Kutoka
10 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Ingia kwa Farao, kwa sababu nimeacha moyo wake na mioyo ya watumishi wake ikuwe migumu,+ ili nionyeshe alama zangu hizi mbele yake,+ 2 na ili muweze kuelezea wana wenu na wajukuu wenu namna nilitendea Misri kwa ukali na alama zenye nilifanya kati yao;+ na hakika mutajua kwamba mimi ni Yehova.”
3 Kwa hiyo Musa na Haruni wakaingia kwa Farao na kumuambia: “Yehova Mungu wa Waebrania anasema hivi: ‘Utakataa kujinyenyekeza kwangu mupaka wakati gani?+ Ruhusu watu wangu waende ili waweze kunitumikia. 4 Kwa maana kama unaendelea kukataa kuruhusu watu wangu waende, angalia, kesho nitaleta nzige ndani ya mipaka yako. 5 Na nzige watafunika uso wa dunia, na haitawezekana kuona udongo. Watakula kila kitu chenye kilibakia kisha mvua ya majiwe na chenye kiliachwa kwa ajili yenu, na watakula miti yenu yote yenye kuota katika eneo la mashamba.+ 6 Watajaa ndani ya nyumba zako, ndani ya nyumba za watumishi wako wote, na ndani ya nyumba zote za Misri kwa kadiri yenye baba zako na mababu zako hawajapata kuona tangu wakati walikuwa katika inchi hii mupaka leo.’”+ Kisha akatoka mbele ya Farao.
7 Kisha watumishi wa Farao wakamuambia: “Mutu huyu ataendelea kuwa hatari kwetu* mupaka wakati gani? Ruhusu Waisraeli waende ili waweze kumutumikia Yehova Mungu wao. Je, hauone kwamba Misri imeangamia?” 8 Kwa hiyo Musa na Haruni wakarudishwa kwa Farao, naye akawaambia: “Muende, mumutumikie Yehova Mungu wenu. Lakini ni nani kabisa wataenda?” 9 Kisha Musa akasema: “Tutaenda pamoja na vijana wetu, wazee wetu, watoto wetu wanaume, na watoto wetu wanamuke, kondoo zetu, na ngombe zetu,+ kwa maana tutamufanyia Yehova sikukuu.”+ 10 Farao akawaambia: “Kama nitawaruhusu ninyi na watoto wenu muende, basi Yehova iko* kabisa pamoja na ninyi!+ Ni wazi kwamba muko na nia ya kufanya jambo fulani la mubaya. 11 Hapana! Ni wanaume wenu tu ndio wanaweza kuenda na kumutumikia Yehova, kwa sababu ni kile muliomba.” Kwa hiyo wakafukuzwa mbele ya Farao.
12 Sasa Yehova akamuambia Musa: “Nyoosha mukono wako juu ya inchi ya Misri ili nzige wakuje juu ya inchi ya Misri na kula mimea yote ya inchi, kila kitu chenye majiwe ya mvua yaliacha.” 13 Mara moja Musa akanyoosha fimbo yake juu ya inchi ya Misri, na Yehova akafanya upepo wa mashariki uvume juu ya inchi muchana wote na usiku wote. Wakati asubui ilifika, upepo huo wa mashariki ukaleta nzige. 14 Na nzige hao wakakuja juu ya inchi yote ya Misri na wakashuka juu ya eneo lote la Misri.+ Hali ilikuwa mubaya sana,+ na hakuna siku kulikuwa kumetokea nzige wengi sana hivyo, na hakuna siku kungekuwa tena nzige wengi kama hao. 15 Walifunika uso wa inchi yote, na inchi ikakuwa na giza kwa sababu yao, nao wakakula mimea yote ya inchi na matunda yote ya miti yenye majiwe ya mvua yalikuwa yameacha; hakuna majani yenye yalibakia juu ya miti wala juu ya mimea ya mashamba yenye yalibakia katika inchi yote ya Misri.
16 Kwa hiyo Farao akaita haraka Musa na Haruni na kusema: “Nimetenda zambi juu ya Yehova Mungu wenu na juu yenu. 17 Sasa, tafazali, musamehe zambi yangu mara hii moja tu, na mumulilie Yehova Mungu wenu ili anitoshee pigo hili lenye kuleta kifo.” 18 Kwa hiyo akatoka* mbele ya Farao na kumulilia Yehova.+ 19 Kisha Yehova akageuza upepo huo, nao ukaanza kuvuma kwa nguvu kuelekea mangaribi, nao ukapeperusha nzige hao na kuwapeleka katika Bahari Nyekundu. Hakuna hata nzige mumoja mwenye alibakia katika eneo lote la Misri. 20 Lakini, Yehova akaacha moyo wa Farao ukuwe mugumu,+ na hakuruhusu Waisraeli waende.
21 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Nyoosha mukono wako kuelekea mbinguni ili kukuwe giza juu ya inchi ya Misri, giza nzito lenye linaweza kuguswa.” 22 Mara moja Musa akanyoosha mukono wake kuelekea mbinguni, na kukakuwa giza nzito katika inchi yote ya Misri kwa siku tatu (3).+ 23 Hakuna mwenye alikuwa anaona mwingine, na hakuna mwenye alitoka mahali alikuwa kwa siku tatu (3); lakini Waisraeli wote walikuwa na mwangaza katika makao yao.+ 24 Kisha Farao akaita Musa na kusema: “Muende, mumutumikie Yehova.+ Ni kondoo zenu na ngombe zenu tu ndio watabakia. Hata watoto wenu wanaweza kuenda pamoja na ninyi.” 25 Lakini Musa akasema: “Wewe mwenyewe pia utatupatia* zabihu na matoleo ya kuteketezwa, na tutayatolea Yehova Mungu wetu.+ 26 Mifugo yetu itaenda pia pamoja na sisi. Hakuna munyama mwenye atabakia,* kwa sababu tutatumia wanyama fulani kati yao ili kumuabudu Yehova Mungu wetu, na hatujue kile tutatoa ili kumuabudu Yehova mupaka wakati tutafika kule.” 27 Kwa hiyo Yehova akaacha moyo wa Farao ukuwe mugumu, na hakukubali kuwaruhusu waende.+ 28 Farao akamuambia: “Toka mbele ya macho yangu! Usipime kutafuta kuona uso wangu tena, kwa maana siku yenye utaona uso wangu, utakufa.” 29 Kwa hiyo Musa akasema: “Kama vile umesema, sitatafuta kuona uso wako tena.”