Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 11
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Ezekieli

      • Wakubwa waovu wanalaumiwa (1-13)

        • Muji unalinganishwa na chungu cha kupikia (3-12)

      • Ahadi ya kurudishwa (14-21)

        • Wanapewa “roho mupya” (19)

      • Utukufu wa Yehova unaondoka Yerusalemu (22, 23)

      • Ezekieli anarudia Ukaldayo katika maono (24, 25)

Ezekieli 11:1

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 10:19
  • +Isa 1:23; Eze 22:27

Ezekieli 11:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “juu ya.”

Ezekieli 11:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Yeye,” muji wa Yerusalemu, kwenye Wayahudi walifikiri watalindwa.

  • *

    Ao “chungu cha kupikia chenye mudomo mukubwa.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 12:27
  • +Eze 24:3

Ezekieli 11:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 3:17; 20:46; 21:2

Ezekieli 11:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mambo yenye kuja katika roho yenu.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Pe. 1:21

Ezekieli 11:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 7:23; 22:3, 4

Ezekieli 11:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 24:6

Ezekieli 11:8

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 38:19

Ezekieli 11:9

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 39:6, 7; 52:24-27

Ezekieli 11:10

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 25:18-21; 2Nya 36:17
  • +2 Fal. 14:25; Yer 52:27
  • +Eze 6:13

Ezekieli 11:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Ezr 9:7; Ne 9:34
  • +Kum 12:29-31; 2Nya 28:1, 3; Zab 106:34-36

Ezekieli 11:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 9:8

Ezekieli 11:16

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 24:14, 15; Yer 24:5
  • +Law. 26:44

Ezekieli 11:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 11:11, 12; Yer 30:10, 11; Eze 34:13, 14; Amo 9:14, 15

Ezekieli 11:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 37:23

Ezekieli 11:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “moyo mumoja.”

  • *

    Ni kusema, moyo wenye kutii muongozo wa Mungu.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 24:7; 31:33; 32:39
  • +Zab 51:10; Eze 36:31
  • +Zek 7:12
  • +Eze 36:26

Ezekieli 11:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mipeto; pneus.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 1:19
  • +Eze 10:18, 19

Ezekieli 11:23

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 9:3; 10:4
  • +Zek 14:4

Maandiko ingine

Eze. 11:1Eze 10:19
Eze. 11:1Isa 1:23; Eze 22:27
Eze. 11:3Eze 12:27
Eze. 11:3Eze 24:3
Eze. 11:4Eze 3:17; 20:46; 21:2
Eze. 11:52 Pe. 1:21
Eze. 11:6Eze 7:23; 22:3, 4
Eze. 11:7Eze 24:6
Eze. 11:8Yer 38:19
Eze. 11:9Yer 39:6, 7; 52:24-27
Eze. 11:102 Fal. 25:18-21; 2Nya 36:17
Eze. 11:102 Fal. 14:25; Yer 52:27
Eze. 11:10Eze 6:13
Eze. 11:12Ezr 9:7; Ne 9:34
Eze. 11:12Kum 12:29-31; 2Nya 28:1, 3; Zab 106:34-36
Eze. 11:13Eze 9:8
Eze. 11:162 Fal. 24:14, 15; Yer 24:5
Eze. 11:16Law. 26:44
Eze. 11:17Isa 11:11, 12; Yer 30:10, 11; Eze 34:13, 14; Amo 9:14, 15
Eze. 11:18Eze 37:23
Eze. 11:19Yer 24:7; 31:33; 32:39
Eze. 11:19Zab 51:10; Eze 36:31
Eze. 11:19Zek 7:12
Eze. 11:19Eze 36:26
Eze. 11:22Eze 1:19
Eze. 11:22Eze 10:18, 19
Eze. 11:23Eze 9:3; 10:4
Eze. 11:23Zek 14:4
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Ezekieli 11:1-25

Ezekieli

11 Na roho ikaniinua na kunileta kwenye mulango mukubwa wa mashariki wa nyumba ya Yehova, mulango mukubwa wenye kuelekea mashariki.+ Pale kwenye muingilio wa mulango mukubwa niliona wanaume makumi mbili na tano (25), na kati yao kulikuwa Yaazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, wakubwa wa watu.+ 2 Kisha Yeye akaniambia: “Mwana wa binadamu, hawa ndio wanaume wenye kupanga uovu na kutoa shauri la mubaya katika* muji huu. 3 Wanasema, ‘Je, huu hauko wakati wa kujenga nyumba?+ Muji* ni chungu cha kupikia,*+ na sisi ni nyama.’

4 “Basi toa unabii juu yao. Toa unabii, mwana wa binadamu.”+

5 Kisha roho ya Yehova ikakuja juu yangu,+ naye akaniambia: “Sema, ‘Yehova anasema hivi: “Mambo yenye mumesema ni kweli, Ee nyumba ya Israeli, na ninajua kile munafikiria.* 6 Mumewafanya wengi wakufe katika muji, na mumejaza wafu katika barabara zake.”’”+ 7 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Maiti zenye mumesambaza katika muji ndizo nyama, na muji ni chungu cha kupikia.+ Lakini ninyi wenyewe mutaondolewa ndani yake.’”

8 “‘Mumeogopa upanga,+ na ni upanga ndio nitaleta juu yenu,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema. 9 ‘Nitawatosha ninyi ndani yake na kuwatia katika mukono wa wageni na kuleta hukumu juu yenu.+ 10 Mutaanguka kwa upanga.+ Nitawahukumu kwenye mupaka wa Israeli,+ na mutalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+ 11 Muji hautakuwa chungu chenu cha kupikia, na hamutakuwa nyama yenye kuwa ndani yake; nitawahukumu ninyi kwenye mupaka wa Israeli, 12 na mutalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova. Kwa maana hamukutembea katika masharti yangu wala kutenda hukumu zangu,+ lakini mumetenda kulingana na hukumu za mataifa yenye kuwazunguka.’”+

13 Wakati tu nilitoa unabii, Pelatia mwana wa Benaya akakufa, na mimi nikaanguka uso chini na kulia kwa sauti kubwa: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova! Je, utaharibu wale wenye watabakia wa Israeli?”+

14 Neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 15 “Mwana wa binadamu, ndugu zako, wamoja kati ya ndugu zako wenye wako na haki ya kukomboa, pamoja na nyumba yote ya Israeli, wameambiwa na wakaaji wa Yerusalemu, ‘Mubakie mbali na Yehova. Inchi ni yetu; tumepewa ili tuiriti.’ 16 Kwa hiyo sema, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Hata kama nimewapeleka mbali kabisa kati ya mataifa, na nimewasambaza kati ya inchi hizo,+ kwa wakati kidogo nitakuwa patakatifu kwa ajili yao katika inchi kwenye wameenda.”’+

17 “Kwa hiyo sema, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Pia nitawakusanya ninyi kutoka kwa vikundi vya watu na kuwakusanya kutoka katika inchi mbalimbali kwenye mumesambazwa, na nitawapatia inchi ya Israeli.+ 18 Nao watarudia kule na kuondoa vitu vyake vyote vyenye kuchukiza na mazoea yake yenye kuchukiza.+ 19 Na nitawapatia moyo wenye kuunganishwa,*+ na nitatia roho mupya ndani yao;+ na nitaondoa moyo wa jiwe katika miili yao+ na kuwapatia moyo wa nyama,*+ 20 ili watembee katika sheria zangu na kushika hukumu zangu na kuzitii. Kisha watakuwa watu wangu, na mimi nitakuwa Mungu wao.”’

21 “‘“Lakini kuhusu wale wenye mioyo yao imeazimia kuendelea katika vitu vyao vyenye kuchukiza na mazoea yao yenye kuchukiza, nitaleta matokeo ya njia yao juu ya kichwa chao,” ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.’”

22 Sasa wale makerubi wakainua mabawa yao, na yale magurudumu* yalikuwa karibu nao,+ na utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.+ 23 Kisha utukufu wa Yehova+ ukapanda kutoka katika muji na kusimama juu ya mulima wenye ulikuwa upande wa mashariki wa muji huo.+ 24 Kisha roho ikaniinua​—⁠kupitia maono kwa roho ya Mungu​—⁠na kunileta kwa watu wenye walikuwa katika uhamisho kule Ukaldayo. Halafu maono yenye nilikuwa nimeona yakaisha. 25 Na nikaanza kuambia watu wenye walikuwa katika uhamisho mambo yote yenye Yehova alikuwa amenionyesha.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine