Kutoka
11 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Nitaleta pigo moja zaidi juu ya Farao na Misri. Kisha pigo hilo atawaruhusu mutoke hapa.+ Wakati atawaruhusu muende, atawafukuza kabisa mutoke hapa.+ 2 Sasa ambia watu kwamba wanaume wote na wanamuke wanapaswa kuomba majirani wao vitu vya feza na zahabu.”+ 3 Na Yehova akafanya watu wakubaliwe mbele ya macho ya Wamisri. Tena, Musa mwenyewe alifikia kuwa mutu mwenye kuheshimiwa sana katika inchi ya Misri kati ya watumishi wa Farao na kati ya watu.
4 Kisha Musa akasema: “Yehova anasema hivi: ‘Karibu katikati ya usiku nitapita katikati ya Misri,+ 5 na kila muzaliwa wa kwanza katika inchi ya Misri atakufa,+ kuanzia muzaliwa wa kwanza wa Farao mwenye kukaa kwenye kiti chake cha ufalme mupaka muzaliwa wa kwanza wa mutumwa mwanamuke mwenye kufanya kazi juu ya jiwe la kusagia la mukono, na kila muzaliwa wa kwanza wa mifugo.+ 6 Kutakuwa kilio kikubwa katika inchi yote ya Misri, kilio chenye hakuna siku kimekwisha kutokea na hakuna siku kitapata kutokea tena.+ 7 Lakini hakuna hata imbwa mumoja mwenye atafokea* Waisraeli, ikuwe watu ao mifugo yao, ili muweze kujua kwamba Yehova anaweza kufanya kukuwe tofauti kati ya Wamisri na Waisraeli.’”+ 8 Na watumishi wako wote hakika watakuja mbele yangu na kuinamisha uso mupaka chini mbele yangu, na kusema, ‘Uende, wewe pamoja na watu wote wenye kukufuata.’+ Na kisha mambo hayo nitaondoka.” Basi akatoka mbele ya Farao akiwa amewaka kasirani.
9 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Farao hatakusikiliza,+ ili miujiza yangu iongezeke katika inchi ya Misri.”+ 10 Musa na Haruni walifanya miujiza hiyo yote mbele ya Farao,+ lakini Yehova aliacha moyo wa Farao ukuwe mugumu, na hivyo Farao hakuruhusu Waisraeli watoke katika inchi yake.+