Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 11
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Yeremia

      • Yuda wanavunja agano pamoja na Mungu (1-17)

        • Miungu mingi kama miji (13)

      • Yeremia anafananishwa na mwana-kondoo mwenye kupelekwa kwenye machinjo (18-20)

      • Watu wa muji wa Yeremia wanamupinga (21-23)

Yeremia 11:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Inaonekana Yeremia ndiye anaambiwa.

Yeremia 11:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 27:26; 28:15

Yeremia 11:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 24:3
  • +Kut 13:3; Kum 4:20
  • +Law. 26:3, 12

Yeremia 11:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Ikuwe vile.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 15:18; Kut 3:8; Law. 20:24; Kum 6:3

Yeremia 11:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “nikiamuka asubui sana na kuonya.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 7:13; 25:4; 35:15

Yeremia 11:8

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 65:2; Yer 7:24, 26; Eze 20:8; Zek 7:11, 12

Yeremia 11:10

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Amu 2:11, 17; 1 Sa. 8:8; 2 Fal. 22:17
  • +2Nya 28:22, 23
  • +Kum 31:16; 2 Fal. 17:6, 7; Ho 6:7

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi (2007 ),

    15/3/2007, uku. 9

Yeremia 11:11

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 22:16; Yer 6:19; Eze 7:5
  • +Isa 1:15; Yer 14:12; Eze 8:18; Mik 3:4

Yeremia 11:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “wanachoma zabihu ili zitoe moshi kwa ajili yake.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 32:37, 38; Yer 2:28

Yeremia 11:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mungu wa haya.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 7:9, 10

Yeremia 11:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Ni kusema, Yeremia.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 7:16; 14:11

Yeremia 11:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “eko.”

  • *

    Ni kusema, zabihu zenye zilitolewa katika hekalu.

Yeremia 11:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 5:2; Yer 2:21
  • +Yer 19:5, 15

Yeremia 11:19

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 18:18

Yeremia 11:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “hisia za ndani kabisa.” Tnn., “figo.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 28:9; Yer 17:10; 20:12

Yeremia 11:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “wenye wanatafuta nafsi yako.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 1:1
  • +Isa 30:10; Amo 2:12; 7:16

Yeremia 11:22

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 36:17; Omb 2:21
  • +Yer 18:21

Yeremia 11:23

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yosh. 21:8, 18

Maandiko ingine

Yer. 11:3Kum 27:26; 28:15
Yer. 11:4Kut 24:3
Yer. 11:4Kut 13:3; Kum 4:20
Yer. 11:4Law. 26:3, 12
Yer. 11:5Mwa 15:18; Kut 3:8; Law. 20:24; Kum 6:3
Yer. 11:7Yer 7:13; 25:4; 35:15
Yer. 11:8Isa 65:2; Yer 7:24, 26; Eze 20:8; Zek 7:11, 12
Yer. 11:10Amu 2:11, 17; 1 Sa. 8:8; 2 Fal. 22:17
Yer. 11:102Nya 28:22, 23
Yer. 11:10Kum 31:16; 2 Fal. 17:6, 7; Ho 6:7
Yer. 11:112 Fal. 22:16; Yer 6:19; Eze 7:5
Yer. 11:11Isa 1:15; Yer 14:12; Eze 8:18; Mik 3:4
Yer. 11:12Kum 32:37, 38; Yer 2:28
Yer. 11:13Yer 7:9, 10
Yer. 11:14Yer 7:16; 14:11
Yer. 11:17Isa 5:2; Yer 2:21
Yer. 11:17Yer 19:5, 15
Yer. 11:19Yer 18:18
Yer. 11:201Nya 28:9; Yer 17:10; 20:12
Yer. 11:21Yer 1:1
Yer. 11:21Isa 30:10; Amo 2:12; 7:16
Yer. 11:222Nya 36:17; Omb 2:21
Yer. 11:22Yer 18:21
Yer. 11:23Yosh. 21:8, 18
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Yeremia 11:1-23

Yeremia

11 Hili ndilo neno lenye lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova, na kusema: 2 “Musikie maneno ya agano hili, ninyi watu!

“Uyaseme* kwa watu wa Yuda na kwa wakaaji wa Yerusalemu, 3 na uwaambie, ‘Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: “Amelaaniwa mutu mwenye hatii maneno ya agano hili,+ 4 yenye niliamuru mababu zenu siku yenye niliwatosha katika inchi ya Misri,+ kutoka katika tanuru ya kuyeyushia chuma,+ nikisema, ‘Mutii sauti yangu, na mufanye mambo yote yenye ninawaamuru ninyi; na mutakuwa watu wangu na mimi nitakuwa Mungu wenu,+ 5 ili nitimize kiapo chenye niliapia mababu zenu, kuwapatia inchi yenye kutiririka maziwa na asali,+ kama vile hali iko leo.’”’”

Na nikajibu: “Amina,* Ee Yehova.”

6 Kisha Yehova akaniambia: “Tangaza maneno haya yote katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu: ‘Musikie maneno ya agano hili, na muyatimize. 7 Kwa maana nilionya kwa uzito mababu zenu siku yenye niliwatosha katika inchi ya Misri na mupaka leo, nikiwaonya tena na tena:* “Mutii sauti yangu.”+ 8 Lakini hawakusikiliza ao kutega sikio lao; tofauti na hilo, kwa kichwa-nguvu kila mumoja aliendelea kufuata moyo wake muovu.+ Basi nikaleta juu yao maneno yote ya agano hili yenye niliwaamuru wafanye na yenye walikataa kuyatimiza.’”

9 Kisha Yehova akaniambia: “Kuko ujanja kati ya watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu. 10 Wamerudilia makosa ya mababu zao wa zamani, wenye walikataa kutii maneno yangu.+ Wao pia wamefuata miungu mingine na kuitumikia.+ Nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda wamevunja agano langu lenye nilifanya pamoja na mababu zao.+ 11 Kwa hiyo Yehova anasema hivi: ‘Angalia, ninaleta juu yao musiba+ wenye hawataweza kuepuka. Wakati wataniita ili kuomba musaada, sitawasikiliza.+ 12 Kisha miji ya Yuda na wakaaji wa Yerusalemu wataenda kwa miungu yenye wanatolea zabihu* na kuomba musaada,+ lakini haitawaokoa hata kidogo wakati wa musiba wao. 13 Kwa maana miungu yako imekuwa mingi kama miji yako, Ee Yuda, na mumetengeneza mazabahu mengi kama barabara zenye kuwa katika Yerusalemu kwa ajili ya kitu cha haya,* mazabahu za kumutolea Baali zabihu.’+

14 “Na wewe,* usisali kwa ajili ya watu hawa. Usilie kwa sauti kubwa wala kutoa sala kwa ajili yao,+ kwa maana sitasikiliza wakati wataniita kwa sababu ya musiba wao.

15 Mupendwa wangu iko* na haki gani ya kuwa katika nyumba yangu

Wakati wengi wametimiza mipango ya uovu?

Je, kupitia nyama takatifu* watazuia musiba wakati utakuja juu yako?

Je, utafurahi wakati huo?

16 Wakati fulani Yehova alikuita muzeituni wenye kusitawi,

Wenye kupendeza na wenye matunda ya muzuri.

Kwa sauti ya mungurumo mukubwa, amemuwasha moto,

Na wamevunja matawi yake.

17 “Yehova wa majeshi, Mupandaji wako,+ ametangaza kwamba musiba utakuja juu yako kwa sababu ya uovu wenye ulifanywa na nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda, wenye wamenikasirisha kwa kumutolea Baali zabihu.”+

18 Yehova alinijulisha ili nijue;

Wakati huo ulinifanya nione mambo yenye walikuwa wanafanya.

19 Nilikuwa kama mwana-kondoo mutulivu mwenye kuletwa kwenye machinjo.

Sikujua kwamba walikuwa wanapanga mupango mubaya juu yangu:+

“Tuharibu muti na matunda yake,

Na tumuondoe katika inchi ya wazima,

Ili jina lake lisikumbukwe tena.”

20 Lakini Yehova wa majeshi anahukumu kwa haki;

Anachunguza mawazo ya ndani kabisa* na moyo.+

Acha nione kisasi chako juu yao,

Kwa maana nimeleta kesi yangu ya hukumu kwako.

21 Kwa hiyo Yehova anasema hivi juu ya watu wa Anatoti+ wenye wanataka kuondoa uzima wako* na wenye wanasema: “Haupaswe kutoa unabii katika jina la Yehova,+ ao utakufa kwa mukono wetu”; 22 kwa hiyo Yehova wa majeshi anasema hivi: “Angalia, nitawaomba watoe hesabu. Vijana watakufa kwa upanga,+ na watoto wao wanaume na watoto wao wanamuke watakufa kwa njaa.+ 23 Hakuna hata mabaki wenye wataachwa kati yao, kwa sababu nitaleta musiba juu ya watu wa Anatoti+ katika mwaka wao wa kuombwa hesabu.”

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine