-
1 Samweli 19:4Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
4 Kwa hiyo Yonatani akazungumuza muzuri na Sauli baba yake kumuhusu Daudi.+ Akamuambia: “Mufalme hapaswe kumutendea zambi mutumishi wake Daudi kwa sababu yeye hajakutendea zambi na mambo yenye amekufanyia yamekuletea faida.
-
-
1 Samweli 25:23, 24Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
23 Wakati Abigaili alimuona Daudi, akashuka haraka kutoka juu ya punda na kujiangusha uso chini mbele ya Daudi, na akainama chini. 24 Kisha akaanguka kwenye miguu yake na kusema: “Bwana wangu, acha lawama ikuwe juu yangu; acha mutumishi wako mwanamuke azungumuze na wewe, na usikilize maneno ya mutumishi wako mwanamuke.
-
-
Esta 4:13, 14Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
13 akamujibu Esta: “Usiwaze kwamba kwa sababu uko katika nyumba ya mufalme utaponyoka kuliko Wayahudi wengine wote. 14 Kwa maana ukinyamaza wakati huu, Wayahudi watapata kitulizo na ukombozi kutoka chanzo kingine,+ lakini wewe na nyumba ya baba yako mutaangamia. Na ni nani anajua ikiwa haiko kwa ajili ya wakati kama huu ndiyo maana umefikia cheo chako cha kifalme?”+
-