Cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati
3 Hawa ndio walikuwa wana wa Daudi wenye alizaa katika Hebroni:+ Amnoni muzaliwa wa kwanza,+ mama yake alikuwa Ahinoamu+ wa Yezreeli; wa pili, Danieli, mama yake alikuwa Abigaili+ Mukarmeli; 2 wa tatu (3), Absalomu,+ mwana wa Maaka binti ya Talmai mufalme wa Geshuri; wa ine (4), Adoniya+ mwana wa Hagiti; 3 wa tano (5), Shefatia, mama yake alikuwa Abitali; na wa sita (6), Itreamu, mama yake alikuwa Egla bibi ya Daudi. 4 Hao sita (6) aliwazaa katika Hebroni; alitawala kule kwa miaka saba (7) na miezi sita, na alitawala katika Yerusalemu kwa miaka makumi tatu na tatu (33).+
5 Hawa aliwazaa katika Yerusalemu:+ Shimea, Shobabu, Natani,+ na Sulemani;+ mama ya hao ine (4) alikuwa Bat-sheba+ binti ya Amieli. 6 Na wana wengine kenda (9) walikuwa Ibhari, Elishama, Elifeleti, 7 Noga, Nefegi, Yafia, 8 Elishama, Eliada, na Elifeleti. 9 Hao wote walikuwa wana wa Daudi, zaidi ya wana wa masuria,* na Tamari+ alikuwa dada yao.
10 Mwana wa Sulemani alikuwa Rehoboamu;+ Abiya+ alikuwa mwana wake, Asa+ mwana wake, Yehoshafati+ mwana wake, 11 Yehoramu+ mwana wake, Ahazia+ mwana wake, Yehoashi+ mwana wake, 12 Amazia+ mwana wake, Azaria+ mwana wake, Yotamu+ mwana wake, 13 Ahazi+ mwana wake, Hezekia+ mwana wake, Manase+ mwana wake, 14 Amoni+ mwana wake, Yosia+ mwana wake. 15 Wana wa Yosia walikuwa Yohanani muzaliwa wa kwanza, wa pili, Yehoyakimu,+ wa tatu (3), Sedekia,+ wa ine (4), Shalumu. 16 Wana wa Yehoyakimu walikuwa Yekonia+ mwana wake na Sedekia mwana wake. 17 Wana wa Yekonia mwenye alikuwa mufungwa walikuwa Shealtieli, 18 Malkiramu, Pedaya, Shenazari, Yekamia, Hoshama, na Nedabia. 19 Wana wa Pedaya walikuwa Zerubabeli+ na Shimei; na wana wa Zerubabeli walikuwa Meshulamu na Hanania (na Shelomiti alikuwa dada yao); 20 na wana wengine tano (5) walikuwa Hashuba, Oheli, Berekia, Hasadia, na Yushab-hesedi. 21 Na wana wa Hanania walikuwa Pelatia na Yeshaya; mwana* wa Yeshaya alikuwa Refaya; mwana* wa Refaya alikuwa Arnani; mwana* wa Arnani alikuwa Obadia; mwana* wa Obadia alikuwa Shekania; 22 na wana wa Shekania walikuwa Shemaya na wana wa Shemaya: Hatushi, Igali, Baria, Nearia, na Shafati—wote walikuwa sita (6). 23 Na wana wa Nearia walikuwa Elioenai, Hizkia, na Azrikamu, watatu (3). 24 Na wana wa Elioenai walikuwa Hodavia, Eliashibu, Pelaya, Akubu, Yohanani, Delaya, na Anani, saba (7).