Cha Pili cha Mambo ya Nyakati
11 Wakati Rehoboamu alifika Yerusalemu, alikusanya mara moja nyumba ya Yuda na Benyamini,+ wapiganaji-vita elfu mia moja makumi munane (180 000) wenye walizoezwa,* wapigane na Israeli ili kurudisha ufalme kwa Rehoboamu.+ 2 Kisha neno la Yehova likakuja kwa Shemaya+ mutu wa Mungu wa kweli, na kusema: 3 “Ambia Rehoboamu mwana wa Sulemani mufalme wa Yuda na uambie Israeli wote wenye kuwa katika Yuda na Benyamini, 4 ‘Yehova anasema hivi: “Hamupaswe kupanda na kupigana na ndugu zenu. Kila mumoja wenu arudie kwenye nyumba yake, kwa maana nimefanya mambo haya yatendeke.”’”+ Basi wakatii neno la Yehova na wakarudia na hawakuenda tena kupigana na Yeroboamu.
5 Rehoboamu aliishi Yerusalemu na alijenga miji yenye ngome katika Yuda. 6 Basi akajenga* Betlehemu,+ Etamu, Tekoa,+ 7 Bet-suri, Soko,+ Adulamu,+ 8 Gati,+ Maresha, Zifu,+ 9 Adoraimu, Lakishi,+ Azeka,+ 10 Sora, Aiyaloni,+ na Hebroni,+ miji yenye ngome yenye ilikuwa katika Yuda na Benyamini. 11 Tena, akafanya imara maeneo yenye ngome na akaweka makamanda ndani na kuwapatia chakula na mafuta na divai, 12 na akatia ngao kubwa na mikuki katika miji yote mbalimbali; akaifanya imara kwa kiwango kikubwa sana. Na Yuda na Benyamini wakaendelea kuwa wake.
13 Na makuhani na Walawi wenye walikuwa katika Israeli yote wakajiweka upande wake, wakikuja kutoka katika maeneo yao yote. 14 Walawi waliacha malisho yao na eneo lao+ na wakakuja Yuda na Yerusalemu, kwa sababu Yeroboamu na wana wake walikuwa wamewaondoa ili wasitumike tena wakiwa makuhani kwa ajili ya Yehova.+ 15 Kisha Yeroboamu akaweka makuhani wake mwenyewe kwa ajili ya mahali pa juu+ na kwa ajili ya pepo wachafu wenye kufanana na mbuzi*+ na vitoto-dume vya ngombe vyenye alikuwa ametengeneza.+ 16 Na wale wenye walitoka katika makabila yote ya Israeli wenye walikuwa wameweka moyo wao ili kumutafuta Yehova Mungu wa Israeli wakawafuata mupaka Yerusalemu ili kumutolea zabihu Yehova Mungu wa mababu zao.+ 17 Kwa miaka tatu (3) walitia nguvu ufalme wa Yuda na kumuunga mukono Rehoboamu mwana wa Sulemani, kwa maana walitembea katika njia ya Daudi na Sulemani kwa miaka tatu.
18 Kisha Rehoboamu akamuchukua Mahalati binti ya Yerimoti mwana wa Daudi na wa Abihaili binti ya Eliabu mwana wa Yese kuwa bibi yake.+ 19 Kisha wakati fulani akamuzalia wana: Yeushi, Shemaria, na Zahamu. 20 Kisha yeye, akaoa Maaka mujukuu wa Absalomu.+ Kisha wakati fulani akamuzalia Abiya,+ Atai, Ziza, na Shelomiti. 21 Rehoboamu alimupenda zaidi Maaka mujukuu wa Absalomu kuliko bibi zake wengine wote na masuria,*+ kwa maana alichukua bibi kumi na munane (18) na masuria makumi sita (60), na akazaa watoto wanaume makumi mbili na munane (28) na watoto wanamuke makumi sita. 22 Kwa hiyo Rehoboamu akamuweka Abiya mwana wa Maaka kuwa kichwa na kiongozi kati ya ndugu zake, kwa maana alikusudia kumufanya kuwa mufalme. 23 Lakini, alitenda kwa uelewaji na akatuma* wamoja kati ya wana wake kwenye maeneo yote ya Yuda na Benyamini, kwenye miji yote yenye ngome,+ na akawapatia chakula kingi na kuwapatia bibi wengi.