Cha Pili cha Mambo ya Nyakati
27 Yotamu+ alikuwa na miaka makumi mbili na tano (25) wakati alikuwa mufalme, na alitawala kwa miaka kumi na sita (16) katika Yerusalemu. Jina la mama yake lilikuwa Yerusha binti ya Sadoki.+ 2 Aliendelea kufanya mambo yenye yalikuwa sawa mbele ya macho ya Yehova, kama vile Uzia baba yake alikuwa amefanya,+ isipokuwa tu hakuingia kwa nguvu katika hekalu la Yehova.+ Lakini watu walikuwa wangali wanatenda kwa uharibifu. 3 Alijenga mulango mukubwa wa juu wa nyumba ya Yehova,+ na alifanya kazi kubwa ya ujenzi kwenye ukuta wa Ofeli.+ 4 Alijenga pia miji+ katika eneo lenye milima la Yuda,+ na alijenga ngome+ na minara+ katika maeneo yenye miti. 5 Alipigana vita na mufalme wa Waamoni+ na mwishowe akawashinda, na hivyo Waamoni wakamupatia katika mwaka huo talanta* mia moja (100) za feza, kori* elfu kumi (10 000) za ngano, na elfu kumi za shayiri. Waamoni walimulipa pia vitu hivyo katika mwaka wa pili na wa tatu (3).+ 6 Basi Yotamu akaendelea kupata nguvu, kwa maana alifanya imara* njia zake mbele ya Yehova Mungu wake.
7 Na mambo mengine ya historia ya Yotamu, vita zake zote na njia zake, yameandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Israeli na wa Yuda.+ 8 Alikuwa na miaka makumi mbili na tano (25) wakati alikuwa mufalme, na alitawala kwa miaka kumi na sita (16) katika Yerusalemu.+ 9 Kisha Yotamu akalalishwa na kupumuzika pamoja na mababu zake, na wakamuzika katika Muji wa Daudi.+ Na Ahazi mwana wake akakuwa mufalme pa nafasi yake.+