Kwa Waroma
13 Kila mutu ajitiishe* kwa mamlaka zenye kuwa kubwa,+ kwa maana hakuna mamlaka isipokuwa kwa ruhusa ya Mungu;+ mamlaka zenye ziko zimewekwa na Mungu katika vyeo vyao vya kadiri.+ 2 Kwa hiyo, mutu yeyote mwenye anapinga mamlaka amepinga mupango wa Mungu; wale wenye wameupinga watajiletea hukumu wao wenyewe. 3 Kwa maana wale watawala ni kitu cha kuogopesha, hapana kwa tendo la muzuri, lakini kwa tendo la mubaya.+ Je, unataka usiogope mamlaka? Endelea kufanya mambo ya muzuri,+ na itakusifu wewe; 4 kwa maana hiyo ni mutumishi wa Mungu kwako kwa faida yako. Lakini kama unafanya mambo ya mubaya, ogopa, kwa maana haibebe upanga bila sababu. Hiyo ni mutumishi wa Mungu, mulipiza-kisasi ili kuonyesha kasirani kali* juu ya ule mwenye anazoea kufanya mambo ya mubaya.
5 Kwa hiyo kuko sababu ya lazima kwenu kujitiisha, haiko kwa sababu ya ile kasirani kali tu, lakini pia kwa sababu ya zamiri yenu.+ 6 Ndiyo sababu munalipa kodi pia; kwa maana wao ni watumishi wa Mungu kwa watu wote, na wanatumika bila kuacha kwa kusudi hili. 7 Mupatie wote haki zao: ule mwenye anataka kodi, kodi;+ ule mwenye anataka ushuru, ushuru; ule mwenye anataka woga, woga;+ ule mwenye anataka heshima, heshima.+
8 Musikuwe na deni lolote kwa mutu yeyote isipokuwa kupendana;+ kwa maana kila mutu mwenye anamupenda mwanadamu mwenzake ametimiza sheria.+ 9 Kwa maana sheria zenye kusema, “Haupaswe kufanya uzinifu,+ haupaswe kuua,+ haupaswe kuiba,+ haupaswe kutamani,”+ na amri ingine yoyote yenye iko, zinatajwa kwa kifupi katika maneno haya: “Unapaswa kumupenda jirani yako kama wewe mwenyewe.”+ 10 Upendo haumufanyie jirani mambo ya mubaya;+ kwa hiyo, upendo ndio utimizo wa sheria.+
11 Na mufanye hivi kwa sababu munajua kipindi hiki, kwamba tayari ni saa ya ninyi kuamuka kutoka katika usingizi,+ kwa maana sasa wokovu wetu uko karibu kuliko wakati tulianza kuamini. 12 Usiku umeendelea sana; muchana umekaribia. Kwa hiyo, tutupe matendo ya giza+ na tuvae silaha za mwangaza.+ 13 Tutembee kwa adabu+ kama wakati wa muchana, hapana katika karamu za kupitisha mipaka na ulevi, hapana katika uasherati na mwenendo mupotovu wa bila haya,*+ hapana katika mizozo na wivu.+ 14 Lakini muvae Bwana Yesu Kristo,+ na musikuwe munapanga mbele ya wakati kwa ajili ya tamaa za mwili.+