Yeremia
12 Wewe ni mwenye haki, Ee Yehova,+ wakati ninakuletea lalamiko langu,
Wakati ninasema na wewe juu ya mambo ya haki.
Lakini sababu gani njia ya waovu imefanikiwa,+
Na sababu gani wadanganyifu hawana wasiwasi?
2 Uliwapanda, na wametia mizizi.
Wamekomaa na kuzaa matunda.
Wewe uko kwenye midomo yao, lakini mbali na mawazo yao ya ndani kabisa.*+
3 Lakini unanijua muzuri, Ee Yehova,+ unaniona;
Umechunguza moyo wangu na kuupata ukiwa katika umoja na wewe.+
Uwaweke peke yao kama kondoo wa kuchinjwa,
Na uwatie pembeni kwa ajili ya siku ya kuuawa.
4 Inchi itaendelea kukauka mupaka wakati gani
Na majani ya kila eneo la mashamba kukauka?+
Kwa sababu ya uovu wa wale wenye kukaa ndani yake,
Wanyama na ndege wamefagiliwa mbali.
Kwa maana wamesema: “Haone kile chenye kitatupata.”
5 Kama unachoka kwa kukimbia pamoja na watu wenye kuenda kwa miguu,
Namna gani unaweza kushindana mbio na farasi?+
Hata kama uko na uhakika katika inchi ya amani,
Itakuwa namna gani kwako kati ya miti mingi midogo-midogo* pembeni ya Yordani?
6 Kwa maana hata ndugu zako mwenyewe, nyumba ya baba yako mwenyewe,
Wamekutendea kwa udanganyifu.+
Wamekulalamikia wakiita ubaya juu yako.
Usiwaamini,
Hata kama wanakuambia mambo ya muzuri.
7 “Nimeacha nyumba yangu;+ nimeacha uriti wangu.+
Nimetia mupendwa wangu* katika mukono wa maadui wake.+
8 Uriti wangu umekuwa kwangu kama simba katika pori.
Ameningurumia.
Basi nimemuchukia.
9 Uriti wangu ni kama ndege mwenye kuwinda, mwenye rangi nyingi;*
Ndege wengine wenye kuwinda wanamuzunguka na kumushambulia.+
Mukuje, mukusanyike pamoja, ninyi wote wanyama wa pori,
Mukuje mukule.+
Wamegeuza fungu langu la udongo lenye kutamanika kuwa jangwa lenye limeachwa ukiwa.
Inchi yote imeachwa ukiwa,
Lakini hakuna mutu mwenye kutia jambo hilo katika moyo.+
12 Wenye kuharibu wamekuja kwenye njia zote za kidogo-kidogo zenye zimekanyangwa sana,
Kwa maana upanga wa Yehova unameza kuanzia mwisho mumoja wa inchi mupaka mwisho mwingine.+
Hakuna amani kwa mutu yeyote.*
13 Wamepanda ngano, lakini wamevuna miiba.+
Wamejichokesha, lakini bila faida yoyote.
Watasikia haya kwa sababu ya mazao yao
Kwa sababu ya kasirani ya Yehova yenye kuwaka.”
14 Yehova anasema hivi juu ya majirani wangu wote waovu, wenye wanagusa uriti wenye nilifanya watu wangu Israeli wakuwe nao:+ “Angalia, ninawangoa kutoka kwenye inchi yao,+ na nitangoa nyumba ya Yuda kutoka kati yao. 15 Lakini kisha kuwangoa, nitawaonyesha tena rehema na kurudisha kila mumoja wao kwenye uriti wake na kwenye udongo wake.”
16 “Na kama kwa hakika wanajifunza njia za watu wangu na kuapa kwa jina langu, ‘Kama vile hakika Yehova anaishi!’ kama vile walifundisha watu wangu kuapa kwa jina la Baali, basi watajengwa kati ya watu wangu. 17 Lakini kama wanakataa kutii, mimi pia nitangoa taifa hilo, nitalingoa na kuliharibu,” ni vile Yehova anasema.+