Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 29
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika 2 Mambo ya Nyakati

      • Hezekia, mufalme wa Yuda (1, 2)

      • Mabadiliko yenye yalifanywa na Hezekia (3-11)

      • Hekalu linatakaswa (12-19)

      • Utumishi wa hekalu unarudishwa (20-36)

2 Mambo ya Nyakati 29:1

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 1:1; Ho 1:1; Mt 1:10
  • +2 Fal. 18:1, 2

2 Mambo ya Nyakati 29:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 31:20
  • +1 Fal. 15:5; 2 Fal. 18:3

2 Mambo ya Nyakati 29:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 6:33, 34; 2Nya 28:24

2 Mambo ya Nyakati 29:5

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 15:11, 12
  • +2 Fal. 18:4

2 Mambo ya Nyakati 29:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 28:22, 23; Yer 44:21
  • +Yer 2:27; Eze 8:16

2 Mambo ya Nyakati 29:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 6:33, 34
  • +Law. 24:2
  • +Kut 30:8
  • +Kut 29:38

2 Mambo ya Nyakati 29:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “cha kuchekelewa.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 24:18
  • +Law. 26:32; Kum 28:15, 25

2 Mambo ya Nyakati 29:9

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 26:14, 17
  • +2Nya 28:5-8

2 Mambo ya Nyakati 29:10

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 15:10-13

2 Mambo ya Nyakati 29:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kupumuzika.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 3:6; Kum 10:8
  • +1Nya 23:13

2 Mambo ya Nyakati 29:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 4:2, 3; 1Nya 23:12
  • +1Nya 23:21
  • +1Nya 23:7

2 Mambo ya Nyakati 29:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 15:16, 17; 25:1, 2

2 Mambo ya Nyakati 29:14

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 25:5
  • +1Nya 25:1

2 Mambo ya Nyakati 29:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 29:5

2 Mambo ya Nyakati 29:16

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 6:36
  • +2 Fal. 23:4, 6; 2Nya 15:16; Yoh 18:1

2 Mambo ya Nyakati 29:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 6:3; 1Nya 28:11

2 Mambo ya Nyakati 29:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Ni kusema, mikate ya wonyesho.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 4:1
  • +1 Fal. 7:40
  • +1 Fal. 7:48

2 Mambo ya Nyakati 29:19

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 28:1, 2, 24
  • +2Nya 29:5

2 Mambo ya Nyakati 29:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 4:3, 13, 14; Hes 15:22-24

2 Mambo ya Nyakati 29:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

  • *

    Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

  • *

    Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 4:4
  • +Law. 4:7, 18

2 Mambo ya Nyakati 29:25

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 25:1, 6; 2Nya 9:11
  • +1Nya 28:12, 13; 2Nya 8:12, 14
  • +2 Sa. 24:11, 12; 1Nya 29:29
  • +2 Sa. 7:2; 12:1

2 Mambo ya Nyakati 29:26

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 10:8; 1Nya 15:24

2 Mambo ya Nyakati 29:27

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 1:3, 4

2 Mambo ya Nyakati 29:30

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 23:1
  • +1Nya 16:7

2 Mambo ya Nyakati 29:31

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Sasa mumejaza mukono wenu.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 1:3

2 Mambo ya Nyakati 29:32

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 3:4; 8:63; 1Nya 29:21, 22

2 Mambo ya Nyakati 29:34

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wanyoofu zaidi wa moyo.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 8:19; 2Nya 30:17; 35:10, 11
  • +2Nya 30:2, 3

2 Mambo ya Nyakati 29:35

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “ukatayarishwa.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 29:32
  • +Law. 3:1, 14-16
  • +Hes 15:5

2 Mambo ya Nyakati 29:36

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 30:12

Maandiko ingine

2 Nya. 29:1Isa 1:1; Ho 1:1; Mt 1:10
2 Nya. 29:12 Fal. 18:1, 2
2 Nya. 29:22Nya 31:20
2 Nya. 29:21 Fal. 15:5; 2 Fal. 18:3
2 Nya. 29:31 Fal. 6:33, 34; 2Nya 28:24
2 Nya. 29:51Nya 15:11, 12
2 Nya. 29:52 Fal. 18:4
2 Nya. 29:62Nya 28:22, 23; Yer 44:21
2 Nya. 29:6Yer 2:27; Eze 8:16
2 Nya. 29:71 Fal. 6:33, 34
2 Nya. 29:7Law. 24:2
2 Nya. 29:7Kut 30:8
2 Nya. 29:7Kut 29:38
2 Nya. 29:82Nya 24:18
2 Nya. 29:8Law. 26:32; Kum 28:15, 25
2 Nya. 29:9Law. 26:14, 17
2 Nya. 29:92Nya 28:5-8
2 Nya. 29:102Nya 15:10-13
2 Nya. 29:11Hes 3:6; Kum 10:8
2 Nya. 29:111Nya 23:13
2 Nya. 29:12Hes 4:2, 3; 1Nya 23:12
2 Nya. 29:121Nya 23:21
2 Nya. 29:121Nya 23:7
2 Nya. 29:131Nya 15:16, 17; 25:1, 2
2 Nya. 29:141Nya 25:5
2 Nya. 29:141Nya 25:1
2 Nya. 29:152Nya 29:5
2 Nya. 29:161 Fal. 6:36
2 Nya. 29:162 Fal. 23:4, 6; 2Nya 15:16; Yoh 18:1
2 Nya. 29:171 Fal. 6:3; 1Nya 28:11
2 Nya. 29:182Nya 4:1
2 Nya. 29:181 Fal. 7:40
2 Nya. 29:181 Fal. 7:48
2 Nya. 29:192Nya 28:1, 2, 24
2 Nya. 29:192Nya 29:5
2 Nya. 29:21Law. 4:3, 13, 14; Hes 15:22-24
2 Nya. 29:22Law. 4:4
2 Nya. 29:22Law. 4:7, 18
2 Nya. 29:251Nya 25:1, 6; 2Nya 9:11
2 Nya. 29:251Nya 28:12, 13; 2Nya 8:12, 14
2 Nya. 29:252 Sa. 24:11, 12; 1Nya 29:29
2 Nya. 29:252 Sa. 7:2; 12:1
2 Nya. 29:26Hes 10:8; 1Nya 15:24
2 Nya. 29:27Law. 1:3, 4
2 Nya. 29:302 Sa. 23:1
2 Nya. 29:301Nya 16:7
2 Nya. 29:31Law. 1:3
2 Nya. 29:321 Fal. 3:4; 8:63; 1Nya 29:21, 22
2 Nya. 29:34Hes 8:19; 2Nya 30:17; 35:10, 11
2 Nya. 29:342Nya 30:2, 3
2 Nya. 29:352Nya 29:32
2 Nya. 29:35Law. 3:1, 14-16
2 Nya. 29:35Hes 15:5
2 Nya. 29:362Nya 30:12
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
2 Mambo ya Nyakati 29:1-36

Cha Pili cha Mambo ya Nyakati

29 Hezekia+ alikuwa mufalme akiwa na miaka makumi mbili na tano (25), na alitawala kwa miaka makumi mbili na kenda (29) katika Yerusalemu. Jina la mama yake lilikuwa Abiya binti ya Zekaria.+ 2 Aliendelea kufanya mambo yenye yalikuwa sawa mbele ya macho ya Yehova,+ kama vile Daudi babu yake alikuwa amefanya.+ 3 Katika mwaka wa kwanza wa utawala wake, katika mwezi wa kwanza, alifungua milango ya nyumba ya Yehova na kuitengeneza.+ 4 Kisha akaleta makuhani na Walawi na kuwakusanya kwenye kiwanja chenye kuwa upande wa mashariki. 5 Akawaambia: “Munisikilize, ninyi Walawi. Sasa mujitakase+ na mutakase nyumba ya Yehova Mungu wa mababu zenu, na mutoshe kitu kichafu mahali patakatifu.+ 6 Kwa maana baba zetu wamekosa uaminifu na wamefanya mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova Mungu wetu.+ Walimuacha na kugeuza nyuso zao kutoka kwenye tabenakulo ya Yehova na kumugeuzia mugongo.+ 7 Pia, walifunga milango ya baraza+ na kuzima taa.+ Waliacha kuchoma uvumba+ na kutoa zabihu za kuteketezwa+ katika mahali patakatifu kwa Mungu wa Israeli. 8 Kwa hiyo, kasirani ya Yehova ikakuja juu ya Yuda na Yerusalemu,+ na hivyo akawafanya kuwa kitu cha kuogopesha na cha kushangaza na kitu cha kupigiwa muluzi,* kama vile munaona kwa macho yenu wenyewe.+ 9 Angalia, mababu zetu walianguka kwa upanga,+ na watoto wetu wanaume, watoto wetu wanamuke, na bibi zetu wakapelekwa katika utekwa kwa sababu ya mambo hayo.+ 10 Sasa ni tamaa ya moyo wangu kufanya agano pamoja na Yehova Mungu wa Israeli,+ ili kasirani yake yenye kuwaka igeuke kutoka kwetu. 11 Wana wangu, sasa haiko wakati wa kupuuza mambo,* kwa maana Yehova amewachagua ninyi musimame mbele yake, ili mukuwe watumishi wake,+ na kuchoma zabihu zake ili zitoe moshi.”+

12 Halafu Walawi wakasimama: Mahati mwana wa Amasai na Yoeli mwana wa Azaria wa Wakohati;+ kutoka kwa Wamerari,+ Kishi mwana wa Abdi na Azaria mwana wa Yehaleleli; kutoka kwa Wagershoni,+ Yoa mwana wa Zima na Edeni mwana wa Yoa; 13 kutoka kwa wana wa Elisafani, Shimri na Yeueli; kutoka kwa wana wa Asafu,+ Zekaria na Matania; 14 kutoka kwa wana wa Hemani,+ Yehieli na Shimei; kutoka kwa wana wa Yedutuni,+ Shemaya na Uzieli. 15 Kisha wakakusanya pamoja ndugu zao na wakajitakasa na kuja, kama vile mufalme alikuwa ameamuru kulingana na maneno ya Yehova, ili kutakasa nyumba ya Yehova.+ 16 Kisha makuhani wakaingia ndani ya nyumba ya Yehova ili kufanya utakaso na wakapeleka inje uchafu wote wenye walipata katika hekalu la Yehova na kuupeleka kwenye kiwanja+ cha nyumba ya Yehova. Walawi nao wakaukamata na kuupeleka inje kwenye Bonde la Kidroni.+ 17 Kwa hiyo wakaanza kazi hiyo ya kutakasa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, na katika siku ya munane (8) ya mwezi huo wakafika kwenye baraza la Yehova.+ Walitakasa nyumba ya Yehova kwa siku munane, na katika siku ya kumi na sita (16) ya mwezi wa kwanza wakamaliza.

18 Kisha, wakaingia kwa Mufalme Hezekia na kusema: “Tumetakasa nyumba yote ya Yehova, mazabahu ya toleo la kuteketezwa+ na vyombo vyake vyote,+ na meza ya mikate yenye kupangwa moja juu ya ingine*+ na vyombo vyake vyote. 19 Na vyombo vyote vyenye Mufalme Ahazi aliondoa wakati wa utawala wake wakati alitenda kwa kukosa uaminifu+ tumevitayarisha na kuvitakasa,+ na viko mbele ya mazabahu ya Yehova.”

20 Na Mufalme Hezekia akaamuka asubui sana na kukusanya pamoja wakubwa wa muji, na wakapanda kuenda kwenye nyumba ya Yehova. 21 Wakaleta ngombe-dume saba (7), kondoo-dume saba, na wana-kondoo dume saba, na mbuzi-dume saba kuwa toleo la zambi kwa ajili ya ufalme, kwa ajili ya patakatifu, na kwa ajili ya Yuda.+ Basi akaambia makuhani, wazao wa Haruni, wawatoe kwenye mazabahu ya Yehova. 22 Kisha wakachinja ngombe hao,+ na makuhani wakakamata damu na kuinyunyiza* kwenye mazabahu;+ kisha wakachinja wale kondoo-dume na kunyunyiza* damu kwenye mazabahu, na wakachinja wale wana-kondoo dume na kunyunyiza* damu kwenye mazabahu. 23 Kisha wakaleta wale mbuzi-dume wa toleo la zambi mbele ya mufalme na kutaniko na wakaweka mikono yao juu yao. 24 Makuhani wakawachinja na kufanya toleo la zambi kupitia damu yao kwenye mazabahu, ili kufunika zambi kwa ajili ya Israeli wote, kwa sababu mufalme alisema kwamba toleo la kuteketezwa na toleo la zambi vilipaswa kuwa kwa ajili ya Israeli wote.

25 Wakati huo, aliweka Walawi kwenye nyumba ya Yehova wakiwa na matoazi, vyombo vya kamba, na vinubi,+ kupitia amri ya Daudi+ na ya Gadi+ muonaji wa mufalme na ya Natani+ nabii, kwa maana amri hiyo ilitoka kwa Yehova kupitia manabii wake. 26 Basi Walawi walikuwa wanasimama wakiwa na vyombo vya Daudi, na makuhani wakiwa na tarumbeta.+

27 Kisha Hezekia akaagiza zabihu ya kuteketezwa itolewe kwenye mazabahu.+ Wakati toleo la kuteketezwa lilianza, wimbo wa Yehova ulianza na pia tarumbeta, kwa kufuata muongozo wa vyombo vya Mufalme Daudi wa Israeli. 28 Na kutaniko lote likainama wakati wimbo huo ulikuwa unaimbwa na wakati tarumbeta zilikuwa zinapigwa⁠—mambo yote hayo yaliendelea mupaka wakati toleo la zabihu lilimalizika. 29 Na wakati tu walimaliza kufanya toleo, mufalme na watu wote wenye walikuwa pamoja naye wakainama na kushusha nyuso chini. 30 Sasa Mufalme Hezekia na wakubwa wakaambia Walawi wamusifu Yehova kwa maneno ya Daudi+ na ya Asafu+ muonaji. Basi wakatoa sifa kwa furaha kubwa, na wakainama na kushusha nyuso chini.

31 Kisha Hezekia akasema: “Sasa kwa kuwa mumewekwa pembeni* kwa ajili ya Yehova, mukuje na mulete zabihu na matoleo ya shukrani kwenye nyumba ya Yehova.” Basi kutaniko likaanza kuleta zabihu na matoleo ya shukrani, na kila mutu mwenye alikuwa na moyo wa kutoa kwa kupenda alileta matoleo ya kuteketezwa.+ 32 Hesabu ya matoleo ya kuteketezwa yenye kutaniko lilileta ilikuwa ngombe makumi saba (70), kondoo-dume mia moja (100), wana-kondoo dume mia mbili (200)⁠—​wote hao wakiwa toleo la kuteketezwa kwa Yehova+⁠— 33 na matoleo matakatifu yalikuwa ngombe mia sita (600) na wanyama elfu tatu (3 000) kutoka katika kundi. 34 Lakini hakukuwa makuhani wa kuenea ili kuondoa ngozi matoleo yote ya kuteketezwa, basi ndugu zao Walawi wakawasaidia+ mupaka wakati kazi hiyo ilimalizika na mupaka wakati makuhani waliweza kujitakasa,+ kwa maana Walawi walikuwa na bidii zaidi* katika kujitakasa kuliko makuhani. 35 Pia, kulikuwa matoleo mengi ya kuteketezwa,+ na vilevile vipande vya mafuta vya zabihu za ushirika+ na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya matoleo ya kuteketezwa.+ Hivyo utumishi wa nyumba ya Yehova ukarudishwa.* 36 Kwa hiyo Hezekia na watu wote wakafurahi juu ya jambo lenye Mungu wa kweli alikuwa amefanyia watu,+ kwa sababu jambo hilo lilikuwa limetokea kwa kushitukia.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine