 Petro 3:7, NW) Lakini namna gani usemi huu, “kila mlima na kila kisiwa viliondolewa mahali pavyo”?
24. (a) Katika unabii wa Biblia, ni wakati gani inaposemwa kwamba milima na visiwa vinatikiswa au kuondolewa uimara? (b) ‘Milima ilitikisikaje’ wakati Ninawi ulipoanguka?
24 Katika unabii wa Biblia, milima na visiwa vinasemwa kuwa vinatikiswa au kuondolewa uimara wakati wa mabadiliko makubwa ya kisiasa. Mathalani, wakati wa kutabiri hukumu za Yehova dhidi ya Ninawi, nabii Nahumu aliandika: “Milima yenyewe imetikisika kwa ajili ya yeye, na vilima halisi vikajikuta vyenyewe vikiyeyuka. Nayo dunia itapinduliwa kwa sababu ya uso wake.” (Nahumu 1:5, NW) Hakuna maandishi yanayoonyesha kuvunjika kokote kwa milima halisi wakati Ninawi ulipoanguka kikweli katika 632 K.W.K. Lakini serikali kubwa ya ulimwengu ambayo hapo kwanza ilionekana kuwa kama mlima katika imara yayo ilianguka ghafula.—Linga Yeremia 4:24.
25. Kwenye ule mwisho unaokuja wa huu mfumo wa mambo, “kila mlima na kila kisiwa” vitaondolewaje mahali pavyo?
25 Kwa hiyo, kimantiki “kila mlima na kila kisiwa” kama inavyorejezewa mwanzoni mwa kufunguliwa kwa kifungo cha sita vingekuwa serikali za kisiasa na matengenezo yanayozitegemea ya ulimwengu huu ambazo zimeonekana kuwa imara sana kwa wengi wa aina ya binadamu. Zitatikiswa zitoke mahali pazo, kwa fadhaa na hofu ya wale ambao hapo kwanza waliziitibari. Kama vile unabii huo uendeleavyo kusimulia, hakutakuwa na shaka lolote kwamba ile siku kubwa ya hasira-kisasi ya Yehova na Mwana wake—lile tetemeko la mwisho kabisa ambalo linaondoa matengenezo yote ya Shetani—imekuja ikiwa na kisasi!
“Angukeni Juu ya Sisi na Kuficha Sisi”
26. Binadamu wanaopinga enzi kuu ya Mungu watatendaje katika hofu yao, na ni maneno gani ya hofu kuu watakayotamka?
26 Maneno ya Yohana yanaendelea: “Na wafalme wa dunia na wenye vyeo vya juu na makamanda wa kivita na matajiri na makamambe na kila mtumwa na kila mtu huru wakajificha wenyewe katika mapango na katika yale matungamo-miamba ya milima. Na wao walifuliza kusema kwa milima na kwa matungamo-miamba: ‘Angukeni juu ya sisi na kuficha sisi kutoka uso wa yule Mmoja aliyeketi juu ya kiti cha ufalme na kutoka hasira-kisasi ya Mwana-Kondoo, kwa sababu siku kubwa ya hasira-kisasi yao imekuja, na ni nani anaweza kusimama?’”—Ufunuo 6:15-17, NW.
27. Ni vilio gani vilivyotamkwa na Waisraeli wasio waaminifu wa Samaria, na maneno hayo yalitimizwaje?
27 Wakati Hosea alipokuwa akitamka hukumu ya Yehova juu ya Samaria, jiji kuu la ufalme wa kaskazini wa Israeli, yeye alisema hivi: “Sehemu za juu za Beth-aveni, dhambi ya Israeli, kwa kweli zitatoweshwa kabisa. Miiba na mibigili yenyewe itapanda juu ya madhabahu yao. Na kwa hakika watu watasema kwa milima yenyewe, ‘Funikeni sisi!’ na kwa vilima, ‘Angukeni juu ya sisi!’” (Hosea 10:8, NW) Maneno haya yalitimizwaje? Basi, wakati Samaria lilipoanguka kwa Waashuri wakatili katika 740 K.W.K. hapakuwa na mahali pa Waisraeli kukimbilia. Maneno ya Hosea huonyesha hisia ya utotumaini, hofu tupu, na kuachwa walikohisi watu hao walioshindwa. Wala vilima halisi wala matengenezo ya Samaria yaliyokuwa kama milima hayangeweza kuwapa himaya, hata ingawa yalikuwa yameonekana kuwa ya kudumu sana wakati uliopita.
28. (a) Ni onyo gani ambalo Yesu aliwapa wanawake wa Yerusalemu? (b) Onyo la Yesu lilitimizwaje?
28 Hali moja na hiyo, Yesu alipokuwa akipelekwa na askari-jeshi Waroma kwenye kifo, yeye alihutubia wanawake wa Yerusalemu na kusema: “Siku zinakuja ambazo katika hizo watu watasema, ‘Wenye furaha ni wale wanawake walio tasa, na matumbo-uzazi ambayo hayakuzaa na matiti ambayo hayakunyonyesha!’ Ndipo wataanza kusema kwa milima, ‘Angukeni juu ya sisi!’ na kwa vilima, ‘Funikeni sisi!’” (Luka 23:29, 30, NW) Ule uharibifu wa Yerusalemu ulioletwa na Waroma katika 70 W.K. umethibitishwa vizuri kimaandishi, na ni wazi kwamba maneno ya Yesu yana maana inayofanana na ile ya maneno ya Hosea. Wakati ule hapakuwa na mahali pa kujificha kwa Wayahudi ambao walikuwa wamebaki katika Yudea. Kokote walikojaribu kujificha katika Yerusalemu, au hata wakati walipokimbilia ngome ya Masada juu ya mlima, wao hawakuweza kuepuka wonyesho wenye jeuri wa hukumu ya Yehova.
29. (a) Wakati siku ya Yehova ya hasira-kisasi inapokuja, ni nini kitakachopata wale ambao wamejitoa kuunga mkono huu mfumo wa mambo? (b) Ni unabii gani wa Yesu utakaotimizwa wakati Yehova anapoonyesha hasira-kisasi Yake?
29 Sasa, kule kufunguliwa kwa kifungo cha sita kumeonyesha kwamba kitu fulani kama hicho kitatukia wakati wa siku inayokuja ya hasira-kisasi ya Yehova. Wakati wa kutikiswa kwa mwisho kabisa kwa huu mfumo wa mambo wa kidunia, wale waliojitoa kuuunga mkono watatafuta sana mahali pa kujificha, lakini hawatapata hata pamoja. Dini bandia, Babuloni Mkubwa, tayari imeshindwa vya kusikitisha sana kuwasaidia. Wala mapango katika milima halisi wala matengenezo ya kisiasa na ya kibiashara yaliyo mfano wa milima hayataandaa usalama wa kifedha au msaada mwingine wa aina yoyote. Hakuna kitu kitakachowakinga wasipatwe na hasira-kisasi ya Yehova. Hofu yao imeelezwa vizuri na Yesu: “Ndipo ishara ya Mwana wa binadamu itaonekana katika mbingu, na ndipo makabila yote ya dunia yatajipigapiga yenyewe kwa ombolezo, na yataona Mwana wa binadamu akija juu ya mawingu ya mbingu akiwa na nguvu na utukufu mkubwa.”—Mathayo 24:30, NW.
30. (a) Ni nini kinachodokezwa na swali hili: “Ni nani anaweza kusimama?” (b) Je! wowote wataweza kusimama wakati wa hukumu ya Yehova?
30 Ndiyo, wale ambao wamekataa kutambua mamlaka ya yule Mpandaji-farasi mweupe mwenye ushindi watalazimika kukubali kosa lao. Wanadamu ambao kwa kupenda wamekuwa mbegu ya yule nyoka wataelekeana na uharibifu wakati ulimwengu wa Shetani unapopitilia mbali. (Mwanzo 3:15; 1 Yohana 2:17) Hali ya ulimwengu kwenye wakati huo itakuwa ya aina ya kwamba, ni kana kwamba wengi watakuwa wakiuliza: “Ni nani anaweza kusimama?” Yaonekana kama watadhani hakuna yeyote kwa vyovyote ambaye anaweza kusimama akiwa anakubalika mbele za Mungu katika siku hiyo ya hukumu yake. Lakini watakuwa wenye kukosea, kama vile kitabu cha Ufunuo kinavyoendelea kuonyesha.
[Maelezo ya Chini]
a Matetemeko ya dunia halisi mara nyingi hutanguliwa na misukosuko yenye mtutumo ambayo husababisha mbwa kubweka au kutenda bila kutulia na hutaharakisha wanyama wengine na samaki, ingawa huenda wanadamu wasishuku mpaka tetemeko lenyewe linapopiga.—Ona Amkeni (Kiingereza), Julai 8, 1982, ukurasa 14.
b Ili kupata maelezo zaidi, ona kurasa 22, 24.
c Kwa zaidi ya miaka 35, kutoka 1895 mpaka 1931, maneno ya Luka 21:25, 28, 31 yalinukuliwa yakawekwa kwenye jalada la gazeti Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) dhidi ya kisetiri-nyuma cha mnara wa taa ukimulikia anga zenye dhoruba juu ya bahari yenye mchafuko.
d Mathalani, katika kampeni ya pekee katika 1931, Mashahidi wa Yehova binafsi walipelekea viongozi wa kidini, wanasiasa, na wafanya-biashara kotekote duniani, maelfu mengi ya kijitabu The Kingdom, the Hope of the World.
e Katika tumizi kama hilo la neno “mbingu,” unabii wa “mbingu mpya” katika Isaya 65:17, 18 ulikuwa na utimizo wao wa kwanza katika ule mfumo mpya wa kiserikali, uliohusu Gavana Zerubabeli na Kuhani Mkuu Yeshua, uliosimamishwa katika Bara la Ahadi baada ya Waisraeli kurudi kutoka uhamisho wa Kibabuloni.—2 Nyakati 36:23; Ezra 5:1, 2; Isaya 44:28.
-
-
Matetemeko ya Dunia Katika Siku ya BwanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 105]
1914 Ulitangulia Kuonwa
“Ilikuwa katika K.K. 606, kwamba ufalme wa Mungu ulikwisha, taji liliondolewa, na dunia yote ikapewa Wasio Wayahudi. Miaka 2520 kutoka K.K. 606, itakwisha katika M.B. 1914.”f—The Three Worlds, kilichotangazwa 1877, ukurasa 83.
“Ithibati ya Biblia ni wazi na thabiti kwamba ‘Majira ya Mataifa’ ni kipindi cha miaka 2520, kutoka K.K. 606 kufika na kutia ndani M.B. 1914”—Studies in the Scriptures, Buku 2, kilichoandikwa na C. T. Russell na kikatangazwa 1889, ukurasa 79.
Charles Taze Russell na Wanafunzi wa Biblia wenzake waling’amua miongo kadhaa mapema zaidi kwamba 1914 ungeonyesha mwisho wa Majira ya Mataifa, au nyakati zilizowekwa za mataifa. (Luka 21:24) Ingawa katika siku hizo za mapema wao hawakuelewa kikamili hii ingemaanisha nini, wao walisadikishwa kwamba 1914 ingekuwa tarehe ya mabadiliko katika historia ya ulimwengu, nao walikuwa sahihi. Angalia dondoo hili linalofuata la nyusipepa:
“Ule mfyatuko wa vita wenye kuogopesha katika Ulaya umetimiza unabii usio wa kawaida. Kwa robo ya karne iliyopita, kupitia wahubiri na kupitia magazeti, wale ‘Wanafunzi wa Biblia,’ wanaojulikana vizuri zaidi kuwa ‘Wanamapambazuko wa Mileani,’ wamekuwa wakitangazia ulimwengu kwamba ile Siku ya Hasira-Kisasi iliyotolewa unabii na Biblia ingepambazuka katika 1914. ‘Lindeni kwa ajili ya 1914!’ kimekuwa ndicho kilio cha mamia ya waevanjeli wasafirio.”—The World, nyusipepa moja ya New York, Agosti 30, 1914.
[Maelezo ya Chini]
f Kwa uongozi wa kimungu, hao Wanafunzi wa Biblia hawakuwa wameng’amua kwamba hakukuwa na mwaka sufuri katikati ya “K.K.” na “M.B.” Baadaye, wakati utafiti ulipofanya ihitajiwe kabisa kurekebisha K.K. 606 kuwa 607 K.W.K., ule mwaka sufuri uliondolewa pia, hivi kwamba ule utabiri ukawa sahihi kwenye “M.B. 1914.”—Ona “The Truth Shall Make You Free,” kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova mwaka wa 1943, ukurasa 239.
[Picha katika ukurasa wa 106]
1914—Kigeukio cha Historia
Kile Kitabu Politikens Verdenshistorie—Historiens Magt og Mening kilichotangazwa 1987 katika Copenhagen, kinatoa oneleo hili kwenye ukurasa 40:
“Imani ya karne ya 19 katika mwendeleo ilipata pigo layo lenye kufisha katika 1914. Ule mwaka uliotangulia mfyatuko wa vita, mwanahistoria na mwanasiasa Mdanishi Peter Munch aliandika akiwa na matumaini mazuri hivi: ‘Ithibati yote iko dhidi ya uwezekano wa kutokea kwa vita kati ya serikali kubwa-kubwa za Ulaya. “Ile hatari ya vita” pia itatoweka katika wakati ujao, kama vile imefanya wakati kwa wakati tangu 1871.’
“Kwa kutofautisha, sisi tunasoma katika kumbukumbu zake za baadaye: ‘Ule mfyatuko wa vita katika 1914 ndio kigeukio kikubwa cha historia ya binadamu. Kutoka katika wakati maalumu ulio mwangavu wa maendeleo, ambao katika huo mambo yangefuatiliwa kwa usalama wenye kiasi, sisi tuliingia kizazi cha msiba, hofu kuu, na chuki, kukiwa na utosalama kila mahali. Hakuna yeyote angeweza kusema, na hata leo hakuna anayeweza kusema, kama giza lililoanguka juu yetu wakati huo litamaanisha uharibifu wenye kudumu wa muundo mzima wote wa kitamaduni ambao binadamu amejiumbia mwenyewe kwa mileani zilizopita.’”
-