Cha Pili cha Mambo ya Nyakati
12 Kisha tu ufalme wa Rehoboamu kufanywa imara kabisa+ na wakati alikuwa amepata nguvu, aliacha Sheria ya Yehova,+ na Israeli wote pia pamoja naye. 2 Katika mwaka wa tano (5) wa Mufalme Rehoboamu, Mufalme Shishaki+ wa Misri alipanda ili kushambulia Yerusalemu, kwa maana walikuwa wamejiendesha kwa kukosa uaminifu kumuelekea Yehova. 3 Alikuwa na magari elfu moja mia mbili (1 200), wapanda-farasi elfu makumi sita (60 000), na maaskari wenye hawawezi kuhesabika wenye walikuja pamoja naye kutoka Misri—Walibya, Wasukii, na Waetiopia.+ 4 Alikamata miji yenye ngome ya Yuda na mwishowe akafika Yerusalemu.
5 Shemaya+ nabii akakuja kwa Rehoboamu na kwa wakubwa wa Yuda wenye walikuwa wamekusanyika Yerusalemu kwa sababu ya Shishaki, na akawaambia: “Yehova anasema hivi: ‘Mumeniacha mimi, basi mimi pia nimewaacha ninyi+ katika mukono wa Shishaki.’” 6 Halafu wakubwa wa Israeli na mufalme wakajinyenyekeza+ na kusema: “Yehova ni mwenye haki.” 7 Wakati Yehova aliona kwamba walikuwa wamejinyenyekeza, neno la Yehova likakuja kwa Shemaya, na kusema: “Wamejinyenyekeza. Sitawaharibu,+ na kisha wakati kidogo nitawaokoa. Sitamwangia Yerusalemu kasirani yangu kali kupitia Shishaki. 8 Lakini watakuwa watumishi wake, na hivyo watajua tofauti kati ya kunitumikia mimi na kutumikia wafalme wa* inchi zingine.”
9 Basi Mufalme Shishaki wa Misri akapanda ili kushambulia Yerusalemu. Akakamata hazina za nyumba ya Yehova+ na hazina za nyumba ya mufalme. Alikamata kila kitu, kutia ndani zile ngao za zahabu zenye Sulemani alikuwa ametengeneza.+ 10 Basi Mufalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba zichukue nafasi ya ngao hizo, akaziweka chini ya ulinzi wa wakubwa wa walinzi,* wenye walilinda muingilio wa nyumba ya mufalme. 11 Kila mara wakati mufalme alikuja kwenye nyumba ya Yehova, walinzi walikuwa wanaingia na kuzibeba, kisha walikuwa wanazirudisha katika chumba cha walinzi. 12 Kwa sababu mufalme alijinyenyekeza, kasirani ya Yehova ikageuka kutoka kwake,+ na hakuwaharibu kabisa.+ Zaidi ya hayo, kulikuwa mambo fulani ya muzuri yenye yalipatikana katika Yuda.+
13 Mufalme Rehoboamu alitia nguvu mamlaka yake katika Yerusalemu na akaendelea kutawala; Rehoboamu alikuwa na miaka makumi ine na moja (41) wakati alikuwa mufalme, na alitawala kwa miaka kumi na saba (17) katika Yerusalemu, muji wenye Yehova alikuwa amechagua kutoka katika makabila yote ya Israeli kuwa mahali pa kutia jina lake. Jina la mama ya mufalme lilikuwa Naama Mwamoni.+ 14 Lakini alifanya mambo ya mubaya, kwa maana hakukuwa ameazimia katika moyo wake kumutafuta Yehova.+
15 Na historia ya Rehoboamu, kuanzia mwanzo mupaka mwisho, je, haiandikwe kati ya maneno ya Shemaya+ nabii na ya Ido+ muonaji katika maandikisho kulingana na ukoo? Na kulikuwa vita sikuzote kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.+ 16 Kisha Rehoboamu akalalishwa na kupumuzika pamoja na mababu zake na akazikwa katika Muji wa Daudi;+ na Abiya+ mwana wake akakuwa mufalme pa nafasi yake.