Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 5
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika 1 Wafalme

      • Mufalme Hiramu anatoa vifaa vya ujenzi (1-12)

      • Watu wa Sulemani wenye waliandikishwa kwa ajili ya kazi ya kulazimishwa (13-18)

1 Wafalme 5:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “alimupenda Daudi sikuzote.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 27:3
  • +2 Sa. 5:11

1 Wafalme 5:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 2:3

1 Wafalme 5:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 7:5; 1Nya 22:7, 8

1 Wafalme 5:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 4:24, 25
  • +Mez. 16:7

1 Wafalme 5:5

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 7:12, 13; 1Nya 22:9, 10; 2Nya 2:4

1 Wafalme 5:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 6:9, 20
  • +2Nya 2:8

1 Wafalme 5:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 2:11, 12

1 Wafalme 5:8

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 6:5; 1 Fal. 6:15; 2Nya 3:5

1 Wafalme 5:9

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 2:15, 16; Ezr 3:7

1 Wafalme 5:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Kori moja ilikuwa sawa na litre 220 (vibaba 200). Angalia Nyongeza B14.

  • *

    Tnn., “za mafuta yenye yalipondwa.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 2:10

1 Wafalme 5:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “agano.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 3:12; 4:29; Yak 1:5

1 Wafalme 5:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 9:15

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/2/2005, uku. 23-24

1 Wafalme 5:14

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 20:24; 1 Fal. 4:6; 12:18

1 Wafalme 5:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “wabeba-mizigo.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 22:15
  • +Yosh. 16:10; 1 Fal. 9:20-22; 2Nya 2:2, 17, 18; 8:7-9

1 Wafalme 5:16

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 9:23

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    1/12/2005, uku. 19

1 Wafalme 5:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 7:9; 1Nya 22:2
  • +Ufu 21:14
  • +1 Fal. 6:7

1 Wafalme 5:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yosh. 13:1, 5

Maandiko ingine

1 Fa. 5:1Eze 27:3
1 Fa. 5:12 Sa. 5:11
1 Fa. 5:22Nya 2:3
1 Fa. 5:32 Sa. 7:5; 1Nya 22:7, 8
1 Fa. 5:41 Fal. 4:24, 25
1 Fa. 5:4Mez. 16:7
1 Fa. 5:52 Sa. 7:12, 13; 1Nya 22:9, 10; 2Nya 2:4
1 Fa. 5:61 Fal. 6:9, 20
1 Fa. 5:62Nya 2:8
1 Fa. 5:72Nya 2:11, 12
1 Fa. 5:82 Sa. 6:5; 1 Fal. 6:15; 2Nya 3:5
1 Fa. 5:92Nya 2:15, 16; Ezr 3:7
1 Fa. 5:112Nya 2:10
1 Fa. 5:121 Fal. 3:12; 4:29; Yak 1:5
1 Fa. 5:131 Fal. 9:15
1 Fa. 5:142 Sa. 20:24; 1 Fal. 4:6; 12:18
1 Fa. 5:151Nya 22:15
1 Fa. 5:15Yosh. 16:10; 1 Fal. 9:20-22; 2Nya 2:2, 17, 18; 8:7-9
1 Fa. 5:161 Fal. 9:23
1 Fa. 5:171 Fal. 7:9; 1Nya 22:2
1 Fa. 5:17Ufu 21:14
1 Fa. 5:171 Fal. 6:7
1 Fa. 5:18Yosh. 13:1, 5
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
1 Wafalme 5:1-18

Cha Kwanza cha Wafalme

5 Wakati Hiramu mufalme wa Tiro+ alisikia kwamba Sulemani ametiwa mafuta kuwa mufalme pa nafasi ya baba yake, alituma watumishi wake kwa Sulemani, kwa maana sikuzote Hiramu alikuwa rafiki ya Daudi.*+ 2 Sulemani pia akatuma ujumbe kwa Hiramu:+ 3 “Unajua muzuri kwamba Daudi baba yangu hakuweza kujenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wake kwa sababu ya vita vyenye watu walipigana naye pande zote mupaka wakati Yehova aliweka maadui wake chini ya vikanyangio vya miguu yake.+ 4 Lakini sasa Yehova Mungu wangu amenipatia pumuziko pande zote.+ Hakuna mutu yeyote mwenye ananipinga na hakuna jambo lolote la mubaya lenye linatendeka.+ 5 Kwa hiyo ninakusudia kujenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wangu, kama vile Yehova alimuahidi Daudi baba yangu, kwa kusema: ‘Mwana wako mwenye nitaweka kwenye kiti chako cha ufalme pa nafasi yako ndiye atajenga nyumba kwa ajili ya jina langu.’+ 6 Sasa amuru watu wako wanikatie mierezi ya Lebanoni.+ Watumishi wangu watafanya kazi pamoja na watumishi wako, na nitalipa malipo ya watumishi wako kulingana na kiasi chenye utaweka, kwa maana unajua kwamba hakuna mutu yeyote kati yetu mwenye anajua kukata miti kama Wasidoni.”+

7 Wakati Hiramu alisikia maneno ya Sulemani, akafurahi sana na kusema: “Yehova asifiwe leo, kwa maana amemupatia Daudi mwana mwenye hekima ili atawale watu hawa wengi!”+ 8 Basi Hiramu akatuma ujumbe kwa Sulemani: “Nimesikia ujumbe wenye ulinitumia. Nitatimiza mambo yote yenye unataka kwa kutoa mbao za mierezi na za miberoshi.+ 9 Watumishi wangu watazishusha kutoka Lebanoni mupaka kwenye bahari, na nitazifunga mafungu-mafungu ili ziende juu ya bahari mupaka mahali utaniambia. Nitazifungua pale, na utazibeba. Na wewe kwa upande wako, utatoa chakula chenye nitaomba kwa ajili ya nyumba yangu.”+

10 Basi Hiramu akatoa mbao zote za mierezi na za miberoshi zenye Sulemani alitaka. 11 Na Sulemani akapatia Hiramu vipimo elfu makumi mbili (20 000) vya kori* vya ngano kuwa chakula kwa ajili ya nyumba yake na vipimo makumi mbili (20) vya kori vya mafuta ya muzuri sana ya zeituni.* Hivyo ndivyo vitu vyenye Sulemani alimupatia Hiramu mwaka kwa mwaka.+ 12 Na Yehova akamupatia Sulemani hekima, kama vile Yeye alikuwa amemuahidi.+ Na kulikuwa amani kati ya Hiramu na Sulemani, na wote wawili wakafanya mapatano.*

13 Mufalme Sulemani aliandikisha wanaume kwa ajili ya kazi ya kulazimishwa kutoka katika Israeli yote; wanaume elfu makumi tatu (30 000) waliandikishwa.+ 14 Alikuwa anawatuma Lebanoni kwa kubadilishana, wanaume elfu kumi (10 000) kila mwezi. Walikuwa wanapitisha mwezi mumoja katika Lebanoni na miezi mbili kwenye nyumba zao; na Adoniramu+ alikuwa anasimamia wale wenye waliandikishwa kwa ajili ya kazi ya kulazimishwa. 15 Sulemani alikuwa na wafanyakazi wa kawaida* elfu makumi saba (70 000) na watu elfu makumi munane (80 000) wenye kuchonga majiwe+ katika milima,+ 16 na pia wasimamizi wa kifalme elfu tatu mia tatu (3 300) wa Sulemani+ wenye walitumika kama wasimamizi ili kusimamia wafanyakazi. 17 Kwa agizo la mufalme, walichimba majiwe makubwa,+ majiwe yenye bei kali,+ ili kujenga musingi wa nyumba kwa majiwe yenye kuchongwa.+ 18 Kwa hiyo wajenzi wa Sulemani na wajenzi wa Hiramu na Wagebali+ walikata majiwe, na walitayarisha mbao na majiwe ili kujenga nyumba hiyo.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine