Wimbo wa Safari za Kupanda.
121 Ninainua macho yangu kuelekea milima.+
Musaada wangu utatoka wapi?
2 Musaada wangu unatoka kwa Yehova,+
Mutengenezaji wa mbingu na dunia.
3 Hataruhusu hata kidogo muguu wako utereze.+
Yeye mwenye kukulinda hatasinzia hata kidogo.
4 Angalia! Hatasinzia hata kidogo wala kulala usingizi,
Yeye mwenye kulinda Israeli.+
5 Yehova anakulinda.
Yehova ni kivuli+ kwenye mukono wako wa kuume.+
6 Muchana, jua halitakupiga,+
Wala mwezi usiku.+
7 Yehova atakulinda na mambo yote yenye kuumiza.+
Atalinda uzima wako.+
8 Yehova atakulinda katika mambo yote yenye unafanya
Kuanzia sasa na milele.