Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 15:14-16
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 14 Vikundi vya watu vitasikia+ na kutetemeka;

      Wakaaji wa Ufilisti watashikwa na uchungu.*

      15 Wakati huo mashehe* wa Edomu wataogopa sana,

      Na kutetemeka kutashika watawala wenye nguvu* wa Moabu.+

      Wakaaji wote wa Kanaani watavunjika moyo.+

      16 Woga na hofu vitaanguka juu yao.+

      Kwa sababu ya mukono wako wenye nguvu watabakia bila kutikisika kama jiwe

      Mupaka watu wako wapite, Ee Yehova,

      Mupaka watu wenye ulitokeza+ wapite.+

  • Yoshua 2:9-11
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 9 Akawaambia: “Ninajua kwamba Yehova atawapatia inchi hii+ na tumeogopa kwa sababu yenu.+ Wakaaji wote wa inchi wamevunjika moyo kwa sababu yenu,+ 10 kwa maana tulisikia namna Yehova alikausha maji ya Bahari Nyekundu mbele yenu wakati mulitoka Misri+ na mambo yenye mulitendea wale wafalme wawili wa Waamori, Sihoni+ na Ogu,+ wenye muliharibu kabisa ngambo ingine ya* Yordani. 11 Wakati tulisikia kuhusu mambo hayo, mioyo yetu ilizimia kwa sababu ya woga,* na hakuna mwenye alikuwa na uhodari wowote kwa sababu yenu, kwa maana Yehova Mungu wenu ni Mungu juu mbinguni na chini duniani.+

  • Yoshua 5:1
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 5 Wakati tu wafalme wote wa Waamori+ wenye walikuwa upande wa mangaribi* wa Yordani na wafalme wote wa Wakanaani+ wenye walikuwa karibu na bahari walisikia kwamba Yehova alikausha maji ya Yordani mbele ya Waisraeli mupaka wakati walimaliza kuvuka, wakavunjika moyo*+ na hawakukuwa na uhodari wowote kwa sababu ya Waisraeli.+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine