Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 19:4
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 4 Kwa hiyo Yonatani akazungumuza muzuri na Sauli baba yake kumuhusu Daudi.+ Akamuambia: “Mufalme hapaswe kumutendea zambi mutumishi wake Daudi kwa sababu yeye hajakutendea zambi na mambo yenye amekufanyia yamekuletea faida.

  • 1 Samweli 25:23, 24
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 23 Wakati Abigaili alimuona Daudi, akashuka haraka kutoka juu ya punda na kujiangusha uso chini mbele ya Daudi, na akainama chini. 24 Kisha akaanguka kwenye miguu yake na kusema: “Bwana wangu, acha lawama ikuwe juu yangu; acha mutumishi wako mwanamuke azungumuze na wewe, na usikilize maneno ya mutumishi wako mwanamuke.

  • Esta 4:13, 14
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 13 akamujibu Esta: “Usiwaze kwamba kwa sababu uko katika nyumba ya mufalme utaponyoka kuliko Wayahudi wengine wote. 14 Kwa maana ukinyamaza wakati huu, Wayahudi watapata kitulizo na ukombozi kutoka chanzo kingine,+ lakini wewe na nyumba ya baba yako mutaangamia. Na ni nani anajua ikiwa haiko kwa ajili ya wakati kama huu ndiyo maana umefikia cheo chako cha kifalme?”+

  • Zaburi 145:11
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 11 Watatangaza utukufu wa ufalme wako+

      Na kusema kuhusu nguvu zako,+

  • Mezali 9:8
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    •  8 Usimukaripie mutu mwenye zihaka, kwa maana atakuchukia.+

      Karipia mwenye hekima, naye atakupenda.+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine