Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 12
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Ezekieli

      • Uhamisho unatabiriwa kupitia mifano (1-20)

        • Mizigo kwa ajili ya uhamisho (1-7)

        • Mukubwa ataondoka katika giza (8-16)

        • Mukate wa mahangaiko, maji ya woga mukubwa (17-20)

      • Usemi wa udanganyifu unaonyeshwa kuwa wa uongo (21-28)

        • “Hakuna neno moja kati ya maneno yangu lenye litacheleweshwa” (28)

Ezekieli 12:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 6:9, 10; Yer 5:21; Rom. 11:8
  • +Eze 2:3, 5

Ezekieli 12:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 36:20; Yer 52:10, 11

Ezekieli 12:5

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 25:4

Ezekieli 12:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 8:18; Eze 4:3; 24:24

Ezekieli 12:10

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 21:7; Eze 21:25

Ezekieli 12:11

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 24:24
  • +Yer 52:15

Ezekieli 12:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 25:4; Yer 39:4

Ezekieli 12:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “makila yangu.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 52:9; Eze 17:20, 21
  • +2 Fal. 25:6, 7; Yer 34:3; 52:11; Eze 17:16

Ezekieli 12:14

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 25:5
  • +Law. 26:33; Yer 42:15, 16

Ezekieli 12:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 26:26

Ezekieli 12:19

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 6:11; Zek 7:14
  • +Zab 107:33, 34; Yer 6:7

Ezekieli 12:20

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 64:10; Yer 25:9
  • +Eze 6:13

Ezekieli 12:22

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 5:19; Amo 6:3; 2 Pe. 3:3, 4

Ezekieli 12:23

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yoe 2:1; Sef 1:14

Ezekieli 12:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “udanganyifu.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 14:14; Omb 2:14; Eze 13:23

Ezekieli 12:25

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Omb 2:17; Zek 1:6
  • +Yer 16:9; Hab 1:5

Ezekieli 12:27

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “nyumba ya.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 5:19; 28:15; 2 Pe. 3:3, 4

Maandiko ingine

Eze. 12:2Isa 6:9, 10; Yer 5:21; Rom. 11:8
Eze. 12:2Eze 2:3, 5
Eze. 12:42Nya 36:20; Yer 52:10, 11
Eze. 12:52 Fal. 25:4
Eze. 12:6Isa 8:18; Eze 4:3; 24:24
Eze. 12:10Yer 21:7; Eze 21:25
Eze. 12:11Eze 24:24
Eze. 12:11Yer 52:15
Eze. 12:122 Fal. 25:4; Yer 39:4
Eze. 12:13Yer 52:9; Eze 17:20, 21
Eze. 12:132 Fal. 25:6, 7; Yer 34:3; 52:11; Eze 17:16
Eze. 12:142 Fal. 25:5
Eze. 12:14Law. 26:33; Yer 42:15, 16
Eze. 12:18Law. 26:26
Eze. 12:19Isa 6:11; Zek 7:14
Eze. 12:19Zab 107:33, 34; Yer 6:7
Eze. 12:20Isa 64:10; Yer 25:9
Eze. 12:20Eze 6:13
Eze. 12:22Isa 5:19; Amo 6:3; 2 Pe. 3:3, 4
Eze. 12:23Yoe 2:1; Sef 1:14
Eze. 12:24Yer 14:14; Omb 2:14; Eze 13:23
Eze. 12:25Omb 2:17; Zek 1:6
Eze. 12:25Yer 16:9; Hab 1:5
Eze. 12:27Isa 5:19; 28:15; 2 Pe. 3:3, 4
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Ezekieli 12:1-28

Ezekieli

12 Neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, unaishi katika nyumba yenye kuasi. Wako na macho ya kuona, lakini hawaone, na masikio ya kusikia, lakini hawasikie,+ kwa maana wao ni nyumba yenye kuasi.+ 3 Sasa wewe, mwana wa binadamu, ujitayarishie mizigo kwa ajili ya kuenda katika uhamisho. Kisha, muchana wakati wako wanaangalia, unapaswa kuenda katika uhamisho. Toka katika nyumba yako na uende katika uhamisho mahali pengine wakiwa wanaangalia. Pengine wataona, hata kama wao ni nyumba yenye kuasi. 4 Tia inje mizigo yako yenye imefungwa kwa ajili ya kuenda katika uhamisho muchana wakiwa wanaangalia, na halafu mangaribi wakiwa wanaangalia, utaondoka kama vile mutu mwenye kupelekwa katika uhamisho.+

5 “Wakiwa wanaangalia, toboa tundu katika ukuta, na ubebe vitu vyako na kupita katika tundu hilo.+ 6 Wakiwa wanaangalia, tia vitu vyako kwenye bega lako na uondoke na vitu hivyo katika giza. Funika uso wako ili usiweze kuona chini, kwa maana ninakufanya kuwa alama kwa nyumba ya Israeli.”+

7 Nikafanya kama vile niliamuriwa. Nikatia mizigo yangu inje wakati wa muchana kama vile mizigo ya kuenda katika uhamisho, na mangaribi nikatoboa tundu katika ukuta kwa mukono. Na wakati kulikuwa giza, nilikamata vitu vyangu, nikavibeba kwenye bega langu mbele ya macho yao.

8 Asubui neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 9 “Mwana wa binadamu, je, nyumba ya Israeli, nyumba yenye kuasi, hawakukuuliza, ‘Unafanya nini?’ 10 Uwaambie, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Tangazo hili linamuhusu mukubwa+ katika Yerusalemu na nyumba yote ya Israeli ndani ya muji.”’

11 “Sema, ‘Mimi ni alama kwenu.+ Kama vile nimetenda, ni vile watatendewa. Wataenda katika uhamisho, katika utekwa.+ 12 Mukubwa mwenye kuwa kati yao atabeba vitu vyake kwenye bega lake na kuondoka katika giza. Atatoboa tundu katika ukuta na kubeba vitu vyake na kupita katika tundu hilo.+ Atafunika uso wake ili asiweze kuona chini.’ 13 Nitatandika wavu wangu* juu yake, naye atakamatwa katika wavu wangu wa kuwindia.+ Kisha nitamupeleka Babiloni, kwenye inchi ya Wakaldayo, lakini hataiona; na atakufa kule.+ 14 Na wote wenye kumuzunguka, wasaidizi wake na wanajeshi wake, nitawasambaza kila upande;+ na nitachomoa upanga ili kuwafuatilia.+ 15 Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova wakati nitawasambaza kati ya mataifa na kuwatawanya kati ya inchi hizo. 16 Lakini nitalinda watu kidogo kati yao kutokana na upanga, njaa, na ugonjwa wa kuambukiza, ili wasimulie kuhusu mazoea yao yote yenye kuchukiza kati ya mataifa kwenye wataenda; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”

17 Na neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 18 “Mwana wa binadamu, unapaswa kula mukate wako kwa kutetemeka na ukunywe maji yako kwa kufazaika na kuhangaika.+ 19 Ambia watu wa inchi, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anaambia wakaaji wa Yerusalemu katika inchi ya Israeli hivi: “Watakula mukate wao kwa kuhangaika na kunywa maji yao kwa kuogopa sana, kwa maana inchi yao itakuwa ukiwa kabisa+ kwa sababu ya jeuri ya wale wote wenye kukaa ndani yake.+ 20 Miji yenye kuikaliwa na watu itaharibiwa, na inchi itakuwa eneo lenye limeachwa;+ na mutalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”’”+

21 Na neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 22 “Mwana wa binadamu, ni mezali gani hii yenye muko nayo katika Israeli yenye inasema, ‘Siku zinapita, na hakuna maono yenye kutimia’?+ 23 Kwa hiyo uwaambie, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Nitafanya usemi huu usikuwe tena, na hawatautumia tena kama mezali katika Israeli.”’ Lakini uwaambie, ‘Siku zimekaribia,+ na maono yote yatatimia.’ 24 Kwa maana hakutakuwa tena maono ya uongo wala uaguzi wa kusifu-sifu* katika nyumba ya Israeli.+ 25 ‘“Kwa maana mimi Yehova, nitasema. Neno lolote lenye nitasema litafanywa bila kuchelewa tena.+ Katika siku zenu,+ Ee nyumba yenye kuasi, nitasema neno na kulitimiza,” ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.’”

26 Neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 27 “Mwana wa binadamu, ni hivi watu wa* Israeli wanasema: ‘Maono yenye anaona ni ya wakati murefu kuanzia sasa, na anatoa unabii kuhusu wakati wenye kuja wenye kuwa mbali.’+ 28 Kwa hiyo uwaambie, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “‘Hakuna neno moja kati ya maneno yangu lenye litacheleweshwa; kitu chochote chenye nitasema kitafanywa,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.”’”

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine