-
1 Wafalme 8:20Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
20 Yehova ametimiza ahadi yenye alitoa, kwa maana nimechukua nafasi ya baba yangu Daudi na ninakaa kwenye kiti cha ufalme cha Israeli, kama vile Yehova aliahidi. Nimejenga pia nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wa Israeli+
-
-
1 Mambo ya Nyakati 17:11-14Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
11 “‘“Wakati siku zako zitafikia mwisho na uende kuwa pamoja na mababu zako, nitainua uzao wako* kisha wewe, mumoja wa wana wako,+ na nitafanya ufalme wake ukuwe imara kabisa.+ 12 Yeye ndiye atanijengea nyumba,+ na nitafanya imara kabisa kiti chake cha ufalme milele.+ 13 Nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwana wangu.+ Sitaondoa upendo wangu mushikamanifu kwake+ kama vile niliuondoa kwa ule mwenye alikutangulia.+ 14 Nitamufanya asimame katika nyumba yangu na katika ufalme wangu milele,+ na kiti chake cha ufalme kitadumu milele.”’”+
-
-
Zaburi 132:11Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
11 Yehova amemuapia Daudi;
Hakika hatakosa kutimiza neno lake:
-
-
Matayo 22:42Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
42 “Munawaza nini juu ya Kristo? Yeye ni mwana wa nani?” Wakamuambia: “Wa Daudi.”+
-