Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 49:10
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 10 Fimbo ya ufalme haitatoka kwa Yuda,+ wala fimbo ya kamanda kutoka katikati ya miguu yake, mupaka wakati Shilo* atakuja,+ na vikundi vya watu vitamutii yeye.+

  • 1 Wafalme 8:20
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 20 Yehova ametimiza ahadi yenye alitoa, kwa maana nimechukua nafasi ya baba yangu Daudi na ninakaa kwenye kiti cha ufalme cha Israeli, kama vile Yehova aliahidi. Nimejenga pia nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wa Israeli+

  • 1 Mambo ya Nyakati 17:11-14
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 11 “‘“Wakati siku zako zitafikia mwisho na uende kuwa pamoja na mababu zako, nitainua uzao wako* kisha wewe, mumoja wa wana wako,+ na nitafanya ufalme wake ukuwe imara kabisa.+ 12 Yeye ndiye atanijengea nyumba,+ na nitafanya imara kabisa kiti chake cha ufalme milele.+ 13 Nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwana wangu.+ Sitaondoa upendo wangu mushikamanifu kwake+ kama vile niliuondoa kwa ule mwenye alikutangulia.+ 14 Nitamufanya asimame katika nyumba yangu na katika ufalme wangu milele,+ na kiti chake cha ufalme kitadumu milele.”’”+

  • Zaburi 132:11
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 11 Yehova amemuapia Daudi;

      Hakika hatakosa kutimiza neno lake:

      “Mumoja wa wazao wako,*

      Nitamutia kwenye kiti chako cha ufalme.+

  • Isaya 9:7
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    •  7 Kuongezeka kwa utawala wake*

      Na amani, havitakuwa na mwisho,+

      Kwenye kiti cha ufalme cha Daudi+ na juu ya ufalme wake

      Ili kuufanya kuwa imara kabisa+ na kuutegemeza

      Kupitia haki+ na uadilifu,*+

      Kuanzia sasa na milele.

      Bidii ya Yehova wa majeshi itatenda mambo hayo.

  • Isaya 11:1
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 11 Na tawi+ litakomaa kutoka kwenye kisiki cha Yese,+

      Na chipukizi+ kutoka kwenye mizizi yake litazaa matunda.

  • Matayo 21:9
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 9 Zaidi ya hilo, watu wengi wenye walikuwa mbele yake na wale wenye walikuwa wanamufuata wakaendelea kusema kwa sauti kubwa: “Okoa, tunaomba, Mwana wa Daudi!+ Amebarikiwa ule mwenye anakuja katika jina la Yehova!*+ Umuokoe, tunaomba, wewe mwenye kuwa kwenye nafasi za juu!”+

  • Matayo 22:42
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 42 “Munawaza nini juu ya Kristo? Yeye ni mwana wa nani?” Wakamuambia: “Wa Daudi.”+

  • Luka 1:32, 33
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 32 Huyo atakuwa mukubwa+ na ataitwa Mwana wa Mwenye Kuwa Juu Zaidi;+ na Yehova* Mungu atamupatia kiti cha ufalme cha Daudi baba yake,+ 33 na atatawala akiwa Mufalme juu ya nyumba ya Yakobo milele, na Ufalme wake hautakuwa na mwisho.”+

  • Yohana 7:42
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 42 Je, andiko haliseme kwamba Kristo anakuja kutoka katika uzao wa Daudi+ na kutoka katika Betlehemu,+ kijiji kwenye Daudi alikuwa?”+

  • Matendo 2:30
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 30 Kwa sababu alikuwa nabii na alijua kwamba Mungu alikuwa amemuapia kwa kiapo kwamba ataikalisha mumoja kati ya wazao wake* kwenye kiti chake cha ufalme,+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine